William Miller: Kama Yesu hakujua Hisabati au kutafsiri mambo bora angalikaa Kimya. Mbona siku ya mwisho wa dunia inakokotoleka kirahisi?

"Kama ilivyo punje moja ya mchanga mbele ya fukwe za bahari kuu za dunia, ndivyo ulivyo ufahamu wetu mbele ya tusiyoyajua duniani na ulimwenguni na mbele ya yale tunayodhani kuwa tunayajua".
 
Soma kitabu cha Ufunuo 13...

1 Kisha nikaona mnyama akitoka katika bahari, mwenye pembe kumi, na vichwa saba, na juu ya pembe zake ana vilemba kumi, na juu ya vichwa vyake majina ya makufuru.
2 Na yule mnyama niliyemwona alikuwa mfano wa chui, na miguu yake ilikuwa kama miguu ya dubu, na kinywa chake kama kinywa cha simba, yule joka akampa nguvu zake na kiti chake cha enzi na uwezo mwingi.
3 Nikaona kimoja cha vichwa vyake kana kwamba kimetiwa jeraha la mauti, na pigo lake la mauti likapona. Dunia yote ikamstaajabia mnyama yule.
4 Wakamsujudu yule joka kwa sababu alimpa huyo mnyama uwezo wake; nao wakamsujudu yule mnyama, wakisema, Ni nani afananaye na mnyama huyu? Tena ni nani awezaye kufanya vita naye?
5 Naye akapewa kinywa cha kunena maneno makuu, ya makufuru. Akapewa uwezo wa kufanya kazi yake miezi arobaini na miwili.
6 Akafunua kinywa chake amtukane Mungu, na kulitukana jina lake, na maskani yake, nao wakaao mbinguni.
7 Tena akapewa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda, akapewa uwezo juu ya kila kabila na jamaa na lugha na taifa.
8 Na watu wote wakaao juu ya nchi watamsujudu, kila ambaye jina lake halikuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia.
9 Mtu akiwa na sikio na asikie.
10 Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye subira na imani ya watakatifu.
11 Kisha nikaona mnyama mwingine, akipanda juu kutoka katika nchi; naye alikuwa na pembe mbili mfano wa Mwana-Kondoo, akanena kama joka.
12 Naye atumia uwezo wote wa mnyama yule wa kwanza mbele yake. Naye aifanya dunia na wote wakaao ndani yake wamsujudie mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona.
13 Naye afanya ishara kubwa, hata kufanya moto kushuka kutoka mbinguni uje juu ya nchi mbele ya wanadamu.
14 Naye awakosesha wale wakaao juu ya nchi, kwa ishara zile alizopewa kuzifanya mbele ya huyo mnyama, akiwaambia wakaao juu ya nchi kumfanyia sanamu yule mnyama, aliyekuwa na jeraha la upanga naye akaishi.
15 Akapewa kutia pumzi katika ile sanamu ya mnyama, hata ile sanamu ya mnyama inene, na kuwafanya hao wote wasioisujudu sanamu ya mnyama wauawe.
16 Naye awafanya wote, wadogo kwa wakubwa, na matajiri kwa maskini, na walio huru kwa watumwa, watiwe chapa katika mkono wao wa kuume, au katika vipaji vya nyuso zao;
17 tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza, isipokuwa ana chapa ile, yaani, jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake.
18 Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na aihesabu hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita, sitini na sita.
 
TAFASRI YA MNYAMA WA KWANZA WA UFUNUO 13

β€œKisha nikaona mnyama akitoka katika bahari, mwenye pembe kumi, na vichwa saba, na juu ya pembe zake ana vilemba kumi, na juu ya vichwa vyake majina ya makufuru. Na yule mnyama niliyemwona alikuwa mfano wa chui, na miguu yake ilikuwa kama miguu ya dubu, na kinywa chake kama kinywa cha simba, yule joka akampa nguvu zake na kiti chake cha enzi na uwezo mwingi.” Ufunuo 13:1-2. Mnyama huyu wa ajabu bila shaka anawakilisha utawala wa Rumi. Kumbuka utawala wa Rumi umepitia katika awamu tatu.


Awamu ya kwanza ni Rumi ya kipagani, iliyodumu kuanzia mwaka 168 KK hadi iliposambaratika mwaka 476 BK. Awamu ya pili ni Rumi ya kidini, chini ya papa iliyodumu kuanzia mwaka 538 BK hadi ilipotiwa jeraha la mauti mwaka 1798 BK. Awamu ya tatu na ya mwisho ni Rumi ya kidini ikiambatana na rumi ya kipagani.

