Why should Magufuli reject Sylvia Mulinge as Vodacom CEO

Hoja ulifanyika usaili au tunafungashiwa tu? Mbona nasisi wapo akina kadogosa wa trl bwanamkulu wa msd kimei wa crdb nehemia mchechu wa nhc
 
Tumeona ma ceo wa hovyo kama kiyoko wa pmw na blady wa acacia hatuwezi kuendelea kufanyiwa majaribio
 
Iko listed DSE tunahaki ya kuhoji

eddy unapoint. Point yako ipo dhahiri na hakuna mtu mwenye ufahamu anaweza kuipinga. Kimei hakusoma mzumbe wala shule za kata. Hakusoma kwenye nchi zinazoamua kupika taarifa za elimu kwa msingi ya kisiasa. Alisoma nchi zinazojitambua na zenye lengo la kujenga taifa imara endelevu kwa kuwekeza kwenye elimu. "human development".


"Dr. Charles S. Kimei is a Managing Director at CRDB Bank Plc and Chairman at Tanzania Bankers Association. Dr. Kimei was previously employed as Director-Economic Research & Policy by Bank of Tanzania.

He received his undergraduate degree from Moscow State University Lomonosov, a graduate degree from Stockholm School of Economics and a doctorate degree from the University of Uppsala."

Ninaomba unzishe uzi, au uombe mods wafungue forum maalumu ya ku address suala la elimu hapa nchini, lisiwe jukwaa la hovyohovyo. Jukwaa litakatoa ushauri namna gani elimu yetu inapashwa kutengenezwa kwanza, namna ya kutengeneza na kupata kina Kimei wengi, namna ya kutengeneza uwezo wa kupambana katika soko la ajira ndani na nje na katika nyanja za kimataifa katik adunia hii ya utandawazi, na namna gani elimu ya juu inapahswa kuwa sambamba na mfumo wa ajira kimataifa katika sekta za umma na hata za binafsi.

NINAOMBA SANA HILI SUALA TULIPE UZITO NA TULIJADILI KWA MTAZAMO WA KIPEKEE KWA MASLAHI YA TAITA LA LEO NA VIZAZI VYETU VIJAVYO.
 
Hoja ulifanyika usaili au tunafungashiwa tu? Mbona nasisi wapo akina kadogosa wa trl bwanamkulu wa msd kimei wa crdb nehemia mchechu wa nhc

hivi yule ceo aliyopita wa voda ian.. na yule aliyepita mzungu.. je tuliletewa tu au ulifanyika usahili...

voda ni kampuni binafsi... maamuzi ni yao wamuajiri nani na kwa mfumo gani??

pia internal post huwa inaangalia wafanyakazi wa ndani tu... ambapo management ya voda iliona huyo mama anafaa kwa hiyo nafasi...

sasa ulitaka wamchukue mchechu ambaye anashinda mahakamani mwizi kaibia nchi yake maskini... mtu anaibia hadi nchi yake maskini hana huruma ndio umpe voda ambayo ni kampuni tajiri si ataiba hadi viti
 
sound good...
 
Vodacom sio kampuni binafsi tangu wauze hisa dse imekuwa plc serikali ina haki ya kuhoji
 
wacha blah blah za jk. Tunazo taratibu za kupata vibali vya kazi kwa wageni lazima zifuatwe.
 
wacha blah blah za jk. Tunazo taratibu za kupata vibali vya kazi kwa wageni lazima zifuatwe.

kama ma ceo wote wa voda walioondoka walipata vibali na sio watanzania... hata huyu mama atapata tu..

kibali cha ajira sio kazi yake kutafuta.. ni voda wanamtafutia bosi wao. na wanapata..

hizi ajira binafsi sio za uma.. wageni wamejaa kila sehemu makampuni binafsi.. na sababu elimu yote ni mbovu na wizi wetu wanatuogopa...
 
