Unajua mkuu nimepitia maisha ya shida sana, moja vitu nilivyo pitia ni pamoja na kunyonywa sana au kupunjwa. Pamoja na yote nilikuwa mvumilivu sana, machozi yangu yalikuwa moyoni sio kwa uwazi kama dada Rubby anavyo fanya. Lakini leo nimejua faida ya kupitia yote hayo, leo nikisimama ni mwanaume hasa yote kwa sababu nilikuwa mvumilivu na bado ni mvumilivu. Darasa la saba nimekuja kwa Treni ya ng'ombe hapa mjini. Leo nakula ubaridi kwangu mpaka kwenye usafiri nakula hewa ya Japan sio mchezo. Yote kwa sababu ya uvumilivu. Uvumilivu ni silaha mpaka kwenye mapenzi.