Why Foreign Aid is hurting Tanzania and other African countries!

Wakati ndugu zetu wanauliwa na kemikali zitokanazo na ujasiriamali wao hatusikii kelele. Tunapoporwa hazina yetu kupitia makampuni hewa kama Meremeta sauti zao hazisikiki. Ndugu yao mmoja apatapo madhara kidogo kulinganisha na madhara wanayotusababishia, tunatishiwa kufutiwa misaada. Pengine kwa kuondoa misaada yao hiyo tutakachopungukiwa ni vumbi tunalotimuliwa na magari tusiyoyahitaji yanayonunuliwa kwa misaada yao hiyo. Na waende na misaada yao!
 

Ninyi niliowekea wino wa bluu na mfanye kazi zenu tulizowaajiri. Isiwe ni harakati za kapeni 2010 kutudanganya mmefanya kazi.

Ila 'miafrika ndivyo tulivyo' tunaomba omba hata visivyoombwa. Kiranja mkuu, mzee wa kaya nadhani magoti yake yana sugu kwa kuombea misaada aaaaaaaaaaaggggggggggggggggggghhhhhhhhhhhhhhhhhhh!!!!!!!!!!!!!
 
Tumechoka sana na hawa mabwana na hivyo ni bora kubaki tukiwa na akili zetu lakini wewe habari hizi umezitoa wapi??
 
Tumechoka sana na hawa mabwana na hivyo ni bora kubaki tukiwa na akili zetu lakini wewe habari hizi umezitoa wapi??
Kweli mkuu, tuanze kufikiri kufanya mambo yetu bila misaada ya hawa wajomba. Wanaweza kututia mfukoni hii tabia ya kuzunguka nje kila kukicha kuombaomba
 
Kweli mkuu, tuanze kufikiri kufanya mambo yetu bila misaada ya hawa wajomba. Wanaweza kututia mfukoni hii tabia ya kuzunguka nje kila kukicha kuombaomba

Bajeti trilioni 9 - kati ya hizo trilioni 4 zatoka kwa wajomba. Tukaze buti tunaweza kujitegemea (Kenya mbona wao wanajitegemea 96%? )
 
Netherlands ni wakoloni kabisa kwa fikra. Ikiwa hawawezi kuchuma kiujanjaujanja watakubatiza kwamba 'you are an unreliable'. Mimi natamani kujua details za hiyo kampuni lakini kwa ninavyowajua inawezekana kabisa Tanzania imeshtukia deal lao feki. Rwanda hivi karibuni imeanza kuachana na hiyo misaada taratibu. Kusema ukweli bora tutafutane waafrica tujadiliane jinsi ya kuleta maendeleo, hayawezi kuletwa na waholanzi. Wanaowaita wawekezaji ni makampuni yao yanayosaidiwa na serikali zao, kuja kufanya ukoloni si wa nchi nzima bali wa visehemu sehemu.
 
I always ask myself... hivi misaada haitakiwi kuwa bila conditions? Nini maana ya msaada? kutoa back favour?
 
I always ask myself... hivi misaada haitakiwi kuwa bila conditions? Nini maana ya msaada? kutoa back favour?
Mkuu hamna msaada usio na conditions. Mtu yoyote anayetoa pesa anataka kuona pesa zinatumika kama ilivyo kusudiwa na si kunufaisha wengine. Misaada doesn't mean unatumia pesa utakavyo. Ni kama scholarship. Ni msaada lakini kuna vigezo unabidi umaintain ili kuendelea kupokea msaada huo.
Kwa maana hiyo hizo pesa za msaada hatuna hata uhuru nazo.
 
Misaada au ukoloni? Kwanza misaada yenyewe wanakula mafisadi tu. Let it go people!!
 
Tumebweteka kujishughulisha na tunaachia raslimali zetu zinaliwa na mgema (cha mlevi huliwa na mgema) kwa kuwa tunategemea misaada. Hatuwezi kujifunza kwa North Korea wanaojifanyia mambo yao bila kutegemea kuwapigia magoti mabwana. Hiyo misaada itatumaliza.
 


