William Ruto na dhihaka kwa ujio wa Obama!

William Ruto na dhihaka kwa ujio wa Obama!

[“Nchi yetu inamcha Mungu...]

Tafsiri ya kweli kumcha Mungu kwa Wakenja ni ipi nikiangalia mauaji ya kisiasa (Tom Mboya, Kariuki, Rift Valley) na tofauti ya maskini na tajiri, .. Ongeza unyakuaji ardhi hata za misitu, mijini na za maskini. LoL Ha ha ha.
Kesi ya The Hague inatoka wapi? kama wanamcha mungu?. Mungu wao ni yupi Lenana Peak au?
 
Sisi tutapokea akina Obama na wenzake na kupiga picha nao lakini ni mwisho wa siku maendeleo kama hatujajipanga tutayasikia kwenye maandishi huku rasirimali zetu zikiondoka mchana kweupe huku tukiwapigia mizinga 21 wezi wa rasirimali zetu!
 
Wao wana rasilimali za kuiba kwani?
 
Wao wana rasilimali za kuiba kwani?

Zipo, lakini huko walishajiimarisha toka kitambo sana. unajua Tanzania ni mke mpya, kwa hiyo lazima Marekani itumie jitihada zaidi kumfurahisha mke huyu mpya. na kama kawaida wake wenza, tushaanza kuchora vidole ardhini, shingo upande, kisha tunamsonya mke mkubwa kenya kwa uzi kama huu ulioletwa
 
Nakubaliana na hoja iliyoko hapo kwenye red japo sikubaliani na hoja za Rais wa Senegal ambazo Ruto amezitumia kama rejea. Rais wa Senegal "amejitetea" mbele ya Obama kwamba hawezi kuruhusu "haki za mashoga" just because Senegal ina "waislamu wengi". Utetezi mfu kabisa kwa Rais wa nchi.

kwann usipeleke makalio yako ili ukubaliane na ushetani
 
1044412_10152967666520713_706893635_n+(1).jpg

Huu ni uchokozi
 
Mkuu wakati anaahidi kutembelea Kenya walikuwa hawajawachagua hawa washtakiwa wa ICC! .

Sababu kubwa iliyomfanya asitembelee Kenya ni kutokana na kesi inayowakabili Raisi na Makamu wake ICC.
Umemaliza.na hivi ndivyo ilivyo na ndivyo Obama alivyosema.hawa ni watuhumiwa wa ICC,msidanganyike eti hawamind wee!!kasema nani???wakenya nchi nzima hawakwenda kazini kusherehekea ushindi wa Obama awamu ya kwanza halafu wasikie mtoto wao anatembelea nyumba ya jirani na kwao hataki kwenda,hata wewe ingekuuma tu wana wakati mgumu ila kikombe hicho hawawezi kukikwepa.
 
Ataenda akistaaf kama kusalimia familia ya babaake!
 

Attachments

  • uploadfromtaptalk1372692904030.jpg
    uploadfromtaptalk1372692904030.jpg
    28.1 KB · Views: 173
Na bora hajaenda maana hawa jamaa walivyo makabila watakua walishamuandalia na mke wa kwao kabisa.
 
hao akina ruto wanajiliwaza bure na kutaka kenyans wasione kama ni issue obana ku-skip nchi yao. Kwani hawajui kuwa wao ndo kikwazo cha obama kutokwenda kenya??

Hawa viongozi wengine ni wanafiki tu!
Akipanga ratiba ya kwenda utawaona wakipigana vikumbo kumpa mkono!
Hata hvyo Obama hajatoka madarakani huenda akaenda Kenya!
Hawa ni majirani zetu zaidi ya USA...hatuna haja ya kujifanya kichwa kwa sababu ya ziara ya Obama kwetu!
Wote bado tu maskini wa akili na hali japo maiti hazidiana harufu......!
 
Kumbe kutembelewa na Obama ni ujiko? Sikujua hilo, Kama walinzi wake tu wana fanya sorting ya mawaziri and other gorvernment officials wa kwenda kumsalimu, ni dhihaka kiasi gani hiyo? Mzee mchonga aliisha wahi mpa kifimbo chake Malkia Elizabeth!

Hakuwa na ubavu huo , hata ule unga wa Yanga tusingeuona.
 
Ruto alikuwa anajifariji kwa kusema kwamba ziara ya Obama ni nothing more than promotion ya ndoa za jinsia moja wakati hapa Dsm Obama hajataja hayo mambo kabisa alikuwa anaongelea issue za kiuchumi na kisiasa.
 
Kumbe kutembelewa na Obama ni ujiko? Sikujua hilo, Kama walinzi wake tu wana fanya sorting ya mawaziri and other gorvernment officials wa kwenda kumsalimu, ni dhihaka kiasi gani hiyo? Mzee mchonga aliisha wahi mpa kifimbo chake Malkia Elizabeth!

Udhalilishaji waliotufanyia hawa Marekani wa kutupangia mpaka mawaziri wa kwenda kuonana na Obama, usingefanyika enzi ya utawala wa "MUSSA"!!
 
attachment.php



WanaJF!

Nimekuwa nikiwaza mahusiano ya Tanzania na nchi jirani za Afrika ya mashariki baada ya ujio wa Obama yatakuwaje?

