Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 144
SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imesema inakusudia kupiga wimbo wa taifa katika kikao cha baraza la wawakilishi kijacho kutokana na marekebisho ya kanuni za baraza la wawakilishi zilizofanywa na wajumbe wa baraza hilo.
Waziri wa Nchi Afisi ya Waziri Kiongozi Hamza Hassan Juma aliwaambia wajumbe wa baraza hilo wakati akifanya majumuisho ya kanuni za baraza la wawakilishi toleo la mwaka 2007 katika kikao hicho kinachoendelea kwa wiki ya tatu sasa.
"Kuimbwa wimbo wa taifa katika baraza letu hili tukufu litawathibitishia wale wanaosema Zanzibar sio nchi wanajua sasa kama hii ni nchi kamili ninachoomba kwa wajumbe hivi sasa waanze kujifunza wimbo huo wa taifa waaze mazoezi ya kuuhifadhi mapendekezo yakipita tu kikao kijacho tunaanza na kuweka CD yetu ambayo itatuongoza na sisi wajumbe sote tutaanza kuimba" alisema Waziri huyo kwa kujiamini.
Kwa mujibu wa marekebisho ya kanuni ya 27 pendekezo la kupigwa wimbo wa taifa limeelezwa kuwa ni kujenga utaifa na kukuza uzalendo wa wajumbe na wananchi wote kwa jumla pamoja na kutoa ishara ya umuhimu wa shughuli zinazofanywa na baraza kitaifa.
Katika marekebisho mengine ya kanuni hizo imependekezwa kwua utaratibu wa uchaguzi katika kuwatafuta wajumbe wa baraza wanaochaguliwa na baraza ili kuwa wajumbe wa tume ya bajeti urekebishwe ili wanaocfhaguliwa wasiwe mawaziri, wala manaibu wala wakuu wa mikoa na angalau mmoja kati yao ni lazima awe mwanamke.
Waziri Hamza alisema kanuni ya 143 mapendekezo hayo yanalenga kuipa uhuru zaidi tume hiyo na kuzingatia usawa wa kijinsia katika vyombo vya kufanya maamuzi ya baraza la wawakilishi.
Waziri huyo pia alisema katika marekebisho mapya marekebisho yamependekeza katika kanuni ya 10 kuwa wenyeviti wa baraza wawe wawili badala ya mmoja kama ilivyo na uchaguzi wao uzingatie jinsia.
Pendekezo hili linalenga kutoa fursa ya kijinsia katika "uongozi wa baraza. Hata hivyo endapo itatokezea waliojaza fomu na kuomba kuchaguliwa wenyeviti ni wajumbe wa jinsia moja tu basi uchaguzi utafanyika kwa wajumbe hao walioomba. Aidha kuna mapendekezo yanayotolewa kwa ajili ya kuoainisha maneno yaliyotumiwa kwenye kanuni na yale yaliotumiwa kwenye katiba. Mfano wa marekebisho hayo ni kanuni ya 59(10)"alisema Waziri huyo.
Katika marekebisho hayo kamati ya PAC inapendekezwa ipewe uwezo zaidi inapopitia hoja za mshibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali ili ijiridhishe pia kwa kiwango cha fedha kinachotumika kulingana na thamani halisi ya kitu au kazi iliyofanywa au kitu kilichonunuliwa (value for money), (kanuni 112).
"Spika atalazimika kukubaliana na ushauri wa kamati ya maadili na endapo atakuwa na mawazo tofauti atapaswa apeleke ushauri huo kwneye baraza kwa uwamuzi wa mwisho (kanuni 114) vile vile idadi ya wajumbe wa kamati teule inapendekezwa iongozwe kupitia marekebisho ya kanuni 115 halikadhalika inapendekezwa kuwa mwenyekiti wa kamati teule awe na kura ya uwamuzi tu bila ya kura ya kawaida" amesema Waziri Hamza.
Katika marekebisho hayo ya kanuni pia kuna marekebisho yanayopendekezwa ili kuondoa kasoro zinazoonekana kuathiri utekelezaji wa kanuni zenyewe. Mapendekezo ya aina hiyo ni pamoja na utekelezaji wa kanuni zenyewe.
"Mapendekezo ya aina hii na marekebisho ya kanuni ya 24 ambayo yanalenga kumpa uwezo Spika kuahirisha kikao cha baraza bila ya kuwahoji wajumbe endapo shughuli za kikao zimemalizika mapema kabla ya kufikia muda wa kawaida wa kuahirisha baraza" alisema Waziri huyo na kusisitiza kwamba kifungu hicho ni muhimu kwa kuwa ipo siku wajumbe watafanya vituko kwa kumkatalia Spika kumaliza shughuli na kubakia kutazamana hivyo kufanyiwa marekebisho hayo kutaongeza ufanisi.
Hata hivyo Waziri huyo alisema inapendekezwa kwamba endapo mapendekezo ya marekebisho hayo yatakubaliwa na kupitishwa basi yaanze kutumika kwenye mkutano ujao wa 18 wa baraza la wawakilishi yaani kikao kinachokuja.
Wakitoa maoni yao wajumbe wa baraza hilo wamekubaliana na hoja zilizotolewa na zaidi hoja ya kupigwa wimbo wa taifa wamesema itakuwa ni furaha ya kuonesha kuwa Zanzibar hivi sasa inaonesha kuwa ni nchi kwa kupigwa wimbo huo ambao kwa muda mrefu wajumbe hao walikuwa wakiulilia na kutaka utumike katika chombo hicho muhimu cha kutunga sheria.
SOURCE:ZANZIBAR YETU WEB BLOG.
Waziri wa Nchi Afisi ya Waziri Kiongozi Hamza Hassan Juma aliwaambia wajumbe wa baraza hilo wakati akifanya majumuisho ya kanuni za baraza la wawakilishi toleo la mwaka 2007 katika kikao hicho kinachoendelea kwa wiki ya tatu sasa.
"Kuimbwa wimbo wa taifa katika baraza letu hili tukufu litawathibitishia wale wanaosema Zanzibar sio nchi wanajua sasa kama hii ni nchi kamili ninachoomba kwa wajumbe hivi sasa waanze kujifunza wimbo huo wa taifa waaze mazoezi ya kuuhifadhi mapendekezo yakipita tu kikao kijacho tunaanza na kuweka CD yetu ambayo itatuongoza na sisi wajumbe sote tutaanza kuimba" alisema Waziri huyo kwa kujiamini.
Kwa mujibu wa marekebisho ya kanuni ya 27 pendekezo la kupigwa wimbo wa taifa limeelezwa kuwa ni kujenga utaifa na kukuza uzalendo wa wajumbe na wananchi wote kwa jumla pamoja na kutoa ishara ya umuhimu wa shughuli zinazofanywa na baraza kitaifa.
Katika marekebisho mengine ya kanuni hizo imependekezwa kwua utaratibu wa uchaguzi katika kuwatafuta wajumbe wa baraza wanaochaguliwa na baraza ili kuwa wajumbe wa tume ya bajeti urekebishwe ili wanaocfhaguliwa wasiwe mawaziri, wala manaibu wala wakuu wa mikoa na angalau mmoja kati yao ni lazima awe mwanamke.
Waziri Hamza alisema kanuni ya 143 mapendekezo hayo yanalenga kuipa uhuru zaidi tume hiyo na kuzingatia usawa wa kijinsia katika vyombo vya kufanya maamuzi ya baraza la wawakilishi.
Waziri huyo pia alisema katika marekebisho mapya marekebisho yamependekeza katika kanuni ya 10 kuwa wenyeviti wa baraza wawe wawili badala ya mmoja kama ilivyo na uchaguzi wao uzingatie jinsia.
Pendekezo hili linalenga kutoa fursa ya kijinsia katika "uongozi wa baraza. Hata hivyo endapo itatokezea waliojaza fomu na kuomba kuchaguliwa wenyeviti ni wajumbe wa jinsia moja tu basi uchaguzi utafanyika kwa wajumbe hao walioomba. Aidha kuna mapendekezo yanayotolewa kwa ajili ya kuoainisha maneno yaliyotumiwa kwenye kanuni na yale yaliotumiwa kwenye katiba. Mfano wa marekebisho hayo ni kanuni ya 59(10)"alisema Waziri huyo.
Katika marekebisho hayo kamati ya PAC inapendekezwa ipewe uwezo zaidi inapopitia hoja za mshibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali ili ijiridhishe pia kwa kiwango cha fedha kinachotumika kulingana na thamani halisi ya kitu au kazi iliyofanywa au kitu kilichonunuliwa (value for money), (kanuni 112).
"Spika atalazimika kukubaliana na ushauri wa kamati ya maadili na endapo atakuwa na mawazo tofauti atapaswa apeleke ushauri huo kwneye baraza kwa uwamuzi wa mwisho (kanuni 114) vile vile idadi ya wajumbe wa kamati teule inapendekezwa iongozwe kupitia marekebisho ya kanuni 115 halikadhalika inapendekezwa kuwa mwenyekiti wa kamati teule awe na kura ya uwamuzi tu bila ya kura ya kawaida" amesema Waziri Hamza.
Katika marekebisho hayo ya kanuni pia kuna marekebisho yanayopendekezwa ili kuondoa kasoro zinazoonekana kuathiri utekelezaji wa kanuni zenyewe. Mapendekezo ya aina hiyo ni pamoja na utekelezaji wa kanuni zenyewe.
"Mapendekezo ya aina hii na marekebisho ya kanuni ya 24 ambayo yanalenga kumpa uwezo Spika kuahirisha kikao cha baraza bila ya kuwahoji wajumbe endapo shughuli za kikao zimemalizika mapema kabla ya kufikia muda wa kawaida wa kuahirisha baraza" alisema Waziri huyo na kusisitiza kwamba kifungu hicho ni muhimu kwa kuwa ipo siku wajumbe watafanya vituko kwa kumkatalia Spika kumaliza shughuli na kubakia kutazamana hivyo kufanyiwa marekebisho hayo kutaongeza ufanisi.
Hata hivyo Waziri huyo alisema inapendekezwa kwamba endapo mapendekezo ya marekebisho hayo yatakubaliwa na kupitishwa basi yaanze kutumika kwenye mkutano ujao wa 18 wa baraza la wawakilishi yaani kikao kinachokuja.
Wakitoa maoni yao wajumbe wa baraza hilo wamekubaliana na hoja zilizotolewa na zaidi hoja ya kupigwa wimbo wa taifa wamesema itakuwa ni furaha ya kuonesha kuwa Zanzibar hivi sasa inaonesha kuwa ni nchi kwa kupigwa wimbo huo ambao kwa muda mrefu wajumbe hao walikuwa wakiulilia na kutaka utumike katika chombo hicho muhimu cha kutunga sheria.
SOURCE:ZANZIBAR YETU WEB BLOG.