WHO yasema idadi ya maambukizi ya Corona hayatakuwa makubwa Afrika kama ilivyokadiriwa

WHO yasema idadi ya maambukizi ya Corona hayatakuwa makubwa Afrika kama ilivyokadiriwa

Besta Mlagila

Senior Member
Joined
May 29, 2018
Posts
101
Reaction score
191
Shirika la Afya Duniani (WHO) limetabiri kuwa idadi ya maambukizi ya virusi vya Corona barani Afrika haitakuwa kubwa kama ilivyokadiriwa na kilele chake pia kitachelewa kufika katika nchi nyingi za bara hilo kutokana na hatua madhubuti zilizochukuliwa kuzuia kuenea kwa virusi hivyo.

Mkurugenzi wa WHO kanda ya Afrika Bibi Matshidiso Moeti amesema utabiri uliotolewa na WHO ulionesha kuwa idadi ya wagonjwa wa virusi vya Corona barani Afrika itafikia kilele chake wiki tano baada ya mgonjwa wa kwanza kugunduliwa katika nchi moja ya Afrika na kwa wastani, asilimia 26 wa watu wote wa Afrika wangeweza kuambukizwa virusi hivyo.

Ameongeza kuwa utabiri huo ulifanywa katika msingi wa maambukizi kati ya watu na watu haswa katika maeneo ya vijijini, lakini hatua zinazochukuliwa na serikali za nchi za Afrika kama vile zuio nusu, umbali wa kijamii na kunawa mikono zimepunguza maambukizi ya virusi.

Ameongeza kuwa WHO inashirikiana na Tanzania, ambayo haijatangaza takwimu ya idadi ya wagonjwa tangu Aprili 29, kufanya hivyo ili kuandaa mpango mwafaka wa kukabiliana na virusi vya Corona.
 
Nitawaona hawa WHO Werevu kama tu wakiacha kututishia Waafrika na wakijikita zaidi katika kupambana kupatikana dawa.
 
Tunaambiwa AU kitengo cha corona imeiambia bongo kutoa takwimu, wewe unaleta mbwembwe za WhO inashirikiana na bongo, akili za kuambiwa changanya na zako
 
Africa huku mijitu inapata Corona afu inapona mumo kwa mumo!! Watakaondondoka ni wenye maradhi ya kudumu na wazee ambao kinga ni changamoto.

Africa tatizo letu sisi si Corona ni udikteta...yaani mtu anaifanya nchi kama sebureni kwake vile!! ...Remote zote kazishika yeye...akienda bafuni ana mute TV yaani hadi arudi.. atawasha apendavyo yeye na channel anayoangalia yeye ni lazima muangalie wote hutaki ondoka....na ukitoka sebureni getini hutoki kuna walinzi kama wote watakubabua balaa..haya ndiyo maisha ya mwafrica.

Uhuru wa habari, uhuru wa kutoa maoni, uhuru wa kukosoa watawala HAUPO KABISA.
 
Aibu imewarudia! Wazungu wamekufa sana ina maana tunawazidi kunawa? Waseme kweli kwamba mchezo wao tumeushtukia.
 
Africa huku mijitu inapata Corona afu inapona mumo kwa mumo!! Watakaondondoka ni wenye maradhi ya kudumu na wazee ambao kinga ni changamoto.

Africa tatizo letu sisi si Corona ni udikteta...yaani mtu anaifanya nchi kama sebureni kwake vile!! ...Remote zote kaishika yeye...akienda bafuni ana mute TV yaani hadi arudi anawaona apendavyo yeye....haya si maisha !!

Uhuru wa habari, uhuru wa kutoa maoni, uhuru wa kukosoa watawala HAUPO KABISA.
Nilikuwa sijui kumbe bara la africa linaongozwa na rais mmoja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizi habari zavijiweni sijui mnaziokotaga wapi? Wakati who wamesema maambukizi Africa yatakuwa mil 250+ na vivo mil 15+
 
Kwa taarifa kama hizi, msishangae kumwona kwenye mawe akipiga picha kwa kicheko cha kejeli.
 
Chadema mtaongea maneno mengi mpaka mnamaliza ila JPM yupo Strong.
 
Tanzania nadhani ina sifa tofauti sana, nimesoma mwanzo hadi mwisho nilijua inataja africa kwa ujumla lakini mwishoni imeitajwa Tanzania moja kwa moja
Tanzania imetoka kuwa kati ya nchi zile zilizokuwa mstari wa mbele barani Africa (Frontline countries) wakati fulani zikiongozwa na mwenyekiti Nyerere mpaka siku hizi kuwa moja ya nchi zilizo mstari wa nyuma barani Africa (Bachline countries) zikiongozwa na 🔒 🔒 .
 
Back
Top Bottom