Kwani inasemekana kitendo cha Obama kuja Tanzania na kuiruka Kenya, kimeleta gumzo, sio tu ndani ya Kenya, bali hata mataifa mengine yameshangazwa na kitendo hicho. Kwani ukizingatia asili ya rais Obama na ahadi yake kwa Kenya, ni wazi kwamba alipaswa atembelee na Kenya kama sehemu ya ziara yake hapa Afrika mashariki.

Sitakuwa na mengi ya binafsi juu ya hili la Ruto na dhihaka yake kwa ujio wa Obama Afrika, bali nime ambatanisha maelezo yake mwenyewe kama ifuatavyo;


NAIBU wa Rais Bw William Ruto, jana alivunja kimya chake kuhusu hatua ya rais wa Marekani Barack Obama kutozuru nchini Kenya kwa kusema hatua hiyo haina madhara yoyote kwa Kenya.

Huku akiongea katika kanisa la Katoliki la St Gabriel Bahati, kaunti ya Nakuru, Bw Ruto alisema "nchi hii ina 'marafiki’ wengine wengi duniani ambao inaweza kushirikiana nao huku akiongezea kuwa hatua ya rais Obama kukwepa kutembelea Kenya haiwezi kutatiza kwa vyovyote vile uhusiano mwema uliopo wa kibiashara baina ya Marekani na Kenya."

Bwana Ruto akasema, “Tunaiheshimu nchi ya Marekani nayo inafaa kuwaheshimu Wakenya,”

Alisema serikali ya Kenya tayari imeanzisha mikakati ya kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na mataifa mengine huku akikariri kuwa safari ya Rais Uhuru Kenyatta nchini Uganda ambapo alikutana na rais wa nchi hiyo Yoweri Museveni na mwenzao wa Rwanda rais Paul Kagame kujadili jinsi nchi hizo tatu zinaweza kushirikiana kibiashara, ni miongoni mwa mikakati hiyo.

Pia akaongezea, “Nchi yetu inamcha Mungu na kamwe hatutaruhusu mataifa ya kigeni kutuletea tamaduni ambazo zinakinzana na desturi zetu,” akasema Bw Ruto huku akirejea hotuba ya Rais Obama nchini Senegal ambapo aliitaka nchi hiyo kuheshimu haki za Mashoga."
Obama atatembelea akimaliza uongozi wake kama mtu mwenye asili ya Kenya na sio sasa... kwa sasa wamalizane na ICC kwanza... uraisi wa marekani ni taasisi sio matakwa ya obama... USA stands against violency and it will contradict if he visits now... well done Obama...
 
Kenya wana wivu wa kijinga sana, nilikuwa naangalia TV moja ya kenya leo asubuhi imenishangaza sana sikujua kama hiliswala la Obama kuja Tanzania limewaathiri kwa kiasi kikubwa hivyo. mtangazaji mmoja akasema "Obama angekuja Kenya akae hata masaa mawili", mwingine akasema "hata bila US kenya itaendelea tu na inazidi kusonga mbele." Yaani Wakenya wamekuwa very desperate, wanatamani hata kulia. Huku Watanzania wengi wanaona hiyo ni ishu ya kawaida sana kutembelewa na marais wa US ambao huja kuzoa utajiri wetu.

Kuna presentative mmoja wa kikenya(BBC Swahili) kasema hata angetua tu airpot akawapungia mkono ingetosha kabisa...aisee nikashangaa sana!!
 
Udhalilishaji waliotufanyia hawa Marekani wa kutupangia mpaka mawaziri wa kwenda kuonana na Obama, usingefanyika enzi ya utawala wa "MUSSA"!!

inasikitisha saana...i do agree with the Obama's arrival especially in economic aspects but kwa hili la kuamua wenyewe nani aonane nae ni ufinyu wa maamuzi kwa serikali yetu kwa sababu hata Rais wetu angeweza kupanga kwa kuzingatia vigezo vya usalama pia.
 
Aende asiende what difference does it make?Stupid Africans.
naona umeongea kiingereza inaonyesha kama msomi au ndo wale wa shule za english medium lakini kichwani hakuna.Hoja ya kimsingi hapa fedha iliyotolewa kwenye miradi ya umeme ikasimamiwa ipasavyo , je tutabaki kama mwanzo na upungufu wa umeme?hizo ni fedha tumepewa misaada ni wajibu wetu sasa kusimamia kuleta maendeleo , ni hatua kuliko hapo awali.jamani tuwe wachambuzi wa kila kitu kulaumu, kubeza, kudharau, pale kwenye hatua ya maendeleo lazima tusema na tupongeze maana pesa ni pesa hata kama imetokea chooni , ina msaada kwenye hatua ya kutatua hoja za manunuzi.Mradi huo wa umeme ni nchi nyingi wanautaka na hawajapa, hivyo mdau jipongeze kuona kuwa nasi hata kama ni watu wa mikataba mibovu , lakini pesa tumepewa itusaidie.Ni wajibu wa bunge letu kuisimamia serikali utekelezeke ipasavyo na si kubweteka baadaye kuja na malalamiko.
 
Uhuruto wanajua sana sabu za obama kutokwenda kenya..wamalizane na ICC,na nina uhakika hawaponi,ruto mwenyewe juzi tu mahakama imemuamuru arudishe shamba heka mia alilojimilikisha kiufisadi..wameze wembe tu..hichi kidogo tulichopata kama kitatumika vizuri tutapiga hatua kubwa sana
 
Back
Top Bottom