Wito Kwa Viongozi Wetu: Unapokosea, hata kwa kujikwaa tu ulimi, tujenge utamaduni wa kuwajibika ili kumuepushia Rais wetu kubeba mzigo wa karma

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,
Karibu, Nipashe ya leo

Kufuatia Watanzania wengi kuwa ni waumini wa dini kuu mbili, Ukristo na Uislamu, hivyo sii wengi wanaijua "karma" ni nini, kwasababu "karma" ni neno la lugha ya ki Hindi "Hindu" na linafundishwa kwenye dini ya Hinduism na Buddhism, mimi nilijifunza kuhusu "karma" wakati nikiishi jiji la New Delhi nchini India.

Huu ni wito kwa viongozi wetu, unapokosea hata kwa kujikwaa tuu ulimi, tujenge tabia ya kuwajibika kwa makosa yetu, tujitokeze kuomba radhi, na ikibidi kuwajibika!.

Kwa vile mimi ni mtu wa mastory story, na sii watu wote ni wapenda mastory, wengine ni wavivu tuu wa kusoma vitu virefu, wanapenda vitu vifupi short and clear, wengine ni just wako too busy hawana muda kusoma vitu virefu, ili kuwatendea haki nisiwachoshe wengine, hii mada nimeikata vipande vipande with sub headings, ili wewe usome only what will interest you!, kwa kusoma kile tuu utakachokuwa na interest nacho.

Tuanze kwa Kuijua Karma, ni Nini na Inafanyaje Kazi
anzia hapa

Kuijua karma "The Power of 'Karma'- Ndio Hukumu Pekee ya Haki Kamili Hapa Duniani!, Unahukumiwa kwa Matendo Yako!
Karma Kwenye Uongozi wa Umma
Njoo hapa Tuacheni ramli chonganishi: Tusihukumu tusije tukahukumiwa. Karma ndio pekee hutoa hukumu ya haki hapa duniani!
My True Story ya Kuzushiwa, Uongo, Fitna na Majungu na Karma Yake.
Karma Yangu, Karma Yao!.
Baada ya kutimuliwa kazi TVT, ndipo nikaenda shule UDSM kusomea fani nyingine kabisa ili niachane na uandishi wa habari na utangazaji!. Wale walionitenda, kila mmoja yalimkuta ya kwake, ila nikijifanyia tathmini ya life yangu ilivyo sasa na kama ningeendelea kuwa TBC, kiukweli majanga mengine ni a blessing in disguise!. Mwinyi alijiuzulu uwaziri tuu wa mambo ya ndani, akaja kuwa rais wa JMT!, hivyo kuna waliotemwa jana, Uspika au Uwaziri tuu, kumbe urais unawasubiri!. Japo kwa CCM, tayari tunaye mgombea wetu wa 2025 ila ... Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye! ila pia kuna hii sauti kuhusu 2025, Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke, japo mambo ya voices from within, sio mambo ya kuzingatia sana, ila pia sio mambo ya kupuuzia!.

Kujiuzulu Kwa Spika Kama ni Kwa Haki, Ni Uwajibikaji, Kama Ameonewa Karma Itamfidia.
Uwajibikaji Enzi za Nyerere, Mwinyi Kujiuzulu na Kisa cha Mzee Mayalla (RIP)
Huu uwajibikaji wa enzi za Mwalimu, umepotelea wapi?. Mahabusu wangapi siku hizi wanakufa mikononi mwa polisi na hakuna uchunguzi wowote wala hatua zozote zinazochukuliwa, na hakuna mtu yeyote anayewajibika?!

Msamaha wa Spika JYN Ulikuwa ni Msamaha Batili, Kajiuzulu Shingo Upande Kwa Shinikizo!
Kwenye Hotuba ya Rais, Kuna Kiongozi Ametajwa, Anasubiri Nini?
Mabadiliko ya Baraza la Mawaziri, Sio Wote Walioachwa ni Wametumbuliwa, Wengine Ni...
Rais Mama Samia Sio Malaika, Naye Ni Binaadamu, Hivyo Anaweza Kukosea, Tumsaidie!
Angalia hapa Rais Samia, sio malaika ni binadamu anaweza kukosea. Tusimlaumu, kumshutumu na kumponda kwa makosa ya kukoseshwa. Tumvumilie tumpe muda

Hitimisho
Ni lini uwajibikaji kwa viongozi wa umma utarejeshwa kwa kiwango cha uwajibikaji wa enzi za Mwalimu?. Yaani kiwango cha uadilifu wa mke wa Kaisari?. Kiongozi wa umma ni mpaka afanye kosa kubwa kiasi gani ndipo awajibike?.
Wito kwa Viongozi Wetu
Viongozi wetu, cheo ni dhamana, ikitokea ukatuhumiwa tuu, tuhuma za wazi, hata bila uthibitisho, ama kanusha ama wajibika, hata mkapishana tuu kauli na mamlaka yako ya uteuzi, ukiona tuu hamko wamoja, jikalie pembeni, usisubiri kuwekwa pembeni!, msimponze bure mama yetu Samia kwa kumtwisha mzigo wa karma zenu, kama mlivyomponza yule mwingine na karma ikafanya mambo yake!.

Ukibebwa kwa mbeleko bebeka kwa kujiachia, lakini ikitokea mbeleko iliyokubeba imelegea, sasa wewe lazima ujibebe mwenyewe, danda na kushikilia kwa nguvu zako zote ili usianguke, na ikitokea wewe umeishiwa nguvu huwezi kushikilia tena, achia mwenyewe udondoke taratibu usiumie, hiyo maana yake ni umefikia kiwango chako cha mwisho cha kubebeka hivyo sasa wewe ni zigo, lisilobebeka tena, ni busara kuachia mwenyewe usipoachia, utabwagwa chini kama zigo na utaumia!, ukiumia karma inamrudia aliyekuumiza!, hivyo kujijutia kwako na maumivu ya kubwagwa, mtatuponzea bure na huyu!, wajibikeni wenyewe msituponzee bure Mama yetu kwa mi karma yenu!.

Safari bado ni ndefu.
Jumapili njema.
Wasalaam,

Paskali.
 
Sasa karma ya nini kama uamuzi aliochukua Rais hauna tatizo?

Unapomuonea mtu kwa sababu amehoji jambo lenye maslahi kwa taifa hiyo karma kama ipo lazima ikutafune tu, au kumtumbua yeyote kwasababu ameonesha dalili za kuutaka urais kama wewe pia itakutafuna tu.

Hakuna sababu ya mtoa hoja kujiuzulu bila kosa kisa ametofautiana na mkubwa wake.
 
Na ndio hapa tunazidi kufahamu kwanini wapinzani wa kweli hapa tz wanapata tabu sana kuendesha siasa zao ni vile tu wale hawapendi mawazo mbadala
 
Kwa nchi yetu somo la UWAJIBIKAJI kwa viongozi bado halieleweki.

Sababu kubwa ni ukosefu wa Uzalendo/uadilifu.

Baadhi ya Viongozi wetu wamejawa na Uchu na tamaa ya kujinufaisha wao wenyewe.

DHAMIRA yao kuu ni kujilimbikizia mali sio kuwatumikia wananchi, ndio maana huwa inakuwa vigumu sana kwao kuwajibika/kuachia madaraka maana hufikiria kuwa atapoteza/watapoteza manufaa yake/yao sio ya wananchi.

Ndio maana ktk nchi za Afrika Uongozi/Madraka hutafutwa kwa udi na uvumba, rushwa na ikibidi hata kumwaga damu yote hayo sio kwa uchungu wa kuwatumikia Wananchi bali kujinufaisha wao!

sasa kama viongozi wanapatikana kwa njia hizo...wanawezaje kuelewa somo la uwajibikaji?!!
Bado tunasafari ndefu ya kutengeneza viongozi wazalendo/waadilifu.
 
Sikuaminigi kuwa serikali kuna uongo, uzushi, fitna na majungu, ila nilipigwa jungu, Enzi hizo TVT iko chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Kuna msamaria mwema akanitonya kuwa kule wizarani kuna barua yenye tuhuma nzito kunihusu inazunguka, hivyo nitang'olewa. Sikufanya chochote kwasababu mimi siamini zengwe, majungu wala fitna.

