William Mganga Ngeleja kuteuliwa Uwaziri Madini na Nishati

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
July 10, 2017
Wakuu,
Hatua ya Mbunge William M. Ngeleja kuamua kurudisha fedha zenye tuhuma nzito Ths.40,420,000 alizopewa na Ndg. James Rugemalira wa IPTL /ESCROW ni njia mojawapo kujisafisha ili kuweka wazi nafasi ya kuteuliwa tena katika baraza la mawaziri kama Waziri wa Nishati na Madini.

Mheshimiwa Wiliam Ngeleja mbunge wa CCM mwenye taaluma ya sheria na mwakilishi wa jimbo lake la ubunge kwa karibu miaka 12 yaani vipindi vitatu vya kuchaguliwa kama mbunge ana uzoefu wa kibunge, unaibu waziri na waziri kamili katika serikali ya awamu ya nne ya CCM.

Pia katika kupitia hotuba zake na michango Bungeni kwa ''level'' ya CCM kama clip hapa chini anaonesha kuwa na umahiri na unyenyekevu kuliko majigambo ya Prof. Muhongo aliyekuwa Waziri wa Madini na Nishati.

Wizara ya Madini na Nishati ili kuepukana na mikataba mibovu inahitaji waziri mwenye taaluma ya sheria na anayeweza kujenga hoja kwa ''weledi'' mkubwa, kitu ambacho wanasheria wengi huwa ndiyo msingi wa taaluma yao.

Awamu ya tano katika teuzi zake tunaweza kuotea kuwa uteuzi wa waziri wa Madini na Nishati anaweza kutoka CCM bila shaka yoyote na pia katika mikakati ya kuapata kura nyingi zaidi za uchaguzi tunaweza kuotea anaweza kutokea wapi n.k


Tusikilize/ tazame mbunge William Mganga Ngeleja akionesha ''uzoefu'' wake wa sekta ya Madini na Nishati na changamoto za kuweka mabo sawa katika sekata hiyo :

Published on 2 Jun 2017
William Ngeleja Afunguka Issue Ya Mchanga
Source: Global Tv Online

Moderator msaada hamishia jukwaa la siasa
 
Ameambiwa ajidai amerudisha pesa ili ateuliwe kuwa waziri wa hiyo wizara.. Ila kwa hii tabiri tabiri mtamfanya asiyepangiwa kupangua mipango!
 
Anapaswa kukamatwa na kusekwa lupango. Sheria zipo wazi. Uwaziri tena asahau. Labda uwaziri wa sketi ya mkewe!
 
anavyochukia wapinzani. Atanteua ngeleja ili tu awakonoe wapinzani.
Nina uhakika kina Lisu wakisema kuwa juma maharagwe hawezi kula mav** atakula ili kuwakomoa. Prove me wrong.

Comment ni yangu JF haihusiki na sio mzimamo wa Jf
 
anavyochukia wapinzani. Atanteua ngeleja ili tu awakonoe wapinzani.
Nina uhakika kina Lisu wakisema kuwa juma maharagwe hawezi kula mav** atakula ili kuwakomoa. Prove me wrong.

Comment ni yangu JF haihusiki na sio mzimamo wa Jf
Ulale!
 
Reactions: BAK
Halafu aendelee kudanganya umma wa Watanzania kwamba anapambana na ufisadi wakati bado anawakingia kifua kwa nguvu zote mafisadi akina Mkapa, Kikwete, Lugumi, Chenge, Tibaijuka etc

anavyochukia wapinzani. Atanteua ngeleja ili tu awakonoe wapinzani.
Nina uhakika kina Lisu wakisema kuwa juma maharagwe hawezi kula mav** atakula ili kuwakomoa. Prove me wrong.

Comment ni yangu JF haihusiki na sio mzimamo wa Jf
 
Halafu aendelee kudanganya umma wa Watanzania kwamba anapambana na ufisadi wakati bado anawakingia kifua kwa nguvu zote mafisadi akina Mkapa, Kikwete, Lugumi, Chenge, Tibaijuka etc
Ila bado siamini kama anaweza kumrudisha ngeleja? Itakuwa ni blanda moja kubwa sana
 
Ameambiwa ajidai amerudisha pesa ili ateuliwe kuwa waziri wa hiyo wizara.. Ila kwa hii tabiri tabiri mtamfanya asiyepangiwa kupangua mipango!

Hah ! Hah ! Tukistaajabu ya Musa Tutaona ya CCM iliyo na kiburi kwa kurudisha huyo huyo ''aliyejisafisha'', maana CCM masuala ya makinia walisema wao ndiyo walipiga kelele sana kuliko wapinzani.

Na kwa hili watasema jamaa anafaa sana kushiriki ktk mazungumzo yanayokuja na BARRICK manake hawawezi kumtegemea Waziri wa Sheria na Katiba Prof. Palamagamba Kabudi awe ''mchezaji-kiraka wa kila namba/wizara'' pamoja na mwanasheria mkuu wa serikali kuongoza ''mazungumzo ya muafaka na BARRICK'' bila uteuzi wa ''dharura'' wa waziri wa wizara ya Madini na Nishati ''mahiri'' kama William Ngeleja.
Leo wilayani Chato, wakati akipokea nyumba za watumishi wa afya, zilizotolewa na taasisi ya Benjamini Mkapa Foundation.

Mh Rais Dr John Pombe Joseph Magufuli, amesema serikali keshokutwa itaanza mazingumzo na kampuni ya Barrick Gold Mine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…