Cannabis
JF-Expert Member
- Jan 20, 2014
- 11,557
- 33,535
Wimbo wa msanii nguli wa bongo flava Harmonize unaoitwa sandakalawe, umezuiwa youtube kutokana na kile kinachosemwa kuwa ni kukiuka hakimiliki za kampuni ya usambazaji mziki ya EMPIRE. Mpaka sasa haijajulikana ni kipengele kipi cha hakimiliki kilichokiukwa lakini tetesi zinasema ni shutuma za wizi wa wimbo ambao unasambazwa na kampuni ya EMPIRE.
Hii si mara ya kwanza kwa Harmonize kukumbwa na matatizo ya hakimiliki dhidi ya wasanii wengine, wimbo wake wa "Your Body" unaofanana na wimbo wa Papa Wemba wa "show me the way" alioshirikiana na Burna Boy kutoka nchini Nigeria uliondolewa kwenye album yake ya Afro East kutokana na matatizo ya haki miliki.
Pia amewahi kukwazana na wasanii mbali mbali kama Magix Enga kutoka Kenya, Rosa Ree kutoka Tanzania na wasanii chipukizi Lizu Dady na Phamo S kwa shutuma zinazofanana za kutumia nyimbo zao bila ya maelewano.
Mpaka sasa msanii huyo hajatoa neno lolote baada ya hit song hiyo kufungiwa kwenye mtandao wa youtube.