Vodacom sio kampuni binafsi tangu wauze hisa dse imekuwa plc serikali ina haki ya kuhoji

multinationals hazitaki degree za vyuo vya kata na english ya ze ze ze nyingi board room

serikali ina hisa kibao NMB ila ceo ni mzungu mama ineke.. nenda kalalamike awekwe mtanzania..

serikali ina hisa kibao puma energy nenda kalalamike mzungu atolewe awekwe mtanzania..

serikali ina hisa kibao TCc nenda kalalamike mgeni atolewe awekwe mtanzania..

serikali ina hisa kibao NBC nenda kalalamike yule mzambia mizinga melu atolewe awekwe mtanzania
 
acacia pamoja na makinikia walikuwa na maceo wazungu tulipigwa pesa ndefu. leo linaendeshwa na mswahili linapata faida na haliuzi makinikia
 
Hayo ndo mambo yakuhoji iweje watanzania wanyimwe fursa za juu tuambulie ulinzi hapa tatizo lipo. Ni wageni sio kwa sababu wana ujuzi kuliko wabongo ni kwa sababu ya mapungufu katika wizara husika mavunde anajua kuangalia michango ya nssf na wcf basi upumbavu mwingine unapita. Nenda UAE australia uone kama mgeni unaweza kuwa ceo
 
Post nzuri sana tena ya kizalendo. Ni matumaini yangu rais wetu atasikiliza na kufanyia kazi ushauri huu. Tanzania ni yetu. Ikiharibika wenye hasara ni sisi. Wengine hata nje ya Tanzania hatupajui. Kulinda rasilimali zetu ndio uzalendo namba moja
Uzalendo usio na tija, mzalendo anayeipenda nchi yake ni yule anayekwenda Kenya anachapa kazi analeta pesa nyumbani, tuige wakenya na wachina siyo uzalendo wa politiki.
 
huoji iweje wakati hujijengi uwezo unalalamika tu..

dunia kijiji nowdays.. ndio maana samatta alipata nafasi tp mazembe huku wacongo kibao wanaililia..

elimu yetu ina mapungufu mengi sana kwamba aliesoma tz tu maisha yake yote kupata nafasi kubwa multinationals ni ishu ngumu.

mtu ana phd au proff kabisa ila kiingereza cha ze ze ze unafikiri nani anataka huo ujinga..

 
Uzalendo usio na tija, mzalendo anayeipenda nchi yake ni yule anayekwenda Kenya anachapa kazi analeta pesa nyumbani, tuige wakenya na wachina siyo uzalendo wa politiki.
kuwa serious ulichoandika hakimake sensi........

kuwa we mfano basi kama kwenda kupiga kazi nnje ni uzalendo basi raia wote duniani walio nnje na nnchi yao ni wazalendo...

umejikanyaga mkuu...pointless....
naona unatupa meaning mpya sasa ya uzalendo from your brain
 
Sorry, unachangia uzi huu au kuna uzi mwingine ulikuwa unataka kuchangia?
 
Angekuwa mtanzania sawa ila kwa raia wakigeni kujifunzia tanzania hapana. Tusifanye nchi yetu sehemu yakujifunzia. Tumahitaji kulinda maslahi yawatanzania tumenunua hisa tumewekeza fedha zetu. Huyu mama hata hisa moja vodacom hana
Wameshatuona guinea pigs, bastards, yaani aje ajifunzie kwetu? Kwanini asijifunzie huko kwao?
 

Kwa hiyo kipimo chako cha kufanya KAZI ni lugha ya malkia.
My goodness.
 
ni caution nzuri ila...

swala sio tu waKQ kuja Tanzania na kuchukua kazi kwenye shirika kubwa na saa zingine kuua makampuni, nchi nyingi zimefaidika na hiki kisiwa chetu cha Amani ni kwa vile tu KQ ni next door.

issue za kuweka sawa ni kuhakikisha taifa lina jenga vijana shupavu, vijana wasio waoga. watu wanasema elimu lakini elimu sio shida kihivyo issue ni communication kama wengi wanavyo hint. English as a communication medium ndio shida kubwa kitaifa. kingereza ni shida kwetu.

nadhani mijadala (debates) kuanzia primary level na kuendelea mashuleni itakuwa step moja wapo katika kukomaza kingereza na communication skills pia. hasa kama kingereza chenyewe kitatumika kama lugha.

practice alone does not make perfect but repetition does
 
BTW I am pretty happy on the response this thread has had. My expectation is the relevant authorities will intervene and prevent our companies from being sabotaged by our competitor.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…