William Erio: Mwisho wa Enzi kwa Boss wa NSSF au Mwanzo Mpya?

William Erio: Mwisho wa Enzi kwa Boss wa NSSF au Mwanzo Mpya?

Freshbrain

Member
Joined
Oct 3, 2011
Posts
29
Reaction score
82
Mr. William Erio ambaye leo ameondolewa katika Cheo cha Mkurugenzi Mkuu NSSF si jina geni. Amekuwa katika cheo kikubwa cha Mkurugenzi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa muda mrefu toka mwaka 2002 alipokuwa Mkurugenzi Mkuu wa PPF hadi mwaka 2018 alipohamishiwa NSSF baada ya kung'olewa Prof. Kahyarara ambaye leo ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Uwekezaji.

Kwa maoni yangu, Erio ni kati ya viongozi walio 'overstay' katika nafasi moja kwa muda mrefu sana, kiasi kwamba inawezekana ubunifu ulikuwa unaelekea au umefika kikomo. Alikaa kama Mkurugenzi Mkuu wa PPF kwa miaka takriban 16 toka enzi za Mkapa hadi enzi za Magufuli. Ukijumlisha na miaka aliyokaa NSSF toka ameteuliwa 2018 inaelekea miaka 20 katika uongozi wa mifuko ya hifadhi ya jamii. Inawezekana aliweza kukaa bila kutikiswa muda mrefu na hata kuendelea kuaminiwa sababu ya mjomba wake Hayati Mkapa (mtakumbuka katika msiba wa ndio alikuwa msemaji wa familia)!.

Pamoja na kwamba kuna wengine mtakuja na hoja kwamba 'experience matters' ila kwa kiongozi wa juu kuoverstay kwa kiasi hicho, kunaleta uwezekano mkubwa wa kutokuwa mbunifu na kuweka 'syndrome' ya kubebana na watu mliokuwa pamoja toka enzi hizo a.k.a ' The Oldboys Club' ili kulinda maslahi yenu yaliyopo kwa muda mrefu.

Hili Erio alilionyesha sana kipindi ameteuliwa kwenda NSSF ambapo licha ya kuhamisha hamisha wafanyakazi lundo waliokuwa wazoefu hapo NSSF na kuwapeleka Serikali Kuu, Halimashauri n.k alihakikisha anabeba viongozi aliokuwa nao PPF na kuhamia nao wote NSSF. Achilia mbali viongozi, ni kama aliihamisha PPF yote kwenda NSSF pamoja na kwamba PPF iliungana na mifuko mingine kuunda PSSSF na hivyo ilibidi asilimia kubwa ya wafanyakazi wake kuwa huko (Ajabu Sana🤔!)

Hii ilipelekea NSSF kutokuwa tena wabunifu na kujikuta inafanya vitu 'kama vilivyokuwa vikifanyika PPF' pamoja na kwamba mazingira ya mifuko hii (operating environment) hayakuwa yanafanana kwa asilimia kubwa kutokana na ukubwa wa mifuko husika na aina ya wateja wake. Hii imeleta usumbufu mkubwa sana kwa wateja katika kipindi cha karibuni na kuchelewesha sana utoaji huduma katika ofisi za mikoa ambapo amepoka mamlaka ya mikoa na maamuzi mengi kufanywa makao makuu. Katika uwekezaji na maeneo mengine nako hali ni hio hio.

Naamini Mr. Masha Mshomba aliyeteuliwa anaenda kurithi hii 'The Oldboys Club' ambapo imeovestay kwa pamoja na Erio, sisemi kwamba awatoe, ila anapaswa kuwa nao makini i.e za kuambiwa changanya na za kwako!.

Namtakia kila lakheri Bw. Mshomba na pia kila la kheri Bw. Erio katika mapumziko yake/kazi mpya na kumpongeza kwa utumishi wa muda mrefu.

Swali kubwa linabaki, je huu ndio mwisho wake? au kuna jema zaidi linakuja?. Wahenga walisema, Muda ni mwalimu mzuri!
 
Erio kazi kubwa aliyokuwa anafanya hapo nssf ni kuhamisha staffs wa Nssf na kuwapeleka halmshauri na kuingiza staffs wa PPF kwa kuamin hawataweza kumhujumu.

Besides hata kuondoka kwa Kyaharara inasemekana ni Erio alienda kupika majungu kwa mwendazake ili aweze chukua yeye hiyo nafas kwa kutumia mgongo wa Benjamin Mkapa (Hayati(, leo pasaka anaitafunia kijiweni, Mungu anatisha
 
Unasema, “...Hili alilionyesha sana kipindi ameteuliwa kwenda NSSF ambapo licha ya kuhamisha hamisha wafanyakazi lundo waliokuwa wazoefu hapo NSSF na kuwapeleka Serikali Kuu, Halimashauri n.k alihakikisha anabeba viongozi aliokuwa nao PPF na kuhamia nao wote NSSF...” Really?

Mkurugenzi wa NSSF aliwezaje kuhamisha wafanyakazi kutoka NSSF kwenda Serikali Kuu na halmashauri? Wafanyakazi wa NSSF nao wako chini ya Civil Service?
 
Unasema, “...Hili alilionyesha sana kipindi ameteuliwa kwenda NSSF ambapo licha ya kuhamisha hamisha wafanyakazi lundo waliokuwa wazoefu hapo NSSF na kuwapeleka Serikali Kuu, Halimashauri n.k alihakikisha anabeba viongozi aliokuwa nao PPF na kuhamia nao wote NSSF...” Really?

Mkurugenzi wa NSSF aliwezaje kuhamisha wafanyakazi kutoka NSSF kwenda Serikali Kuu na halmashauri? Wafanyakazi wa NSSF nao wako chini ya Civil Service?
Sheria ya Mashirika imefutwa. Hivyo kwa sasa Watumishi wote wapo chini ya Utumishi. Kuhamishwa kutoka kwenye Shirika la umma kwenda Halmashauri au Serikali Kuu ni jambo la kawaida tangu awamu ya 5 iingie madarakani.

Ni matumaini yetu Mama ataangalia tena hilo eneo ili utaratibu wa zamani urejeshwe.
 
Sheria ya Mashirika imefutwa. Hivyo kwa sasa Watumishi wote wapo chini ya Utumishi. Kuhamishwa kutoka kwenye Shirika la umma kwenda Halmashauri au Serikali Kuu ni jambo la kawaida tangu awamu ya 5 iingie madarakani.

Ni matumaini yetu Mama ataangalia tena hilo eneo ili utaratibu wa zamani urejeshwe.

Shukrani kwa ufafanuzi!
 
Sema tumerudi kwenyr kutolewa station A kupelekwa B!! MTU anaonekana hatoshi anasogezewa pengine kisa woga wa kutumbua!!
 
Majungu tu.

Kwaiyo umechaguliwa wewe?
 
Acheni majungu yasiyo na kikomo, hujui kitu, eti mwendazake ujinga mtupu. Mliyoyategemea hayajaja jiandaeni na maumivu kama kawa.Tanzania haitakaa irudi nyuma. Chuma chuma tu
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] pole sana mkuu,, maombolezo yanaendelea.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom