WITO Mhesh Ruto jahazi lazama, chutama, usione fedhea , fanya hima mtafute mheshimiwa Uhuru, kumbuka jungu kuu halikosi ukoko!

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2020
Posts
3,585
Reaction score
8,106
Wadau hamjamboni nyote?

Huu ni wito wangu binafsi kwa Mheshimiwa William Ruto Rais wa Jamhuri ya Kenya ambao umezingatia maslahi mapana ya nchi hiyo!

Mheshimiwa

Nikuombe Ndugu yangu usione aibu wala fedhea, chutama, zika ufahari wako, usisite, usijali, usiogope, usione aibu wala fedhea , wewe nenda tu mtafute Mheshimiwa Uhuru naamini yapo mengi utajifunza kwake

Nikuombe usahau yalopita hayana nafasi muda huu chamsingi ukiwa wewe ndiye nahodha tambua chombo kinazama baharini hivyo ni muhimu kuokosa jahazi kwa njia zozote!

Nirudie kukuomba umuone uhuru jungu kuu kamwe halikosi ukoko!

Niwatakie usiku mwema Ndugu zetu wakenya

Niwatakie usiku mwema Ndugu zetu Watanzania na Afrika Mashariki
 
Jukwaa limejaa habari za Kenya pekee, Vipi nyie mko sawa sawa? au ni kwa sababu Taifa limejaaa Mazezeta? Unamshauri Ruto vipi Mama yenu? au yuko sawa kwa sababu Nchi imejaaa wapumba kama weww hapo?

Hamna matatizo ya Kodi Tanzania? Tuna ajira za kutosha kabisa? Hakuna ufisadi? Hakuna matumizi ya anasa ya Pesa za Umma?
Unaweza zania sisi ni Ulaya kumbe tuna matatizo kuliko Wakenya hata, Ila kwa sababu Taifa limejengwa kwa misingi ya Upumbavu, basi tunajiona tuko sawa.
 
Mkalenjini huyu ana kiburi kile cha asili. Sijui labda atausikiliza ushauri wako.
 
Aende kwa Putin, yeye ndo asili ya jambo hili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…