Wito Maalum:Taifa Stars Kushinda 'bila chuji, boban na kaseja' Inawezekana

Wito Maalum:Taifa Stars Kushinda 'bila chuji, boban na kaseja' Inawezekana

Teamo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2009
Posts
12,271
Reaction score
1,052
Nasikitishwa sana na watanzania wenzangu walio 'wenye mapenzi binafsi' na wasakata kandanda wanaoripotiwa kukosa nidhamu na kujiananisha na 'professional players' wa kiwango cha akina iniesta au kina peter czech wakati hawana lolote.

Watanzania(ambao engine ni makocha pia) wamekuwa na mchango mkubwa katika kuumaliza uwezo wa kisoka wa hawa wachezaji wakubwa waliojihakikishia namba katika timu ya taifa.

Kama jana taifa starz wangefungwa tungeyasikia mengi sana mitaani 'mara chuji hayupo',mara 'pengo la boban',mara 'pengo la kaseja',lakin sasa hiv naona.......................

Ninachokifahamu mimi ni kwamba:

-mchezaji ni pamoja na nidhamu
-sio kweli kwamba tanzania hamna viungo azuri zaidi ya chuji,na boban
-sio kweli kwamba tanzania haina kipa mzuri zaidi ya kaseja

HOFU YANGU:labda tumeamua kuzeeka na wachezaji wetu 'vipenzi'

KILIO CHANGU:watanzania naomba tuamke!tuwe wakweli,tuwe wawazi,TUACHE USHABIKI:tanzania inaweza kushinda bila achezaji wetu vipenzi.

TUTAFIKA TU!hongera kazimoto,hongera TEGETE,hongera maximo!tupo pamoja
 
ila hatuna mbinu....team inacheza tuuu haina mbinu....wale nao walikuwa kama wamechoshwa na hali hewa.....hawajaizoea hata.....ila sio kweli timu yetu nzuri kiasi kile......
 
ila hatuna mbinu....team inacheza tuuu haina mbinu....wale nao walikuwa kama wamechoshwa na hali hewa.....hawajaizoea hata.....ila sio kweli timu yetu nzuri kiasi kile......

hujiamini tu skills!TUNAWEZA SISI.am telling you.

rome yenyewe HAIKUJENGWA KWA SIKU MOJA
 
Tumekatazwa kutumia lugha chonganishi ila kwa mtu mwenye ufahamu mzuri uliyekulia katika familia ambazo fitna na uzandiki ni dhambi utakubali soka letu liko chini na bila mikakati madhubuti ya kiufundi hatutafika kokote zaidi ya kutiana moyo soka letu limepanda. Jana hiyo mechi tumecheza ndani 14 maana Mbaga alikua sijui kala ndumu au ndio mambo yetu yale ya ukayuni, goli la kusawazisha sio goal ni offside dhahiri na yeye analijua hilo ila mambo ya ujinga wa kusaidiana ndio likastay, goal la pili zuri sina tatizo nalo. Tatizo langu ni kwa viongozi wa TFF na Waamuzi ni ovyo sana naanza kuwa na wasiwasi na Bwn Tenga sijui ni uzee au ndivyo alivyo maana hukuna chochote cha maana zaidi ya politics. Hatujiulizi why waamuzi wetu hawachezeshi mechi za maana zaidi ya za kirafiki na makombe yetu ya bia na mbuzi? utombo wanaoufanya unajulikana that is true, shame on you Mbaga na Kayuni plus all TFF. Wachezaji sio lazima tunaowapenda ila waonyeshe mpira wa kufundishwa sio pasi mbili ,kubutua na kudrible wenyewe wanaita kukimbiza. Walijitahidi lakini kiwango baado tutaundelea kukaa huko huko number 100 plus on FIFA rankings. Maximo mhh hamna kitu, akagombee ubunge tu Ilala au Kinondoni maana keshakua mwanasiasa tu .
 
Kwa jinsi nilivyo fuatilia mtanange ule pengo la Nsajigwa,Chuji,Boban wakuu tuwe wa wazi lilionekana dhahili.
 
Mi nafikiri tatizo letu( watanzania washabiki wa soka) kubwa ni kukosa subira.Tunataka mambo makubwa bila kuyatolea jasho (tazama DECI). Hivi wale vijana waliocheza jana tulitaka wafanye nini zaidi ya kufunga yale magoli mawili? Ni mafanikio makubwa sana kwao kuwafunga mabingwa wa bara la Oceania, tusitafute visingizio vya hali ya hewa n.k, tungefungwa sisi hakuna mtu amabaye angetaka kusikia visingizio vya timu haina uzoefu n.k
Hitimisho:
1. Ushindi amabao timu yetu imekuwa inaupata chini ya Maximo,hauondoi ukweli kuwa bado tuko safarini kuelekea mafanikio endelevu ya kisoka.
2. Tujiamini kuwa tunaweza, tuwape muda wachezaji, makocha n'k kuendelea kunoa wachezaji.
3. Watakaokuja kuiletea sifa nchi yetu ni vijana (under 17) wanaolelewa vizuri katika mafunzo ya soka ya kisasa, tuweke kipaumbele huko.
4. Vilabu ndio kisima cha kutoa wachezaji bora kwa timu ya taifa. Ziwekeze katika timu za vijana na kuajiri makocha bora.
 
goli la kusawazisha sio goal ni offside dhahiri na yeye analijua hilo ila mambo ya ujinga wa kusaidiana ndio likastay, ..

HAPA SIKUBALI MKUU!wewe wasema

Tatizo langu ni kwa viongozi wa TFF na Waamuzi ni ovyo sana

naanza kuwa na wasiwasi na Bwn Tenga sijui ni uzee au ndivyo alivyo maana hukuna chochote cha maana zaidi ya politics.

, shame on you Mbaga na Kayuni plus all TFF. Wachezaji sio lazima tunaowapenda ila waonyeshe mpira wa kufundishwa sio pasi mbili ,kubutua na kudrible wenyewe wanaita kukimbiza.

Walijitahidi lakini kiwango baado tutaundelea kukaa huko huko number 100 plus on FIFA rankings.

Maximo mhh hamna kitu, akagombee ubunge tu Ilala au Kinondoni maana keshakua mwanasiasa tu .

haya nakubali kaka!lakini TUNAWEZA KUCHEZA BILA CHUJI,BOBAN,KASEJA?
 
Kwa jinsi nilivyo fuatilia mtanange ule pengo la Nsajigwa,Chuji,Boban wakuu tuwe wa wazi lilionekana dhahili.

ni mawazo tu!uweli kutoka moyoni NAPINGANA NA WEWE KWA HILI
 
Mi nafikiri tatizo letu( watanzania washabiki wa soka) kubwa ni kukosa subira.Tunataka mambo makubwa bila kuyatolea jasho (tazama DECI). Hivi wale vijana waliocheza jana tulitaka wafanye nini zaidi ya kufunga yale magoli mawili? Ni mafanikio makubwa sana kwao kuwafunga mabingwa wa bara la Oceania, tusitafute visingizio vya hali ya hewa n.k, tungefungwa sisi hakuna mtu amabaye angetaka kusikia visingizio vya timu haina uzoefu n.k
Hitimisho:
1. Ushindi amabao timu yetu imekuwa inaupata chini ya Maximo,hauondoi ukweli kuwa bado tuko safarini kuelekea mafanikio endelevu ya kisoka.
2. Tujiamini kuwa tunaweza, tuwape muda wachezaji, makocha n'k kuendelea kunoa wachezaji.
3. Watakaokuja kuiletea sifa nchi yetu ni vijana (under 17) wanaolelewa vizuri katika mafunzo ya soka ya kisasa, tuweke kipaumbele huko.
4. Vilabu ndio kisima cha kutoa wachezaji bora kwa timu ya taifa. Ziwekeze katika timu za vijana na kuajiri makocha bora.

NAUNGA MKONO HOJA BABA!
thank u!
 