Rejea mwanamke aliyekaa juu ya mnyama katika Ufunuo 17. Huo ulikuwa ni utambulisho juu ya huyu mnyama wa ajabu. Katika vichwa vya huyu mnyama kulikuwa na majina ya makufuru.

Tukirudi katika Danieli 7:8 tunaona pembe ndogo iliyochomoza kutoka kwa yule mnyama, yaani upapa, ilinena maneno ya makufuru. Hivyo ni lazima utakuwa ni utawala uleule. Paulo aliligusia hili wakati anazungumzia mtu wa kuasi, β€œMtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu; yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu.” 2 Thes 2:3-4.

Uasi ulikuwa umeanza kuingia taratibu katika kanisa hata Paulo akingali hai. Lakini Paulo anasema siku ya Bwana isingaliweza kuja kama hajafunuliwa mtu wa kuasi, ajiinuaye nafsi yake juu ya Mungu. Askofu wa Rumi (papa) anatimiza unabii huu. Makasisi wa kanisa la Rumi wanadai kusamehe dhambi, jambo ambalo ni Mungu pekee anaweza kufanya. Hata Yesu alipofanya hivyo wayahudi walitaka kumpiga mawe kwa madai ya kukufuru, Mathayo 9:3. Mara kadhaa hapo nyuma katika machapisho ya kanisa katoliki, papa anadaiwa kushikilia mahali pa Mungu duniani, kwamba ni mwakilishi wa Mungu. Hivyo kufanya jambo lolote ambalo ni Mungu pekee mwenye uwezo wa kufanya ni kukufuru. Kanisa katoliki linakufuru kwa kudai kuwa na uwezo wa kusamehe dhambi. Linakidhi maneno ya unabii yaliyoandikwa, kwamba kichwani kwa mnyama huyu kulikuwa na majina ya makufuru.


Paulo anaendelea kueleza, β€œNa sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake. Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa. Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi,..” 2 Thes 2:6-8. Tumeona kuwa siri ya uasi ilikuwa ikitenda kazi hata wakati wa Paulo lakini kuna mtu alikuwa akizuia uasi huu usifunuliwe kwa mapana yake, ni nani huyu aliyekuwa akizuia? Tumekwisha ona awamu tatu za utawala wa Rumi mwanzoni kabisa mwa hili andiko, na wakati Paulo akiishi ni Rumi ya kipagani ndiyo iliyokuwa na mamlaka chini ya Kaisari. Hivyo ni sahihi kuhitimisha kuwa uwepo wa Rumi ya kipagani katika mamlaka ndiyo nguvu iliyozuia uasi huu usifunuliwe. Historia inaonyesha kuwa mwaka 330 BK Constantine alipohamisha kiti chake cha enzi kutoka mji wa Rome kwenda Constantinople, mji wa Rome ulikabidhiwa kwa askofu wa Rumi (papa). Mwaka 538 BK askofu wa Rumi akawa kiongozi mkuu wa makanisa yote na mrekebishaji wa mafundisho ya uongo. Hivyo kiti cha Rumi kilikaliwa na papa; na mamlaka ya papa yalitoka kwa yule joka.


Tukidumu katika fungu la pili, tunaona mnyama huyu alikuwa kama chui, alikuwa na miguu kama ya dubu na mdomo kama wa simba. Mnyama huyu alikuwa na tabia zote za wanyama wale wa Danieli 7. Kwa maneno mengine ni kwamba utawala huu ulikuwa na tabia za tawala za nyuma zilizopita. Chui aliwakilisha utawala wa uyunani (ugiriki). Tunaona miungu mingi ya kigiriki iliendelea kuabudiwa na rumi, majina tu ndiyo yaliyobadilika. Mfano mungu wa miungu yote ya kigiriki aliitwa Zeus. Ni huyu ambaye kwa warumi aliitwa Jupiter, jina ambalo ilipewa sayari kubwa kupita zote. Huo ni mfano mmoja tu, lakini kuna miungu mingi na taratibu nyingi za ibada zilizoazimwa kutoka ugiriki. Dubu aliwakilisha umedi na uajemi. Sifa kuu ya utawala wa umedi na uajemi ilikuwa kwamba sharia iliyopitishwa haiwezi kubadilika kwa namna yoyote ile. Rumi pia inayo hiyo sifa. Hata ile pembe ndogo (upapa) katika Danieli 7:8 tunaona ilikuwa na macho na mdomo lakini haikuwa na masikio. Hii ni kielezo kuwa Rumi ni ile ile leo na hata kesho. Simba aliwakilisha utawala wa Babeli. Ibada ya jua iliyofanyika katika Babeli yaa zamani iliendelea hata katika Rumi japo kwa namna na majina mengine.


