Kamanda Kazi
JF-Expert Member
- Dec 15, 2012
- 2,613
- 795
Haya waambie wenzako aliyekufundisha hadithi hii na kama inatufundisha nini eeeh mtoto mzuri!!!???
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
- Hivi kweli mkuu ulihitaji kumjibu mtu anayetumwa tumwa kila siku kuchafua wanasiasa kwenye mitandao? Alisema Bunge la katiba linavunjwa na halikuvunjwa toka pale huwa siamini anything anachosema huwa anatumwa na wanasiasa kumjibu ni kumpa ujiko wa bure mkuu nex time ni kumjibu kwenye thread yake, kumjibu like this unampa ujiko wa bure mkuu sasa kweli gazeti la mawio unaweza kulihesabu kuwa ni gazeti ofisi zake zipo wapi kama sio mtaani, please!!
Le Mutuz
Membe pia anategemea mbeleko ya Mama Salma kwenye urais.
Ndugu yangu YERIKO NYERERE
kadiri unavyozidi kuleta thread zako ndivyo unavyoharibu image yako hapa JF. mimi ni mwenzako kiitikadi lakini,kuna vitu huwa sikukubali hata kidogo,Lengo la andiko lako kumkashifu Membe halina maana,Namupa Seminary yenyewe huijui,unasikia tu,aliyeanzisha Namupa Seminary humfahamu una depend kwenye hearsay oh ! mara dawati la tatu toka wapi? kwa nani? kwa nani? halafu huyo padre unayemtaja Mariano sijui wa wapi Lindi hatuna padre huyo wala kama alikuwa ni Mbenediktini mmisionari hayupo tena,Kifupi wewe ni muongo hujui chochote kuhusu membe hasa maisha yake ya Useminari Namupa! Fanya tafiti kwanza halafu uje na data za maana.
Matamko aliyoyatoa Membe juu ya mgogoro wa Rwanda,Malawi ziwa nyasa ni sawa,angenyamaza kimyaa ungekuwa wa kwanza kupiga kelele,mimi sifurahii kuona rais wa nchi anatukanwa na Nchi fulani,hata kama rais huyo anatoka chama tofauti na nachokipenda,Rais ni wa wote kama taifa bila kujali chama.
Kifupi ulichoandika kuhusu mheshimiwa Benard Membe ni upuuzi uliopitiliza.Membe ndani ya chama chake ni mmoja ya watu wenye rekodi safi kabisa.
Angekuwa hana uwezo asingeweza kudumu usalama kwa miaka mingi hivyo.Asingepewa wizara nyeti kama hiyo.Tupende tusipende Membe ni kachero na Mwanadiplomasia Mbobezi hapa TZ.
Siku nyingine jaribu kushirikisha ubongo wako unaporusha uzi hapa.
Leo asubuhi tumeshuhudia makala ya kipropaganda dhidi ya Waziri Membe ikisambazwa na kijana Yericko Nyerere akimsema Waziri Membe kuwa hana historia kubwa katika mafanikio ya kielimu na uongozi na amechangia kudidimiza diplomasia yetu. Pia amehoji weredi wa Waziri Membe katika idara ya usalama wa taifa.
Tunachoweza kumjibu kijana Yericko Nyerere ambaye baadhi yetu tumekuwa tukisoma baadhi ya makala zake katika gazeti la Mawio ni kwamba Waziri Membe kielimu hana historia legevu au dhoofu kutokana na ukweli kwamba elimu yake haiwezi kuhojiwa mahali kutokana na uhalali wake.
Yericko Nyerere arejee makala ya Prof.Kitila Mkumbo kuhusu Waziri Membe ambaye ni mwanachama mwenzao wa upinzani na Mhadhiri wa chuo kikuu.
Itakuwa ajabu kwa watu aina ya Yericko kuacha kuhoji ubatili wa elimu ya Waziri Membe miaka ya nyuma waje wahoji leo mwaka wa uchaguzi.Hakika hizi ni hekaya za abunuwasi.Hakika Yericko katumwa kumchafua Waziri Membe.
Kuhusu weredi wa Waziri Membe idara ya usalama wa taifa eti hakuna mission aliyowahi kuisimamia na kuifanikisha hatutopenda kuzungumzia haya kwasababu hatuna mamlaka ya kufanya hivyo.
Kwa kuhitimisha tu niwaase vijana aina ya Yericko kuwa wanafanya utafiti kabla ya kuandika.Waziri Membe hajawahi kuwa naibu waziri wa mambo ya nje.Nina imani tumeeleweka!
Huku ndio kujibu hoja kweli?
Kijana, mambo usiyoyajua usitake kuyarukia pasi uelewa. Mimi sio mtetezi wa Membe lakini sipendi watu waongo na wazandiki kama wewe. Mwaka 1982/83 Membe alikuwa Katibu Mkuu wa serikali ya wanafunzi UDSM ikishirikisha Mlimani, Muhimbili na Sokoine. Labda miaka hiyo ulikuwa chekechea?
Hebu jaribu kujirekebisha bado ukingali na muda. Maisha ni safari ndefu.
clossed minded! unaleta upuuzi tu1! oH mara dawati la tatu kulia,so what? mkuu angalia sio unaleta nyuzi za kibwege ----- tu! link hiyo google uone!
MATUKIO-MICHUZI: Hon. Membe addresses UN General Assembly
Mmetumwa mchafue watu!!
Leo asubuhi tumeshuhudia makala ya kipropaganda dhidi ya Waziri Membe ikisambazwa na kijana Yericko Nyerere akimsema Waziri Membe kuwa hana historia kubwa katika mafanikio ya kielimu na uongozi na amechangia kudidimiza diplomasia yetu. Pia amehoji weredi wa Waziri Membe katika idara ya usalama wa taifa.
Tunachoweza kumjibu kijana Yericko Nyerere ambaye baadhi yetu tumekuwa tukisoma baadhi ya makala zake katika gazeti la Mawio ni kwamba Waziri Membe kielimu hana historia legevu au dhoofu kutokana na ukweli kwamba elimu yake haiwezi kuhojiwa mahali kutokana na uhalali wake.
Yericko Nyerere arejee makala ya Prof.Kitila Mkumbo kuhusu Waziri Membe ambaye ni mwanachama mwenzao wa upinzani na Mhadhiri wa chuo kikuu.
Itakuwa ajabu kwa watu aina ya Yericko kuacha kuhoji ubatili wa elimu ya Waziri Membe miaka ya nyuma waje wahoji leo mwaka wa uchaguzi.Hakika hizi ni hekaya za abunuwasi.Hakika Yericko katumwa kumchafua Waziri Membe.
Kuhusu weredi wa Waziri Membe idara ya usalama wa taifa eti hakuna mission aliyowahi kuisimamia na kuifanikisha hatutopenda kuzungumzia haya kwasababu hatuna mamlaka ya kufanya hivyo.
Kwa kuhitimisha tu niwaase vijana aina ya Yericko kuwa wanafanya utafiti kabla ya kuandika.Waziri Membe hajawahi kuwa naibu waziri wa mambo ya nje.Nina imani tumeeleweka!
This shows you can not counter what I have said. If you can, try to debunk it. Otherwise, your silly statement belongs to my dustbin.that's too cheap!!!!..
Yeriko Nyerere nani anayekutuma kuandika hayo?
Bernard Membe Mtanzania aliyefeli katika utumishi wa Umma !
View attachment 224363
Bernard Kamilius Membe ni waziri wa Mashauri ya Kigeni nchini Tanzania, ni mwanachama wa chama cha mapinduzi,
Historia ya Membe inaanzia mbali kidogo toka kusini mwa Tanzania katika mikono salama ya upadre, chini ya ukasisi wa Namupa Seminari.
Bernard Kamilius Membe kijana wa kati mwenye uso angavu akiketi dawati la Tatu kutoka kulia, alikuwa mtoto mwenye akili ya kawaida akiwa nyuma ya watoto wenye vipaji shuleni hapo, Kasisi Mariano anamueleza kama Bernard mvivu wakusimamiwa kila jambo,
Hayo ni ya Namupa Seminari na Itaga Seminari katika mapito yake kielimu. Bernard Membe kutoka Darasa la awali hadi High School yani kidato cha sita, hakuna mahali panapotaja uimara wake kiakili darasani wala hakuna tukio lolote la kishujaa la kukumbukwa, iwe katika mitiahani, michezo, uongozi shuleni ama sifa yoyote toka kwa wakufunzi wake.
