LGE2024 Wiki moja baada ya agizo la RC Kilimanjaro: Wizi wa Vitabu vya Majina ya Wakazi, Polisi mmefikia wapi?

LGE2024 Wiki moja baada ya agizo la RC Kilimanjaro: Wizi wa Vitabu vya Majina ya Wakazi, Polisi mmefikia wapi?

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Ni zaidi ya Wiki moja sasa tangu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu, alipotoa agizo kwa Jeshi la Polisi kuwasaka na kuwachukulia hatua wale waliohusika katika wizi wa vitabu vya majina ya wakazi katika kituo cha Josho, kijiji cha Kikelelwa, wilayani Rombo. Tangu wakati huo, hakuna taarifa za hatua zilizofikiwa, hasa ikizingatiwa kuwa agizo hilo lilijiri kufuatia wizi wa vitabu viwili vilivyokuwa na majina ya wananchi 1,105.
1730204125687.png
Nakumbuka polisi waliripoti kuwashikilia watu wanne kwa mahojiano kufuatia na tukio hilo. Hata hivyo, taarifa rasmi kuhusu uchunguzi huo bado hazijatolewa kwa umma.

Soma: Kilimanjaro: Wasiojulikana waiba madaftari ya kujiandikishia, wengine wachoma moto Ofisi ya Mtendaji
 
Back
Top Bottom