Wito Maalum:Taifa Stars Kushinda 'bila chuji, boban na kaseja' Inawezekana

Wito Maalum:Taifa Stars Kushinda 'bila chuji, boban na kaseja' Inawezekana

Mi nafikiri tatizo letu( watanzania washabiki wa soka) kubwa ni kukosa subira.Tunataka mambo makubwa bila kuyatolea jasho (tazama DECI). Hivi wale vijana waliocheza jana tulitaka wafanye nini zaidi ya kufunga yale magoli mawili? Ni mafanikio makubwa sana kwao kuwafunga mabingwa wa bara la Oceania, tusitafute visingizio vya hali ya hewa n.k, tungefungwa sisi hakuna mtu amabaye angetaka kusikia visingizio vya timu haina uzoefu n.k
Hitimisho:
1. Ushindi amabao timu yetu imekuwa inaupata chini ya Maximo,hauondoi ukweli kuwa bado tuko safarini kuelekea mafanikio endelevu ya kisoka.
2. Tujiamini kuwa tunaweza, tuwape muda wachezaji, makocha n'k kuendelea kunoa wachezaji.
3. Watakaokuja kuiletea sifa nchi yetu ni vijana (under 17) wanaolelewa vizuri katika mafunzo ya soka ya kisasa, tuweke kipaumbele huko.
4. Vilabu ndio kisima cha kutoa wachezaji bora kwa timu ya taifa. Ziwekeze katika timu za vijana na kuajiri makocha bora.
Tusijipe moyo kwa kufumbia macho MATATIZO ya msingi ya soka letu:

1.Football Administration yetu ina matatizo megi na YAKUJITAKIA.Kuna WATU PALE TFF wamefanya TFF ni mali yao.Alizungumza Mogella kuhusiana na aina ya Viongozi waliopo pale kwa misingi ya kwamba wao wanaelimu.Elimu ni muhimu lakini unatakiwa upate na ukaribishe mawazo ya watu kama Mogella waliocheza mpira WAKAWEKA alama mpaka leo vizazi vinawakumbuka.Kayuni na wenzake wanaharibu kitengo kile cha Ufindi.

2.Uwezo wa wachezaji wetu TUNAOWAONA PALE uwanjani ni mdogo mno.Wachezaji TUNAOLETEWA timu ya taifa siyo BEST PLAYERS(tofautisha majina na uwezo) wengi wanaMAKUBALIANO MAALUMU na viongozi wa kitengo cha Ufundi TFF.

3.U-17 imemkimbiza TINOCCO ,mfano pale karume Tinocco alichagua wachezaji kwa kuwatambua kwa namba za jezi zao, siku ya kambi aliletewa vijana tofauti na kamati ya ufundi ya TFF,bahati nzuri alishtuka akauliza baadhi yao ambao walikuwa na features tofauti na wenzao, akajua ameingizwa mjini.Vilevile tusisahau kuwa muda wote alikuwa akitumiwa na Maximo timu ya taifa kama assistant wake baada ya Itamar kuondoka,sisi wengine hatukushangaa alipoondokea kulekule Abdijan.

4.Maximo amepewa mkataba mpya wa kufundisha,lakini bado anahangaika na kujenga kikosi UKITAKA KUJUA UWEZO WA MAXIMO nenda kazungumze na ITAMAR pale Azam ndipo utakapojua kuwa WaZT tumeingia mkenge,juzi Mtemi Ramadhani kaonyesha concern yake pia kwa suala ya kufumua kikosi mara kwa mara.Kimsingi tunahitaji KOCHA MPYA badala ya Maximo huwezi kuwa mtu usiye na MSAMAHA,hakuna ASIYEJUA UWEZO WA BOBAN ,he is the best midfielder kwa sasa nchini kwetu,GAGARINO alikuwa mtovu wa nidhamu lakini mwisho wa siku tulikuwa tunampima kwa results.

5.Administration ya Vilabu ni UTAPELI MTUPU.Nini amefanya MANJI/MADEGA pale jangwani? HAKUNA, jengo lilelile la mwaka 47 vilevile kwa watani wao Simba hakuna maendeleo,kina MAGORI na wenzake FRIENDS OF SIMBA hakuna kitu ambacho wanaweza kuonyesha wakajivunia wamefanya ambacho ni life yake ni zaidi ya miaka 10 or 20 ijayo.TUNASHAWISHIKA KUSEMA WOTE HAO SIO WAFADHILI WA HIVI VILABU bali WANAVITUMIA KUFANIKISHA MALENGO YAO.Hapa tunaona kumbe hata wazee wale wazamani wanaonekana walikuwa na Vision nzuri kuliko wa sasa,ZIPO WAPI SIMBA B na YANGA B, kule kulitoa wachezaji wazuri,Michezo mashuleni hoi,VIWANJA VYA MICHEZO VINAUZWA KWA WAWEKEZAJI.

6.Chama cha Waamuzi kiache kuendeshwa kiubabaishaji,ndiyo maana hatuna hata mwamuzi mmoja anayechezesha hata mashindano makubwa ya Afrika.Tangu waondoke kina Hafidh Ally imekuwa aibu tupu.Jana goli la kwanza lilikuwa offside ya wazi Mwamuzi alitubeba ni fedheha.

6.Tushangilie ushindi lakini TUACHE UNAZI,tunashabikia hata kile kisichofaa.
 
Uwezo wa wachezaji wetu TUNAOWAONA PALE uwanjani ni mdogo mno.Wachezaji TUNAOLETEWA timu ya taifa siyo BEST PLAYERS(tofautisha majina na uwezo) wengi wanaMAKUBALIANO MAALUMU na viongozi wa kitengo cha Ufundi TFF..


Wayne Rooney,
JUSTIFY THE ABOVE STATEMENT!
 
Wayne:
Umenena ukweli mtupu hata hao mawaziri wa michezo ni wizi mtupu hakuna wanalolifanya kazi kujikomba kwa wadhamini wapewe bia za bure. Sijaona kitu hata kimoja walichokifanya. Yaani kuanzia chama mpira, vilabu,waamuzi yaani hakuna kitu.
 
magehema babaangu!nipe criterias za 'kipa bora' mimi naanza hapa:

1-NIDHAMU

2-KUPATA NAFASI KATIKA FIRST TEAM YA TIMU YAKO YA KLABU

3-KUPATA NAFASI KATIKA TIMU YA TAIFA-FIRST TEAM

4-MCHANGO WAKO BINAFSI KATIKA TIMU

twende kazi baba!

Nidhamu ni sawa, ila sio ile tafsiri wa wengi ya nidhamu ni shikamoo na kuongea huku unanyenyekea umeweka mikono nyuma.

5. Kipa lazima awe na maamuzi sahihi (good judgement) muda gani atoke golini, muda gani asitoke
6. Kipa lazima awe mwepesi (agility), awe ananyumbulika
7. Kipa bora lazima awe na uwezo wa hali ya juu ya kujipanga (positioning) 8. Kipa bora lazima awe na akili ya kutambua mawazo/malengo ya mhambuliaji (bravery)
 
Tanzania hadi tuje kuinuka ki-michezo tuwe na wachezaji wengi wa kimataifa wakulipwa,viongozi walio makini na michezo labda 2030
 
ila hatuna mbinu....team inacheza tuuu haina mbinu....wale nao walikuwa kama wamechoshwa na hali hewa.....hawajaizoea hata.....ila sio kweli timu yetu nzuri kiasi kile......

tukishinda tunasema hawajazoea hali ya hewa, tukishindwa maximo hamna kitu. lakini ukweli ni kwamba tume improve sana. Nafurahia mtindo wa Maximo wa kuendelea kusaka vipaji. tatizo letu kubwa si maximo ni mifumo yetu ya usimamizi wa mpira kuwa mibovu. mbona timu zetu ni mbovu sana hazina historia ya kushinda mpaka kufikia kuchukua makombe ya africa? zinatolewa mapema sana. sasa Maximo badala ya kuunganisha wachezaji wazuri katika taifa stars, anaanza upya.
mtashangaa hata akiletwa kocha gani mzuri(uwezo wa kulipa upo?) anashindwa kama hali ya vilabu haitatengamaa
 
Wayne Rooney,
JUSTIFY THE ABOVE STATEMENT!
Mkulu
KUCHEZA TIMU YA TAIFA SASA HIVI NI DEAL.Iwe ya Wakubwa au ya U-17

1.Hao jamaa wa Ufundi wanapeleka watoto wao na wadogo zao, wakifahamu kuwa hapo ndipo pakutokea kimaisha.

2.Wanakubaliana na wachezaji kuwa, anapendekeza majina yao kwa Maximo na kila mapato yatakayopatikana, a certain percentage yanarudi kwake.Kama kuna watu Maximo anawasikiliza na kuwaamini basi ni Kayuni.

Nakushauri jaribu kufuatilia au kuwa karibu na watu wa TFF na Timu ya Taifa ikiwa pamoja na wachezaji wenyewe, ndipo utagundua kuna TATIZO KUBWA SANA.

Kama kuna ADUI wetu mkubwa anayeturudisha nyuma katika soka ni huyu Mkurugenzi wa hiki kitengo cha ufundi.
 
too far bwana!


Mpira sio majina kaka, ni kujituma tu. Akina Mwinyi KAzimoto ni majina ya kawaida sana, lakini yamefanya vizuri sana Jumatano iliyopita. Mpira ni mazoezi na kujituma, na wala si majina makubwa...
 
WITO MAALUMU:TAIFA STARZ KUSHINDA 'bila chuji,boban na kaseja' INAWEZEKANA! Kabisa na sio hao tu hata bila Kayuni, Madadi, Mbaga na Maximo inawezekana kushinda tu maana hawa jamaa hamna kitu. Tunahitaji watu walio commited na wasio mafisadi. Mimi siwezi kushangilia ushindi wa kifisadi maana goli la kusawazisha ni SHAME kwa Tanzania Football, Tegete alikua offside na on top of that aliupiga ngumi mpira na linesman or woman sijui alikua nani aliona wazi wazi. Jana Channel 10 walionyesha hilo SHAMEFUL goal kwenye taarifa ya habari.
 
N-handsome UMENENA
 
Hakika maximo umefanya kazi
Wapi kazi gani kafanya muda wote huo hana first eleven pamoja na kupewa support na watanzania wachezaji wanapata kila kitu wanalala pazuri usafiri mzuri kitu ambacho hakikuwahi kutokea hapo kabla bado anatuambia tuwe na subira..amekalia visasi na wachezaji kama ni nizamu kwa wachezaji yeye ndiyo mwalimu si awarekebishe na siyo kuweka vinyongo nao akumbuke yeye ni kama mzazi mbona akina Diof walikuwa watovu wanizamu lkn leo hii wamebadilika. Maximo tuna mshukuru kwa kutuunganisha wana-Simba na Wana-Yeboyebo kurudisha mapenzi kwenye timu ya Taifa maana hapo kabla ilikuwa akipata mpira mchezaji wa simba wana simba ndiyo watakao mshangilia wakati wapenzi wa yanga wata mzomea leo hii angalau tumejua tofauti ya (Simba, Yanga...) na Taifa Star...
 
ila hatuna mbinu....team inacheza tuuu haina mbinu....wale nao walikuwa kama wamechoshwa na hali hewa.....hawajaizoea hata.....ila sio kweli timu yetu nzuri kiasi kile......
Yawezekana kweli. Tujipange kukabiliana na challenges zilizopo. Moja kubwa ni kusupport anayoyafanya kocha. Naunga mkono hoja ya timu yenye nidhamu na exposure ya kutosha. Majina makubwa yenye kunata bila mpango tuyaache simba na yanga hukohuko
 
Nipo nje ya mada japo kidogo, hivi kwa sasa Tz ni ya ngapi katika football ranking wolrdwide ?
 
Nipo nje ya mada japo kidogo, hivi kwa sasa Tz ni ya ngapi katika football ranking wolrdwide ?
Tanzania ni ya 109 kati ya 202 hiyo ni standing ya as of 05 June 2009
 
Nipo nje ya mada japo kidogo, hivi kwa sasa Tz ni ya ngapi katika football ranking wolrdwide ?

NI rahisi sana kucheza na akili za watz, sasa hivi wanataka kujua TZ ni ya ngapi katika rank za FIFA wakati jirani zetu wa Kenya na Rwanda wapo kwenye mchakato wa kushiriki AFCON NA WC. Safi sana Maximo!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom