Pia haka kawimbo mara ya kwanza kukadaunlodi nikajua nimeingia chaka...coz kwa jinsi unavyoanza huwezi kuuzania kama ndo ule ambao unawapaga watu jambajamba wanapousikiaga.
Barantanda kasahau kueleza kitu cha Muhimu ktk ule wimbo.
Amesahau kuwajulisha wazalendo kuwa wimbo ule upo ktk mahadhi ya Pop, chakacha, country, jazz, yenu, nk nk nk nk...
Ok wimbo ule uko katika mahadhi ya Opera.
Opera ni aina za nyimbo zinazoaminika kuwa ndo nyimbo ngumu zaidi kuimba.
Na mfalme wa nyimbo hizo ni Hayati Luciano Pavarotti.
Watu wa soka weeengi ulimwenguni wamezoea kuuita wimbo ule kuwa ni wimbo wa AC Milam.
Coz inaaminika kuwa kabla ya mechi kuanza timu zinapokuwa zinatoka vyumbani na kwenda kujipanga uwanjani wachezaji wa Milan enzi hizo wakiongozwa na Paolo Maldini, seedorf, pirlo, cafu, stam, ambrosini, rui costa, pippo the poucher, shevchenko, gattuso na dida basi inakuwa kama vile wanapigiwa wao yani.
Pia napenda kuliweka wazi hili kuwa msimu huu wa ligi ya serie A ni wazi kuwa AC Milan haikuanza vizuri.
Na ktk hili makamu wa rais wa klabu hii muheshimiwa Adriano Galliani alikuwa anaingia na redio kwenye chumba cha mapumziko ktkt ya mechi huku redio ikipiga wimbo huu.
yeye aliamini kuwa AC huwa wako makini sana ktk mashindano ya ulaya. So wanapousikia wimbo huo ni wazi kuwa watakuwa makini na katika hilo mzee huyu alifanikiwa kwa kiasi kikubwa kuamsha morari ya timu.
Kisha baada ya kukaa sawa aliachana na mbinu ile.
Forza Milan...