Kweli siku ya siku, tena mimi ndio nimapangwa kusoma habari siku hiyo, nikiwa kwenye kikao cha idara, mara nikaitwa kutoka nje ya kikao, ndio nikakutana na mesenja wa Confidencial Registry na briefcase nyeusi, ameandamana na FFU wawili, wameshika bunduki standby as if mimi ni terrorist, huyo jamaa anaitwa jina la utani la Isirael, ndio huwa anasambaza barua za watu kupunguzwa kazini. Basi nikapewa barua yangu, na kusaini despatch kuwa nimepokea, kuifungua, niliishiwa nguvu!, nimepigwa "summary dismissal kwa kosa la insubordination!".

Yule Siraeli akarudi nyuma FFU na mimitu yao huku wamenielekezea, ingia ndani kusanya kilicho chako, tunakusindikiza mpaka getini. Kiukweli niliishiwa nguvu, kumbuka ofisini kwangu ndio kuna kika na niko na watumishi
 
We jamaa bhana...

Yaani Mwigulu Nchemba anaingia bungeni na mkoba kwa ajili ya kusoma bajeti huku Ndugai na wenzake wakimpigia shangwe kama lote!!

Nchemba anaeleza mambo kadhaa, na kwa muktadha huu ana-highlight vyanzo mbalimbali vya mapato kwa ajili ya kugharamia bajeti husika!!

Wakati akiendelea kusoma, hatimae anafikia hapa:-

Hapo sijataja mikopo ya kibiashara!! Mwisho wa hotuba, Mwigulu anatoa hoja na kuliomba bunge lipitishe bajeti hiyo!!

Baada ya hapo, majadiliano fake yanaanza, and finally, Ndugai anawauliza wenzake: "Wanaosema Ndiyo?"

Wabunge: "NDIYOOOOOOOOOOOOOOO"

Kisha Ndugai anatoa kila kicheko chake halafu tena anauliza "Wanaosema siyo?"

Wabunge wawili watatu wanajibu "siyo"!

Ndugai tena, kwa mbwembwe, tambo na majivuno anasema "Waliosema NDIYO wameshinda"!

Na kama kungekuwa na wapinzani, anaanza kuwakejeli huku akisifia "bajeti bora kuliko zote kuwahi kutokea!!"

Unajua tafsiri ya hiyo "NDIYOOOOOOOOOO"

Manake ni kwamba Ndugai na wenzake, pamoja na mambo mengine pia wanamruhusu Samia na timu yake akiwemo Mwigulu Nchemba, wakakope!!

Miezi michache baadae, Ndugai yule yule anatoka tena hadharani na kukejeli kile kile ambacho taasisi anayoiongoza iliidhinisha tena kwa shangwe kubwa, halafu unasema "ameonewa"?

Hivi unajua maana ya collective responsibility?
 
Pole sana Mkuu Paskali.
huwa nasoma hicho kisa chako cha kufukuzwa kazini kwa ajili ya Majungu na fitina naumia sana.

kwani tabia hizo hadi leo hii bado zipo sana, kuna watumishi makini na waadilifu wanaumizwa na fitina na majungu na hawana wa kuwatetea.

kisa chako kinafaa kiwe somo na fundisho.
viongozi mlio pewa madaraka tendeni Haki kwa walio chini yenu vinginevyo tegemeeni kuangamizwa na nguvu ya Mungu.
 
Kuna wanaosema Ndugai katumia njia sahihi sababu Bunge bado halijaanza...

Kuna wewe unayesena kakosea kui address chamani, angei address bungeni...

Au angesubiri mpaka Bunge lianze ndiyo ajiuzuru....

Which is which?
 
Tujikumbushe kidogo wakati impunity ilipokuwa inaishi na kutawala Tanzania😁😁😁
Your browser is not able to display this video.
 
Kuna wanaosema Ndugai katumia njia sahihi sababu Bunge bado halijaanza...

Kuna wewe unayesena kakosea kui address chamani, angei address bungeni...

Au angesubiri mpaka Bunge lianze ndiyo ajiuzuru....

Which is which?
Anyway ila kwa Ndugai hata kama amelazimishwa kujiuuzulu, hata kama taratibu hazikufuatwa kikatiba, tuunge mkono tu kilichotokea kwa kuwa UFEDHULI aliofanya una madhara kuliko hizo taratibu za kumtoa. The end justifies the means
 
Pole sana bro kisa cha Baba yako I hope kimekujenga kwenye ustahimilivu kimaisha. Siku hizi kika kitu ni fake kwanzia nafsi ya Rais hadi sisi mmoja mmoja na pia pengine kiwango cha udikteta na umwinyi kimepungua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…