Mkuu ukiwa na sentensi general kama za Mugabe utakuwa unakosea. Sasa hivi Tanzania haiwezi kuwa koloni na sina hakika kama Uholanzi ina ambitions za Ukoloni. Tunachotakiwa kufanya ni kutumia akili na busara zetu, na si kuwaita wawekezaji hata wakiwa ni wawekezaji uchwara, wakoloni. Tuangalie ni namna gani tunanufaika, ni namna gani tunavuna kutokana na ushirikiano wetu. Westerners huwa wanasema THERE IS NO FREE LUNCH, sasa usitegemee kuwa m-dutch atatoa pesa zake halafu yeye asinufaike.
Inawezekana kuna mtu aliomba mlungula akanyimwa, inawezekana jamaa alitaka kurahisisha mambo halafu akagonga mwamba. Yote yanawezekana. Lakini sidhani kama ni sahihi kuwa na Mugabe mentality, kuwa wawekezaji ni wakaloni. Kama ndio hivyo tufukuze wote tubaki wenyewe.
 

Mkuu I think he is talking about neo-colonialism na siyo classic colonialism.
 
Mkuu I think he is talking about neo-colonialism na siyo classic colonialism.

Mkuu mbona huu upo tayari. Sasa hivi hatuwezi kusema kuwa hatupo under neo colonialism. Si waholanzi tu, nadhani Kenya ndio ina practice vizuri sana neo colonialism hapa Tanzania kuliko hata Uholanzi, lakini hailalamikiwi unaweza kuona element fulani ya ubaguzi.
 

Nimekupata mkuu. Mimi nadhani huu utegemezi wetu ndiyo una sababisha huo uneo-colonialism.
 

Ni sahihi kabisa, Nchi inapotegemea misaada haiwezi kupata maendeleo hata kidogo. Ili uweze ku-move/develop unahitaji kuwa na strategic plans ambazo unaweza kuzitekeleza. sasa kama unaishia kuomba omba tu, hizo plan utazitoa wapi???
 
Baada ya kulisoma Azimio la Arusha na kulielewa nimekuwa siku zote naamini kuwa ipo siku itatubidi kui-practice mifumo ambayo azimio hili liliiweka bayana kama kweli Tanzania kama nchi inataka kusonga mbele.

Nasema hivi kwasababu viongozi wa Tanzania sasa akili zao zimekuwa zinawaza misaada tu kwenye kufanya kazi za kimaendeleo. Wakati nchi hii ina rasilimali kubwa na nyingi katika kujiendeleza yenyewe tunachohitaji ni viongozi wenye akili za kuweka mipango mikakati jinsi gani ya kutumia ardhi, madini, mbuga za wanyama, milima, utamaduni wa asili kama Maasai, historical sites etc etc kwenye kujiletea maendeleo ya kutosha.

Sasa athari za kutegemea misaada ndio hizi kuwa nchi wahisani zinataka hadi raia wao wanaokuja kufanya uwekezaji uku wapate favour mpaka katika kuvunja kanuni na sheria zetu katika uwekezaji. Hivi si jambo la kushangaza mwekezaji kutoka nje badala ya kwenda kwenye vyombo husika kutatua matatizo yake, yeye anaenda kwa Prime Minister, hiki kiburi anapata wapi. Ndiyo yaleyale aliyosema hayati Mwalimu Nyerere kuwa watu wachache wataiweka serikali kwenye mifuko yao kama serikali haitokuwa makini.

Serikali ya awamu ya nne imeweka kipaumbele chake kwenye misaada kuliko jambo lolote lile kwa kuhakikisha hilo soma bajeti zote ambazo zimeshasoma zote ni tegemezi. Mfano mzuri ni barabara ya Manyoni-Dodoma ambayo serikali inategemea pesa kiasi cha bilioni 40 kutoka kwa wahisani ili kuijenga, sasa suppose ndo hivi wameanza kuchikichia ndio hatupati barabara watu wa kanda ya kati au la.

Misaada siyo suluhisho la matatizo yetu, tutakufa masikini tu tukiendelea na tabia hii ya kizembezembe.
 