Kwaujumla alikuwa ni mwanafunzi wa kawaida kabisa ambae hawezi kusonga mbele bila usimamizi wa walimu wake kinyume na wanafunzi wengine,
Mwaka 1978 Membe aliingia kwenye ajira ya serikali akihudumu Ofisi ya Rais Idara ya Usalama wa Taifa kitengo cha uchambuzi wa taarifa za kijasusi, Kazi hiyo amehudumu kwa mika kumi na mbili tu akahamishiwa Wizara ya Mashauri ya Kigeni na kwenda Ottawa Canada kuwa mshauri wa Kibalozi kutoka 1992-2000,
Utumishi wake ndani ya Idara ya Usalama haukuwa wa kutukuka na hakuna kumbukumbu lake na la mfano ndani ya idara kwa ujumla zaidi ya kuwa mmoja ya majasusi wa Tanzania waliopata mafunzo ya mda kuke Scotland Uk, Hakuna mission yoyote aliyowahi kupewa na akaifanya kwa ufanisi wenye kukubalika ndani ya Idara, anamshinda hata Eliamkim Maswi yule wa Escrow ambae yeye alipewa mission ya kuiua NCCR ya Mrema na akafanikiwa kwakujipenyeza mpaka kuwa mbeba mikoba wa Mrema enzi zile na kuizika NCCR MAGEUZI kabisa,
Mwaka 2000 aliingia kwenye siasa akawa Mbunge wa Jimbo la Mtama, nakisha tarehe 17/10/2006 hadi 1/11/2007 aliteuliwa kuwa naibu Waziri wa Nishati na Madini, na kisha 1/12/2007 mpaka sasa ni Waziri kamili wa Mashauri ya Kigeni,
Kulegalega kwa Diplomasia ya Tanzania kunatokana na udhaifu wa Bernard Membe katika wizara hii ya mashaiuri ya Kigeni, Diplomasia ya nchi imeshuka na sasa sio Tanzania ile yenye sauti ya UTU.
Katika kipiti cha utmishi wa Bernard Membe ndani ya Wizara taifa limeshuhudia migogoro mikubwa ya Kidiplomasia na mataifa ya kigeni, ambayo kimsingi ni ufinyu wa maarifa wa Bernard Membe katika kukabiliana nayo,
Mathalani Mgogoro na Malawi wa Ziwa Nyasa, Mgogoro na Rwanda, Mgogoro na Kenya, Mgorogoro na Uingeraza, Mgogoro na ummoja wa nchi wa Hisani wa Maendeleo za Ulaya,
Haya yote yametukia katika uongozi wa Bernard Membe katika wizara inayohusika na mashauri ya Kigeni, lakini hili linatokana na historia ya mtumishi huyu ambaye hajawahi kuwa kiongozi wala hajawahi kujiongoza yeye mwenyewe,
Je dhamana kubwa kabisa ya Urais wa Jamhuri anaweza ikiwa Wizara tu imemshinda?
Zingatia, Bernard Membe hajawahi kuwa kiongozi wa umma tangu AZALIWE 1953 mpaka 2000 alipoingia kwenye siasa, hivyo uongozi sio kipaji chake!
Tatizo tulionalo kwa kweli wenye uzoefu wanahusika na UFISADI ktk kila kona, wengine kama Zitto, Makamba, Mwigulu na Kingwalangala bado muda labda 2020, sasa Membe pamoja kwamba akiongea wengine tunasikia kusinzia, wengine ni kina nani? Mwandosya hovyo Wizara ya Maji ilikuwa ujiko aonyeshe makeke, Wassira hata kumfikiria hapana, Lowassa atauza nchi, Migiro haijui nchi, Kinana ......, Mama Makinda I don't know, Jaji Augustino labda, kichwa kinauma nawaachie nyie..