Nasikitishwa sana na watanzania wenzangu walio 'wenye mapenzi binafsi' na wasakata kandanda wanaoripotiwa kukosa nidhamu na kujiananisha na 'professional players' wa kiwango cha akina iniesta au kina peter czech wakati hawana lolote.

Watanzania(ambao engine ni makocha pia) wamekuwa na mchango mkubwa katika kuumaliza uwezo wa kisoka wa hawa wachezaji wakubwa waliojihakikishia namba katika timu ya taifa.

Kama jana taifa starz wangefungwa tungeyasikia mengi sana mitaani 'mara chuji hayupo',mara 'pengo la boban',mara 'pengo la kaseja',lakin sasa hiv naona.......................

Ninachokifahamu mimi ni kwamba:

-mchezaji ni pamoja na nidhamu
-sio kweli kwamba tanzania hamna viungo azuri zaidi ya chuji,na boban
-sio kweli kwamba tanzania haina kipa mzuri zaidi ya kaseja

HOFU YANGU:labda tumeamua kuzeeka na wachezaji wetu 'vipenzi'

KILIO CHANGU:watanzania naomba tuamke!tuwe wakweli,tuwe wawazi,TUACHE USHABIKI:tanzania inaweza kushinda bila achezaji wetu vipenzi.

TUTAFIKA TU!hongera kazimoto,hongera TEGETE,hongera maximo!tupo pamoja

Ni bahati mbaya/nzuri sana soka ni mchezo ambao kila shabiki anaamini mawazo yake ndo sahihi, sishangai timu inaposhinda shabiki kushangalia au inaposhindwa shabiki kuzomea. Hili suala la Kaseja, Chuji na Boban bado ni kitendawili, hakuna anayejua utovu wa nidhamu ulioonyeshwa na hao wachezaji hadi leo, kilichopo ni hisia tu kwamba walifanya hivi au walifanya vile. Ni vizuri pia tukafahamu nidhamu ya soka sio kumpa mwalimu shikamoo na mambo mengine kama hayo, nidhamu ya soka ni pamoja na kufuata maelekezo ya mwalimu hata kama maelekezo hayo hayaleti faida kwenye timu (tunakumbuka CL final Man U vs Barca) pamoja na kuwa formation ya Man haikuwa fruitful yet kwa nidhamu ya wachezaji walicheza vile vile kama walivyoelekezwa na mwalimu. Tukirudi kwa hao wahanga wa Maximo, ni bahati nzuri kwamba mpira unachezwa hadharani kila mtu anaona, kwa sasa tunavyozungumza hakuna kipa kama Kaseja Tanzania hiyo ipo wazi, tumeona makosa ya kijinga yanayofanywa na Dihile, sifa ya kipa sio kudaka ni kuokoa hatari zinazoelekezwa langoni. Dihile hana timing hata kidogo, he is still a raw, ni hivi majuzi mwalimu wa kipa wa timu ya taifa alilalamika kuhusu uwezo wa makipa wake. Kuhusu Chuji na Boban wapo watu wanaoweza kuziba mapengo yao ingawa itachukua muda kuwasahau. Nimalizie kwa kusema kocha ni kama mzazi, na mzazi mzuri humfunza mwane adabu na wala sio kushindana nae na kumsusa.
 
....kwa sasa tunavyozungumza hakuna kipa kama Kaseja Tanzania hiyo ipo wazi....

katika hili hapana baba angu!kaseja anafungwa magoli YA KAWAIDA SANA
 
Huyo Chuji, Kaseja na Boban hawana msaada kama hawawezi kuingia ndani yamfumo wa timu yetu. wapo watu ambao wanawadanganya kuwa wao ni wachezaji wakubwa. kwa mtazamo wangu naona kuna vijana wengi sana, wadogo, wenye vipaji na moyo wa kucheza mpira wa kisasa na mafanikio sio hao vibaraka wa timu zenu za hapa mjini (-a--a na -i--a). tunataka watoto wasiishie kucheza ligi ya Vodacom na Taifa cup tu wawaze kwenda mbele zaidi.

