asante sana mpendwa nawe nakutakia kila la heri kwa kila mkono wako unalotia bidii kulifanyaMungu akubariki sana
Tusubirie tu naona atatuletea ready madepole na maandalizi dada. sasa ma-best gal nguo tunashonesha lini,manake mie fundi wangu wa manzese yuko busy ibidi booking mapema. ama shem anatuagizia ulaya? navaa size zero,lol
pole na maandalizi dada. sasa ma-best gal nguo tunashonesha lini,manake mie fundi wangu wa manzese yuko busy ibidi booking mapema. ama shem anatuagizia ulaya? navaa size zero,lol
Tusubirie tu naona atatuletea ready made
hahaha, kwa kweli kwa sasa sijaanza kupangilia masuala ya nguo, hata rangi ya harusi sijaichagua, lol! nimetingwa na mambo mengine chungu mzima, tuombe Mungu taratibu tutafika tu wapendwa
stay blessed!
hehehe, hebu fanya mipango bana manake tushajiwahia u-bestigeli hapa manake na sie tuna hamu ya kupigwa picha atii! usijali mamii, yeye aliyeianzisha kazi hii ndani yako ataimaliza yeye mwenyewe na utashangaa mambo yatakavyoenda sawa bila nguvu nyingi.
1.
Nimepata wa thamani, ni hakika si majungu,
Mwingine sitatamani, nimefunga moyo wangu,
Sikupotea ramani, nimezikubali pingu,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
2.
Kila nionapo wingu, sikosi kuona mbingu,
Huwezi ingia mbingu, bila liingia wingu,
Wingu liko na mbingu, mbingu zina mawingu,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
3.
Hayawi hayawi yawa, thelathini siku zawa
Sio nyingi kama chawa, zi nyepesi kama buwa,
Kwa sala na zote duwa, maombi yamejibiwa,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
4.
Tangu tulipozianza, ndoto za baba na mama,
Ni mengi tumejifunza, tukabakiza kuhama,
Na sasa twende kufyonza, tamu iliyofichama
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
5.
Mwaka ule si karibu, subira ndio mtaji,
Tele hayo majaribu, yasiyopozwa na maji,
Imara kama bawabu, makini kama hujaji,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
6.
Nyakati nayo majira, na zama zimetimia,
Mapenzi haya imara, silaha kuu ya ndoa,
hazijalishi ngawira, mapendo tumekamia,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
7.
mpira ulipoupiga, niliepa nisidake,
kwa mengi ulinikoga, japo hunayo makeke,
na sasa nimejibwaga, hirimu wangu nishike,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
8.
za mwizi hazikawii, zetu walizikamia,
pamoja nayo bidii, ya maombi kuazimia,
agizo sasa kutii, la ndoa na familia,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
9.
asante mpenzi wangu, kimasomaso menitoa,
mapendo kama uchungu, kwa machozi nimeloa,
lishike vizuri rungu, kwako nimeshajitoa,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
10.
tuijenge hiyo nyumba, yenye kujaa vicheko,
watoto nao kuumba, mbinguni tupate heko,
wala tusije kuyumba, kwani tunao upako,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
11.
udumu cha nyumba kichwa, mimi ni wako ubavu,
bidii ipite mchwa, ushinde wote uchovu,
nyuma tusije kuachwa, kwa Yesu uko wokovu
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
12.
Asante wote wapendwa, kwa maombi nazo dua,
Ni kweli hamkushindwa, shetani kumkemea,
Upendo uliopandwa, hitaji kuu la ndoa,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
wapendwa,
pamoja na kuzidiwa na majukumu mengi kikazi, Mungu aliyajibu maombi tena vizuri sana. mchumba wangu anaitwa Naiman na ni mzaliwa wa Iringa. kama mjuanvyo masuala haya yana logistics nyingi na hivyo kukamilisha yote yaliyo ya muhimu inahitaji muda. hadi sasa mengine hayajakamilika. hapo katikati nilibahatika kupata scholarship ya kuripoti chuoni september mwaka huu na hivyo mtaona kuna kibarua cha kupangilia mambo hapo, kupata ruhusa na likizo ya masomo kazini na kuandaa harusi na wakati huohuo kutakiwa kuwa chuoni. so baada ya panga pangua, natarajia kwenda chuoni kwanza na kisha kurudi nyumbani november kwa ajili ya kufunga ndoa.
