Sasa tunawakumbuka
Walio kufa kwa tabu
Bila hata matibabu
Wengi hawana hesabu
Walio kufa kwa tabu duniani
Mwana Lumumba wa kongo
Alimpiga vigongo
Wakamvunja mgongo
Wakamtoa ubongo
Wala sisemi uongo
Ni ukweli
Tom mboya wa Kenya
Si kiongozi mbaya
Kala risasi ya taya
Maharamia wabaya
Wala hawaoni haya kumuua
Na maiti na maiti si mwingine ni amini
Wananchi ndugu zangu mwasikia
Maneno yaliyo semwa majuzi huko Uganda
Maiti nazo husema aaaa
Wacha Tanzania utaitambua.
Amini kapiga ngoma gaddafi kaimba wimbo
Maiti nazo husema aaa wacha tanzania utaitambua
Gaddafi wewe Tanzanian utaitambua
Amini wewe Tanzanian utaitambua