SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 7,895
- 12,975
Ni jambo jema kupeleka mechi kubwa katika maeneo tofauti ili watu wa maeneo ya huko ambao huwa hawana nafasi ya kuziona mechi kama hizo waweze kupata fursa hiyo. Shida kubwa inakuja kuwa viwanja hivyo haviandaliwi vizuri ili viendane na hadhi ya mechi husika. Ingekuwa vyema mechi kama hizi ambazo nyingi huwa zinajulikana mapema, ziende na uwekezaji mkubwa katika miundombinu ya maeneo husika ili ladha ya mechi isipotee na wenyeji tuwaache na kitu watakachokitumia baada ya mechi husika kuisha.
Tukumbuke sababu tuliyopewa ya kupeleka mechi zote za ngao ya Jamii Tanga ni kwamba uwanja wa Benjamin Mkapa uko katika matengenezo. Tunajua sehemu ya pitch kwa kiasi kikubwa matengenezo yake yatakuwa tayari yameisha au yako mwishoni maana tuliona mabadiliko makubwa katika pitch wakati wa mechi za mwisho mwisho za Yanga za shirikisho na zile za timu ya taifa dhidi ya Uganda na ile ya Niger. Cha kushangaza tofauti na taarifa tulizopewa na TFF, tumeambiwa siku ya sherehe za Yanga wiki ijayo zitafanyikia uwanja huo huo ikiwemo mechi kati ya Yanga dhidi ya Kaizer Chiefs. Hii inaashiria maboresho yanayoendelea pale hayazuii shughuli zingine kuendelea ikiwemo mechi kubwa kuchezwa.
Mechi zote 3 za mwaka huu za Ngao ya Jamii ni mechi kubwa na zitakazovutia watu wengi kuzifuatilia. Nashauri ili kulinda ladha ya mechi husika na pia kutoa fursa za watu wengi zaidi kuhudhuria, mechi hizo titawanywe katika miji tofauti. Tanga wabaki na mechi moja (kama ikibidi), nyingine ipelekwe Mbeya au Morogoro maana ni muda maeneo haya hawajapelekewa mechi kubwa kama hizi na fainali irudishwe Dar es Salaam. Mechi ya mshindi wa tatu iondolewe.
Uwanja wa Mkwakwani hauwezi kuhimili kutumika kwa mechi 4 mfululizo ndani ya muda mfupi kama ratiba ilivyotolewa inavyosema. Ikifika fainali ile pitch itakuwa kwenye hali mbaya sana na tutashuhudia fainali mbovu na pia uwezekano wa wachezaji kupata majeraha kwa sababu ya ubovu wa kiwanja.
Pia natoa rai kwa TFF kama taasisi ya umma waache tabia ya kudanganya na kutoa taarifa za uongo ili tu maamuzi yao yaweze kukubalika ambayo mengine yanaonekana yanafanywa kwa maslahi binafsi ya watu fulani.
FAINALI YA NGAO YA JAMII 2023 IRUDISHWE DAR ES SALAAM.
Tukumbuke sababu tuliyopewa ya kupeleka mechi zote za ngao ya Jamii Tanga ni kwamba uwanja wa Benjamin Mkapa uko katika matengenezo. Tunajua sehemu ya pitch kwa kiasi kikubwa matengenezo yake yatakuwa tayari yameisha au yako mwishoni maana tuliona mabadiliko makubwa katika pitch wakati wa mechi za mwisho mwisho za Yanga za shirikisho na zile za timu ya taifa dhidi ya Uganda na ile ya Niger. Cha kushangaza tofauti na taarifa tulizopewa na TFF, tumeambiwa siku ya sherehe za Yanga wiki ijayo zitafanyikia uwanja huo huo ikiwemo mechi kati ya Yanga dhidi ya Kaizer Chiefs. Hii inaashiria maboresho yanayoendelea pale hayazuii shughuli zingine kuendelea ikiwemo mechi kubwa kuchezwa.
Mechi zote 3 za mwaka huu za Ngao ya Jamii ni mechi kubwa na zitakazovutia watu wengi kuzifuatilia. Nashauri ili kulinda ladha ya mechi husika na pia kutoa fursa za watu wengi zaidi kuhudhuria, mechi hizo titawanywe katika miji tofauti. Tanga wabaki na mechi moja (kama ikibidi), nyingine ipelekwe Mbeya au Morogoro maana ni muda maeneo haya hawajapelekewa mechi kubwa kama hizi na fainali irudishwe Dar es Salaam. Mechi ya mshindi wa tatu iondolewe.
Uwanja wa Mkwakwani hauwezi kuhimili kutumika kwa mechi 4 mfululizo ndani ya muda mfupi kama ratiba ilivyotolewa inavyosema. Ikifika fainali ile pitch itakuwa kwenye hali mbaya sana na tutashuhudia fainali mbovu na pia uwezekano wa wachezaji kupata majeraha kwa sababu ya ubovu wa kiwanja.
Pia natoa rai kwa TFF kama taasisi ya umma waache tabia ya kudanganya na kutoa taarifa za uongo ili tu maamuzi yao yaweze kukubalika ambayo mengine yanaonekana yanafanywa kwa maslahi binafsi ya watu fulani.
FAINALI YA NGAO YA JAMII 2023 IRUDISHWE DAR ES SALAAM.