Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
Shirika la afya duniani WHO, leo limeelezea wasiwasi kwamba mataifa tajiri yanayotishiwa na kuzuka kwa aina mpya ya kirusi cha Omicron huenda yakahodhi chanjo za ugonjwa wa COVID-19 na kutatiza usambazaji wa chanjo hizo kote duniani hali itakayotatiza juhudi za kukabiliana na janga hilo.
Mkuu wa idara ya chanjo na biolojia wa shirika hilo la WHO Daktari Kate O'Brien, amesema namna ya pekee ya kukabiliana na ugonjwa huo ni kwa kila mtu hasa katika maeneo yanayokabiliwa na hatari zaidi za maambukizo kuchomwa chanjo.
O'Brien ameongeza kuwa inaonekana kuwa lengo hilo limepuuzwa. Baada ya mkutano na wataalamu wake, shirika hilo lilisisitiza ushauri wake kwa mataifa dhidi ya matumizi makubwa ya chanjo za nyongeza kwa raia wake ili mataifa yenye chanjo zaidi badala yake yaweze kupeleka chanjo hizo kwa mataifa maskini ambayo yana nakisi kubwa ya chanjo hizo.
DW
Mkuu wa idara ya chanjo na biolojia wa shirika hilo la WHO Daktari Kate O'Brien, amesema namna ya pekee ya kukabiliana na ugonjwa huo ni kwa kila mtu hasa katika maeneo yanayokabiliwa na hatari zaidi za maambukizo kuchomwa chanjo.
O'Brien ameongeza kuwa inaonekana kuwa lengo hilo limepuuzwa. Baada ya mkutano na wataalamu wake, shirika hilo lilisisitiza ushauri wake kwa mataifa dhidi ya matumizi makubwa ya chanjo za nyongeza kwa raia wake ili mataifa yenye chanjo zaidi badala yake yaweze kupeleka chanjo hizo kwa mataifa maskini ambayo yana nakisi kubwa ya chanjo hizo.
DW