β€œNikaona kimoja cha vichwa vyake kana kwamba kimetiwa jeraha la mauti, na pigo lake la mauti likapona. Dunia yote ikamstaajabia mnyama yule.” Ufunuo 13:3. Pigo la mauti hapa linawakilisha ukomo wa utawala wa papa mwaka 1798 BK ambapo jenerali Berthier, kwa amri ya Napoleon, aliingia Vatican na kumteka papa Pius VI na kumpeleka uhamishoni ambapo alifia huko mnamo mwaka 1799 BK. Likatimia neno la Ufunuo 13:10 β€œMtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga.” β€œNaye akapewa kinywa cha kunena maneno makuu, ya makufuru. Akapewa uwezo wa kufanya kazi yake miezi arobaini na miwili.” Fungu la 5. Miezi arobaini na miwili inayotajwa hapa ndiyo miaka mitatu na nusu kwenye ufunuo 12 na ndiyo siku 1260 ambazo utawala wa papa ulipewa upate kufanya kazi yake na kuwatesa watu wa Mungu. Tukitumia kanuni ya siku sawa na mwaka (Ezekieli 4:6) tunapata miaka 1260. Hii ilianza mwaka 538 BK hadi mwaka 1798 BK upapa ulipopata pigo la mauti. Katika kipindi hiki mamilioni ya wakristo walipoteza uhai wao kwa amri ya askofu wa Rumi.


Pigo la mauti lilipona! Papa Pius VI alipofia uhamishoni huko ufaransa watu wakadhani kuwa mwisho wa upapa umefika, lakini kama andiko lilivyosema, mwaka 1929 BK Benito Mussolini aliingia makubaliano na upapa na kuitambua Vatican kama nchi huru, hivyo mamlaka aliyokuwa nayo papa kama kiongozi wa nchi na dini yakarudi, na kwa kufanya hivyo jeraha lake la mauti likawa limepona. Na hadi leo Papa ndiye kiongozi wa dini zote duniani na pia ni kiongozi wa Vatican kama nchi.
 
TAFSIRI YA MNYAMA WA PILI WA UFUNUO 13.

β€œKisha nikaona mnyama mwingine, akipanda juu kutoka katika nchi; naye alikuwa na pembe mbili mfano wa Mwana-Kondoo, akanena kama joka.” Ufunuo 13:11. Bwana Wesley, katika maelezo juu ya Ufunuo 13 aliyoandika mwaka 1754, akizungumzia mnyama mwenye pembe mbili; β€œHajaja bado, japo hawezi kuwa mbali sana: kwa maana amekusudiwa kuonekana mwishoni mwa miezi arobaini na miwili ya yule mnyama wa kwanza.”



Mnyama wa kwanza alipanda kutoka kwenye bahari, ambayo inaonyesha kuinuka kwake kutoka katika watu wengi na mataifa mengi ya wakati huo (Ufunuo 17:5), wakati huyu wa pili anainuka kutoka katika nchi. Hii inaonyesha kuwa mnyama wa pili angetokea mahali ambapo hapakuwa na watu wengi, wala mataifa, lugha na jamaa. Mwaka 1798, wakati mamlaka ya kipapa yalipotiwa jeraha la mauti, utawala wake ulienea maeneo yote muhimu ya Ulaya, Asia na Afrika; na mahali pekee kwa ajili ya mnyama wa pembe mbili kuendelea palikuwa ni bara la magharibi. Tukilitazama hili bara tunaona marekani ndilo taifa huru lililokuwa na idadi ndogo ya watu kwa wakati huo. Taifa la Marekani lilijitangazia uhuru wake kutoka kwa mkoloni mwingerza tarehe 4 Julai 1776. Hivyo wakati papa Pius VI akichukuliwa kwenda uhamishoni, taifa la Marekani lilikuwa likikua na kujiimarisha.


Pembe huwakilisha utawala au sehemu ya utawala, kama ilivyoainishwa katika Danieli 7:7, 8, 24, 25. Pembe kama za mwana-kondoo zinaonyesha uchanga, kutokuwa na hatia na upole. Soma Great controversy, 442. Pembe mbili zaweza kuwakilisha kanuni zilizoongoza serikali, uhuru wa kisiasa na kidini.


Mbali na kuwa na pembe mbili kwa maana kwamba dini na serikali ni vitu viwili tofauti, mnyama huyu baadae alikuja kunena kama joka! β€œNaye atumia uwezo wote wa mnyama yule wa kwanza mbele yake. Naye aifanya dunia na wote wakaao ndani yake wamsujudie mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona.” Ufunuo 13:12. Sifa kuu ya upapa ilikuwa ni kuunganisha dini na serikali. Kanisa lilipoasi huko zamani likatafuta msaada kwa serikali na hivyo kutumia serikali kuwaadhibu wale ambao walijaribu kwenda kinyume na mafundisho ya kanisa. Ndipo tunasema upapa ulipata nguvu na mamlaka kutoka kwa yule joka. Joka aliwakilisha Shetani lakini kupitia serikali ya Rumi.


Taifa la marekani lilikuwa taifa la kiprotestanti tangu kuanzishwa kwake, na lilikuwa kimbilio kwa wakristo ambao walikimbia mateso kule Ulaya. Ni taifa ambalo lilikuwa na uhuru wa kidini, uhuru wa dhamiri, serikali haikuingilia mambo ya dini. Tarehe 7 Januari 1984, Raisi wa Marekani aliyekuwa madarakani, Ronald Reagan, alimteua balozi kuiwakilisha Marekani huko Vatican; huo ukawa mwanzo wa kujenga mahusiano baina ya Marekani ya kiprotestanti na upapa. Tangu hapo mahusiano baina ya pande hizi mbili yamekuwa yakiimarika siku baada ya siku ikiwemo viongozi kutembeleana. Na kama ilivyotabiriwa; katiba ya marekani imekuwa ikifanyiwa marekebisho kwa zaidi ya mara kumi na nne, lengo na kusudi ni kuondoa uhuru wa dhamiri, uhuru wa kidini, kuunganisha dini na serikali na hivyo taifa la Marekani lililokuwa la kiprotestanti litakuwa limefuata nyayo za Rumi na litakuwa limenena kama joka.


β€œNaye afanya ishara kubwa, hata kufanya moto kushuka kutoka mbinguni uje juu ya nchi mbele ya wanadamu.” Ufunuo 13:13. Taifa la Marekani limekuwa kituo cha ishara na miujiza. Wahubiri wengi wenye kufanya miujiza wametokea katika taifa hili. Kunena kwa lugha kunakofanywa leo miongoni mwa wakristo kulianzia Marekani mwanzoni mwa miaka ya 1900. Watu wanadai kushukiwa na Roho mtakatifu lakini ukweli ni kwamba moto unaowaka ndani ya hawa watu siyo moto wa mbinguni bali ni moto wa kigeni! Vuguvugu la karismatiki ambalo linaenea kwa kasi miongoni mwa wakatoliki pia limeanzia katika taifa hili. Vuguvugu la kizazi kipya na wahubiri wakubwa wa mambo hayo chanzo chao ni Marekani. Dini nyingi za siri zinazomwabudu Lusifa zimeanzishwa katika taifa hili.


β€œNaye awakosesha wale wakaao juu ya nchi, kwa ishara zile alizopewa kuzifanya mbele ya huyo mnyama, akiwaambia wakaao juu ya nchi kumfanyia sanamu yule mnyama, aliyekuwa na jeraha la upanga naye akaishi. Akapewa kutia pumzi katika ile sanamu ya mnyama, hata ile sanamu ya mnyama inene, na kuwafanya hao wote wasioisujudu sanamu ya mnyama wauawe.” Ufunuo 13:14-15. Juu ya sanamu ya mnyama, Ellen G White anaandika, β€œsanamu ya mnyama inawakilisha namna ya uprotestanti ulioasi ambao utaundwa wakati makanisa ya kiprotestanti yatakapotafuta nguvu ya serikali kwa ajili ya kushurutisha watu wafuate mafundisho yao ya dini” The great controversy ukurasa wa 445.


β€œNaye awafanya wote, wadogo kwa wakubwa, na matajiri kwa maskini, na walio huru kwa watumwa, watiwe chapa katika mkono wao wa kuume, au katika vipaji vya nyuso zao; tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza, isipokuwa ana chapa ile, yaani, jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake.” Ufunuo 13:16-17. Baada ya makanisa ya kiprotestanti kuungana katika baadhi ya vipengele vya mafundisho ambavyo wanafanana hasa hasa ibada ya jumapili, yatashinikiza serikali kuweka sheria kwa kuifanya jumapili kuwa siku ya mapumziko na adhabu kutolewa kwa wale ambao watakiuka agizo hilo.