Mungu awabariki sana,
Glory to God!
Mtarajiwa wa kiume na imagine ana hali gani saa hizi
Ina maana hii ni kaole au?Usanii bin masanja mkandamizaji tumeshitukaaaa ha hha hhaa ha ha nimeiba password ya Dena .........................
Ndoa hapa ipo kweli gaga?
Ina maana hii ni kaole au?
1.
Nimepata wa thamani, ni hakika si majungu,
Mwingine sitatamani, nimefunga moyo wangu,
Sikupotea ramani, nimezikubali pingu,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
2.
Kila nionapo wingu, sikosi kuona mbingu,
Huwezi ingia mbingu, bila liingia wingu,
Wingu liko na mbingu, mbingu zina mawingu,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
3.
Hayawi hayawi yawa, thelathini siku zawa
Sio nyingi kama chawa, zi nyepesi kama buwa,
Kwa sala na zote duwa, maombi yamejibiwa,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
4.
Tangu tulipozianza, ndoto za baba na mama,
Ni mengi tumejifunza, tukabakiza kuhama,
Na sasa twende kufyonza, tamu iliyofichama
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
5.
Mwaka ule si karibu, subira ndio mtaji,
Tele hayo majaribu, yasiyopozwa na maji,
Imara kama bawabu, makini kama hujaji,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
6.
Nyakati nayo majira, na zama zimetimia,
Mapenzi haya imara, silaha kuu ya ndoa,
hazijalishi ngawira, mapendo tumekamia,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
7.
mpira ulipoupiga, niliepa nisidake,
kwa mengi ulinikoga, japo hunayo makeke,
na sasa nimejibwaga, hirimu wangu nishike,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
8.
za mwizi hazikawii, zetu walizikamia,
pamoja nayo bidii, ya maombi kuazimia,
agizo sasa kutii, la ndoa na familia,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
9.
asante mpenzi wangu, kimasomaso menitoa,
mapendo kama uchungu, kwa machozi nimeloa,
lishike vizuri rungu, kwako nimeshajitoa,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
10.
tuijenge hiyo nyumba, yenye kujaa vicheko,
watoto nao kuumba, mbinguni tupate heko,
wala tusije kuyumba, kwani tunao upako,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
11.
udumu cha nyumba kichwa, mimi ni wako ubavu,
bidii ipite mchwa, ushinde wote uchovu,
nyuma tusije kuachwa, kwa Yesu uko wokovu
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
12.
Asante wote wapendwa, kwa maombi nazo dua,
Ni kweli hamkushindwa, shetani kumkemea,
Upendo uliopandwa, hitaji kuu la ndoa,
Mimi nawe Naimani, ni kama wingu na mbingu!
wapendwa,
pamoja na kuzidiwa na majukumu mengi kikazi, Mungu aliyajibu maombi tena vizuri sana. mchumba wangu anaitwa Naiman na ni mzaliwa wa Iringa. kama mjuanvyo masuala haya yana logistics nyingi na hivyo kukamilisha yote yaliyo ya muhimu inahitaji muda. hadi sasa mengine hayajakamilika. hapo katikati nilibahatika kupata scholarship ya kuripoti chuoni september mwaka huu na hivyo mtaona kuna kibarua cha kupangilia mambo hapo, kupata ruhusa na likizo ya masomo kazini na kuandaa harusi na wakati huohuo kutakiwa kuwa chuoni. so baada ya panga pangua, natarajia kwenda chuoni kwanza na kisha kurudi nyumbani november kwa ajili ya kufunga ndoa.