Milango inafunguka sasa. hao Kaseja, chuji na boban wamekuwapo hapo walipo kwa muda gani hawataki kwenda Profession? je wana nafasi gani ktk Taifa stars? wengine walipangwa kule Ivory Coast hata kipindi kimoja kiliwashinda.

Hongera Taifa Star, Hongera Maximo, hongera wachezaji wote. ongezeni bidii ili muuzike ulaya.
 
nakubaliana na mtoa hoja kuwa tunaweza kucheza bila chuji na boban, lakini kwa jinsi tulivyo cheza jana pengo lao limeonekana dhahiri. Kucheza kwa kiwango cha jana kama ndio lengo letu basi tutaendelea kushinda tu friendly huku tukiburuzwa kwenye mashindano.
 
.wapo watu ambao wanawadanganya kuwa wao ni wachezaji wakubwa. .

watu wenyewe ni:
1-jamhuri kihwelo 'julio,arbelto perreira'

2-sleslaid mziray 'super-coach'

3-zamoyoni mogella 'golden boy'

4-kondic dussan 'kocha wa chuji'

5-patrick phiri 'kocha wa boban'

6-mashabiki 'wanazi' wa simba na yanga

ANGALIZO:TUNAJUA KILAKITU MNACHOFANYA,na tumewashuhudia mkiwachukua wachezaji maarufu mkienda kuwapiga bia na kuwapa moyo kwa 'blah blah'.HAKIKA MWISHO WENU WAJA.na ninyi ndio wapandikizaji wakubwa wa chuki kwa wapenzi wa soka tanzania.


.Milango inafunguka sasa. hao Kaseja, chuji na boban wamekuwapo hapo walipo kwa muda gani hawataki kwenda Profession? je wana nafasi gani ktk Taifa stars? wengine walipangwa kule Ivory Coast hata kipindi kimoja kiliwashinda.

Hongera Taifa Star, Hongera Maximo, hongera wachezaji wote. ongezeni bidii ili muuzike ulaya.

MKUU KUNA HUYU BOBAN,alileta kinyaa wakati simba ilipocheza na vancouver,alibanwa na misuli muda wote,mara atoke,mara aingie.ALIKERA SANA1lakini huwez amini ndio kipenzi cha mashabiki.

MILANGO INAFUNGUKA!hakika maximo umefanya kazi
 
Mtakubaliana nami kuwa bado timu yetu ya Taifa haina golikipa ambaye ataitwa TANZANIA ONE, timu yeyote ya taifa lazima iwe na golikipa tegemezi kwa nchi na lazima kuwe na golkipa watatu ambao wanaaminika kuwa hata numba moja akikosekana basi namba 2 yupo.

1.Niambieni wadau wa soka nchi yetu ya Tanzania yenye mikoa 27 bara na mikowa mingine visiwani tuna kosa kabisa magolikipa wazuri kwa maslai ya taifa.
2. Bado hatuna safu ya washambuliaji kweli timu zote z mpira nchini kwetu tunakosa washambuliaji wazuri.
3. najua kuwa Maximo kwli amejitaidi kututoa mbali but hii ya kubadilisha wachezaji ovyo nayo inachangia kutokukomaa kw kikosi cha taifa, nielewavyo mie kikosi cha taifa kinagawanyika mara 2 nikimaanisha stars A & B na mara nyingi wachezaji wa timu ya taifa huwa wanadumu kwa muda na wanachukuliwa wakiwa bado wachanga hadi wanakomaa ktk timu ya taifa.
4. mashabiki najua wanapenda kumlaumu kocha pale timu inapofanya vibaya, hebu tujiulize kama tungekuwa na timu nyingi za vijana na tukatengeneza programs za miaka miwili hii ni kufundisha tu timu kwa dhamira na vitendo tungefika mbali sana na siajabu tungeweza shiriki kombe hili linalokuja la dunia.