Mkulo dismisses Dutch aid threat

By Mkinga Mkinga

Finance and Economic Affairs minister Mustafa Mkulo has played down the Dutch Government's intention to suspend aid to Tanzania. A Dutch minister was infuriated by "mistreatment" of his countryman who is involved in a timber business and asked his Parliament to suspend aid.

Mr Mkulo toldo The Citizen yesterday it was unfortunate that the country was basing its case on events involving only one businessman.

He said the Government had formally been informed of the Netherlands' decision and that several consultation meetings were held on the issue with no amicable agreement.

Dutch Development minister Bert Koenders wrote to the Lower House in his country, explaining that Tanzania was an unreliable partner for foreign investors. The minister took the decision after an unnamed Dutch businessman lost his investment in Tanzania.

However, the letter neither names the businessman nor gives details of the case, but the minister said "enough is enough". The bilateral budget for Tanzania for 2009 is 81 million euros (Sh148.2 billion).

This consists of 30 million euros for general budget support, 21 million euros for health care (including the programme for combating HIV/Aids), 18 million euros for good governance (decentralisation), 10 million euros for drinking water and sanitation and 1.1 million euros for improving the business climate.

The Netherlands' aid in 2008 totalled 69.7 million euros (Sh127.5 billion according to current exchange rates). The aid was directed towards health care, local government and private sector development.

Mr Mkulo told The Citizen yesterday that there was a Dutch businessman who wanted to be given special treatment.

"The Dutch was engaged in logging business, he was conducting his business from Mkumbara. He was a private businessman but there was a lot of interventions by his embassy," Mr Mkulo said.

He said the businessman had sought to meet Prime Minister Mizengo Pinda in his quest to be given special treatment in his business. But he was asked to contact Natural Resources and Tourism minister Shamsa Mwangunga instead.

When the businessman met the minister, he was directed to conduct his business in accordance with the laws and regulations, but he refused and forwarded the matter to his embassy.

"But it is diplomatically understood across the world that there is no country which is allowed to intervene in internal affairs of another country.

If, for instance UK sets its own regulation to remove hawkers in London, Tanzania cannot intervene simply because Tanzania hawkers are going to be affected... it is against the Geneva Convention,"explained Mr Mkulo without naming the businessman.

He said he had met the Dutch envoy and discussed the matter without knowledge that the businessman had gone to the Prime Minister on the same matter. Mr Mkulo referred this paper to Ms Mwangunga for further clarification but her phone was switched off.

The permanent secretary in the Ministry of Tourism and Natural Resources, Dr Ladislaus Komba, said he was unaware of the issue. But Tanzania is not the only country which has suffered Dutch aid freeze.

Mr Koenders named other countries which will miss aid from the Netherlands as Bosnia-Herzegovina, Albania, Armenia and Macedonia because they were receiving more funds from other sources.

Also affected are Eritrea and Sri Lanka for political turmoil, while Cape Verde will also miss Dutch aid on the grounds that its economy was performing well, the minister said in his letter.

The Netherlands each year spends 0.8 per cent of its gross domestic product on fight ingpoverty with half of the aid going to Africa.

In 36 countries it supports, the money is spent on improving governance, human rights and business opportunities.

Source: TheCitizen Newspaper
 
If the "AID" as provided by the Netherlands, has got such stupid strings we should not be held accountable by the stupid log thief from The Netherlands.
Has any one has got the mans business and address in Tanzania so that he can be pettitioned to leave for his good country?
 
Sijui watanzania wanajua kiasi gani serikali hii inavyoendeshwa kibinafsi. Tunafuja fedha za walipakodi wa ulaya kupitia viongozi wetu. Ni kweli hatuna ubavu wa kuishi bila misaada, ushahidi ni misaada inavyochangamkiwa kila mahali. Mwaka jana tuliambiwa bajeti yetu itasaidiwa kwa asili mia 34; mwaka huu mmesikia asili mia ngapi? Hiyo ndiyo bongo(lala)
 
Last edited:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…