Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 57,951
- 32,619
BINTI YANGU NJOO NIKUAMBIE HAPA.
Mithali 20:7
[7]Mwenye haki aendaye katika unyofu wake, watoto wake wabarikiwa baada yake.
Haki katika ndoa yako ambayo Mungu amekupa hakikisha unaishi katika haki, wamama wengi siku hizi hasa hawa mabinti wanajivunia watoto wao wakiwa wazuri wa sura, wakiwa na akili darasani, na akivaa nguo inamkaa utasikia wanangu wana damu za nguo jamani.
Yaani ndio imekuwa mada yaani umeona watoto wa wengine ni kama vigengedere tu.
Sasa ni hivi mmeacha kuomboleza, mmeacha kumtumikia Mungu, mmeacha kuheshimu ndoa zenu, yaani mmeacha kuwa wenye haki.
Andiko tajwa hapo juu linazungumzia mzazi atakae kwenda ktk unyofu wa haki hakika watoto wake watabarikiwa badala yake, yaani watoto watarithi nini kutoka kwako?
Natamani Ukue uone jinsi gani Dunia imeharibika nje kumeoza ni kwamba Kama jamii haiko salama basi watoto wako hawako salama.
Acha kujipiga msamba tamani kuwa mama muombolezaji na uwafanye watoto wako wana wa Mungu.
Ni maombi yangu watoto wetu wawe wana wa Mungu.
YESU LUGHA YANGU.
Mithali 20:7
[7]Mwenye haki aendaye katika unyofu wake, watoto wake wabarikiwa baada yake.
Haki katika ndoa yako ambayo Mungu amekupa hakikisha unaishi katika haki, wamama wengi siku hizi hasa hawa mabinti wanajivunia watoto wao wakiwa wazuri wa sura, wakiwa na akili darasani, na akivaa nguo inamkaa utasikia wanangu wana damu za nguo jamani.
Yaani ndio imekuwa mada yaani umeona watoto wa wengine ni kama vigengedere tu.
Sasa ni hivi mmeacha kuomboleza, mmeacha kumtumikia Mungu, mmeacha kuheshimu ndoa zenu, yaani mmeacha kuwa wenye haki.
Andiko tajwa hapo juu linazungumzia mzazi atakae kwenda ktk unyofu wa haki hakika watoto wake watabarikiwa badala yake, yaani watoto watarithi nini kutoka kwako?
Natamani Ukue uone jinsi gani Dunia imeharibika nje kumeoza ni kwamba Kama jamii haiko salama basi watoto wako hawako salama.
Acha kujipiga msamba tamani kuwa mama muombolezaji na uwafanye watoto wako wana wa Mungu.
Ni maombi yangu watoto wetu wawe wana wa Mungu.
YESU LUGHA YANGU.