Kutiwa chapa katika mkono wa kuume ni kukubali kutii agizo kwa kutofanya kazi. Katika vipaji vya uso ni kusadiki au kuamini ya kwamba agizo hilo ni halali. Funuo 13:18, hesabu ya mnyama ni namba 666. Kofia ya papa imeendikwa kilatini "VICARIUS FILII DEI" ambayo tafasiri yake ni Vicar of the Son of God. Maana yake ni aliye badala ya Mwana wa Mungu. Ukilinyambulisha hilo neno VICARIUS FILII DEI kwa kutumia herufi za kirumi unapata jumla ya namba 666.
 

Unachokifanya ni mambo ya "kipagani" sana katika Mijadala.Mjadala ni juu ya fomula ya Miller na mwendelezo wake uliofanywa na wasabato kama ninyi juu ya tarehe ya kurudi kwa Yesu.Badala ya kujenga hoja juu ya vijenzi vya hoja kuu(premises) wewe umekuja na mada mpya kabisa! Unataka tukuweke katika kundi gani katika tasnia ya mijadala ya kisomi?
 
Nyie Wasabato mpoje? Huo ndio UPINGA KRISTO ,Yesu alisema jihadharini na manabii wa Uongo Sasa wewe unaona hakuna shida kutafsiri au kutabiri uongo


Matayo 7:15-19
Manabii Wa Uongo
15 β€œJihadharini na manabii wa uongo wanaowajia wakiwa wamevaa ngozi ya kondoo, kumbe ndani ni mbwa mwitu wakali. 16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je, unaweza kuchuma zabibu kwenye miiba au tini kwenye michongoma? 17 Vivyo hivyo mti mzuri huzaa matunda mazuri na mti mbaya huzaa matunda mabaya. 18 Mti mzuri hauwezi kuzaa matunda mabaya na mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri. 19 Kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa katwa na kutupwa motoni.20 Hivyo, mtawatambua kwa matunda yao.”
 


πŸ™πŸ™πŸ™ perfect umeeleza vzr sana lengo kuu ni kuwaattack wasabato akidhani hawana ushahidi na uelewa wa kupinga hayo maneno yake
 
Aisee...atatoka lini humo chumbani? Yaani ni ngumu sana kufuta spiritual mistakes za mtu bila kumkana. Kwanini msiseme miller na Helen walikosea...halafu nyinyi mkafata njia sahihi hii cover ups haiwajengi inazidi kuwaboboa. Miller na hellen bi simba destroyed you big time...mtupeni pembeni muendelee na imani sahihi
 
Anawaombea watenda dhambi kwa Baba yake. Mtu anapoomba msamaha wa dhambi, Yesu anayapeleka maombi hayo kwa Baba yake kwa ajili ya msamaha.
Hii ni mpya...yesu anaomba sisi tusamehewe au yeye ndo anatusamehe dhambi. Mkuu unaenda OP sana. Ndiyo maana watu huwema wasabato si wakristo..naona mnaspiritual flaws nyingi kuliko nilivyodhani mwanzoni. Kosa kubwa ni kuchukua mawazo ya mtu na kuyafanya ndiyo msimamo wa imani. Hellen amwkuwa kama Mao na red book
 
Kuhusu kusali jumapili zitto junior alifafanua vizuri sana ktk ile mada ya mitale na midimu ya kuumbwa kwa siku ya saba hapa huna jipya.
 
πŸ™πŸ™πŸ™ perfect umeeleza vzr sana lengo kuu ni kuwaattack wasabato akidhani hawana ushahidi na uelewa wa kupinga hayo maneno yake
Msubiri tuwaoneshe jinsi Ellen G White alivyopinga Utatu Mtakatifu mpaka GC kuficha nyaraka zake
 
Wanafanya hivyo kwa kuwa Ellen G White alimfananisha Yesu na Malaika Mikaeli..

Yani Wasabato wanapinga Yesu si Mungu ila Malaika Gabrieli...hivyo usishangae wao kudai Yesu alijibanza kwenye kachumba huko mbinguni
 
πŸ™πŸ™πŸ™ perfect umeeleza vzr sana lengo kuu ni kuwaattack wasabato akidhani hawana ushahidi na uelewa wa kupinga hayo maneno yake
Hivi hujui Ellen G White alisema Yesu sio Mungu ila Malaika Gabrieli...

Tembelea JF tutakujuza
 
Hivi hujui Ellen G White alisema Yesu sio Mungu ila Malaika Gabrieli...

Tembelea JF tutakujuza
Huo ni uongo...hakuna sehemu EGW alipinga kuwa Yesu si Mungu. UONGO. Biblia inamtaja Yesu kuwa Mikaeli, malaika mkuu, lakini haimanishi kuwa Yesu si Mungu. Hilo ni jina lake jingine kama alivyoitwa mwana kondoo wa Mungu, au simba wa Yuda. Usipotoshe watu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…