Upande wa TFF, jamani nawaomba mumuwachie kocha wa timu ya taifa afanye kazi yake kwa ufasaha bila kumuingilia,kocha w taifa anatakiwa apewe nafasi ya kuzunguka mikoa yote hata timu za michangani ktafut wachezaji,timu ya taifa haijegwi kwa timu mbili kubwa simba na yanga,kuna timu nzuri sana za mchangan watu wncheza vizuri kabisa kuliko hao wachezaji wa simb na yanga na asganti na nyinginezo.
Tuwache ushabiki wa 10% ktk soka tunapo chagua wachezaji tusinganganie kweka wachezaji wa timu kubwa tu za simba na yanga,mtibwa na nyinginezo. tuchague timu ke kuweka wachezaji wanao stahili kuwapo ktk kikosi cha kwanza na chapili kwa muda,
hebu tuwaangalie nchi za wenzetu watu wanacheza ktk kikosi cha taifa hadi wanastaafu, siye tangu tumeanza kuwa na hii timu ya taifa niwachezaji wngapi washabadilisha??
 
watu wenyewe ni:
1-jamhuri kihwelo 'julio,arbelto perreira'

2-sleslaid mziray 'super-coach'

3-zamoyoni mogella 'golden boy'

4-kondic dussan 'kocha wa chuji'

5-patrick phiri 'kocha wa boban'

6-mashabiki 'wanazi' wa simba na yanga

ANGALIZO:TUNAJUA KILAKITU MNACHOFANYA,na tumewashuhudia mkiwachukua wachezaji maarufu mkienda kuwapiga bia na kuwapa moyo kwa 'blah blah'.HAKIKA MWISHO WENU WAJA.na ninyi ndio wapandikizaji wakubwa wa chuki kwa wapenzi wa soka tanzania.
Umesahau pamoja na kuwapiga mizinga wachezaji ktk posho zao
 
borntown,
UKWELI NASHUKURU SANA KWA MAWAZO YAKO!naamini wadau wa soka anasoma mawazo yako mazuri na watayafanyia kazi
 
katika hili hapana baba angu!kaseja anafungwa magoli YA KAWAIDA SANA
Suala hapa sio kufungwa, hata Gordon Banks alikuwa anafungwa, suala la hapa ni yupi bora kati ya makipa tulio nao.
 
magehema babaangu!nipe criterias za 'kipa bora' mimi naanza hapa:

1-NIDHAMU

2-KUPATA NAFASI KATIKA FIRST TEAM YA TIMU YAKO YA KLABU

3-KUPATA NAFASI KATIKA TIMU YA TAIFA-FIRST TEAM

4-MCHANGO WAKO BINAFSI KATIKA TIMU

5-

6-

7-

8-

twende kazi baba!
 
Milango inafunguka sasa. hao Kaseja, chuji na boban wamekuwapo hapo walipo kwa muda gani hawataki kwenda Profession? je wana nafasi gani ktk Taifa stars? wengine walipangwa kule Ivory Coast hata kipindi kimoja kiliwashinda.

Hongera Taifa Star, Hongera Maximo, hongera wachezaji wote. ongezeni bidii ili muuzike ulaya.

Mpingo unachanganya class na form, form ya mchezaji inabadilika kutokana na mambo mengi sana ila class ya mchezaji ipo pale pale. Unapotoa mfano wa mchezaji kushindwa kucheza mchezo mmoja unazungumzia form na sio class ya mchezaji. Kama ni mfutiliaji mzuri wa soka nitakukumbusha mechi moja tu kukuonyesha tofauti ya form na class, hiyo ilikuwa ni final ya WC kati ya Brazil na Italy 94, wing defender (Jogihno) ambaye tangu mechi ya kwanza alikuwa ni 1st eleven alicheza kwa dakika 20 tu katika ile fainali akatolewa akaingia Cafu, pale suala halikwa kiwango bali form yake siku ile ilikuwa low, kwa hiyo suala la Haruna kutolewa 1st half kule Ivory Coast sio sababu kwamba kiwango chake ni kidogo.
 
Back
Top Bottom