Mungu awabariki sana,
Glory to God!
Kaole orijino Shantal my dear.....................hujui??? Kha?? twende chemba basi nikupashe
Ina maana hii ni kaole au?
Hongera wetu mrembo, faraja nakutakia
Kaivae hiyo nembo , ya Mrs kwenye ndoa
Uviepuke vikumbo, na mazonge ya dunia
Pokea wangu wimbo, kheri ninakuombea
Akikuita laazizi , honey nawe itikia
Myakoleze mapenzi, msije yachakachua
Akiomba tangawizi, usije mcheleweshea
Usimtie simanzi, akachukia dunia
Tabasamu mpatie, kila akikuangalia
Atakacho mridhie, cha halali na sawia
Aibu msitirie , usiwe kiguu na njia
Vitamu umpikie, mapenzi yatazidia
Mpendane akupende, mema ninawaombea
Ndoa nje msiende , sumu ikaja ingia
Mlishane peremende, usiku ukiingia
Penzi lenu mlilinde, huu ni wangu wosia
Ndoa sio lelemama, yataka ujiandae
Sahau yalo sinema, uhalisia uvae
Jiandae na zahama, subira ndio siriye
Sikuombei kukwama, nakutaka ukomae.
Kalamu ninaiacha , wino umemalizika
Kapake rangi za kucha, umngoje muhibaka
Usije badili bucha , nyama nyengine kutaka
Nitakuja piga picha, hiyo kazi naitaka.
Hongera Miss Judith na nakutakia maisha mema ya ndoa wewe na mwenzi wako na penzi lenu lidumu daima. aaaaaaaaaaaaaaaaaaamen!
Mpwa mie waifu wangu simpeleki kwa mkongo hata siku moja! akisisitiza sana namng'olea mbali hayo makucha yake.mpwa kuna wakongo nasikia wanapaka hadi kucha...sasa Miss JF wetu sijui mmewe atampaka kucha au Wakongo watamsaidia kwa hili?
Mpwa mie waifu wangu simpeleki kwa mkongo hata siku moja! akisisitiza sana namng'olea mbali hayo makucha yake.
Mkongo anamkata mdada kucha unakuta mguu wa mdada kauweka kwenye zipu ya suruali bana! Khaaa kama miguu inapata ujauzito hawa wadada zetu wangekuwa na maguu pacha kibao kwa wakongo.mie wangu kucha akilala nazikatakata kwa sana tu...
Basi hujajua yote,wanakatwa kucha,kusuguliwa miguu.kukandwa mpaka mapajani yaani vurugu tupu na akitoka hapo anaenda kusuka kwa mmasai asiyevaa chupi na kichwa kuwekwa mapajani akiangalia mkia we acha tu urembo kazi mjini lol! Na hapo bado mpaka kucha rangi wa mtaani hahaha!Mkongo anamkata mdada kucha unakuta mguu wa mdada kauweka kwenye zipu ya suruali bana! Khaaa kama miguu inapata ujauzito hawa wadada zetu wangekuwa na maguu pacha kibao kwa wakongo.
kudadeki! hakatwi waifu kucha kwenye himaya yangu.
hehehe kamanda hapa unauwa soko la watu sasa. Hivi kuna greti thinka kweli ataruhusu waifu wake aende kwa mmasai au mkongo baada kusoma hii post yako?Basi hujajua yote,wanakatwa kucha,kusuguliwa miguu.kukandwa mpaka mapajani yaani vurugu tupu na akitoka hapo anaenda kusuka kwa mmasai asiyevaa chupi na kichwa kuwekwa mapajani akiangalia mkia we acha tu urembo kazi mjini lol!
Mi nilimpeleka shemeji yako kwa wamasai pale ilala baada ya kuona mazingira nikatoa laki asukwe na mademu we acha tu.hehehe kamanda hapa unauwa soko la watu sasa. Hivi kuna greti thinka kweli ataruhusu waifu wake aende kwa mmasai au mkongo baada kusoma hii post yako?