WIVU: Maana, faida na hasara zake


Thanx...........
 
Jiamini tu kama mpenzi wako akupenda wewe
 
Wivu ni maradhi hayana dawa, pole sana aisay :biggrin:
 
Wivu ni dalili za kutojiamini kwa upande fulani, anaglia chanzo, je unahisi unaibiwa au mpenzi wako si mwaminifu?
 
Wivu ni dalili za kutojiamini kwa upande fulani, anaglia chanzo, je unahisi unaibiwa au mpenzi wako si mwaminifu?

Ni mwaminifu sema nina woga si unajua wakiwa wazuri basi unahisi kuibiwa
 
Kaunga ...........ubarikiwe sana, kweli JF in ma great thinkerz! Max hebu turudishie ka batan ka senks
 
I like the way umeelezea

Kujiamini ni jibu la tatizo hilo
 
Hivi kuna namna ya kuzuia usipatwe na wivu wa mapenzi?unapokuwa na wivu wa kimapenzi kwa mtu ni
dalili ya kuwa unampenda mtu,sidhani kama utakuwa na wivu kama hujampenda mtu.Wivu husababisha
mtu kufanya maamuzi mabaya ambayo yanaathari na anaweza kujutia baadaye....hebu tusaidiane kama
kuna namna au jinsi ya kutibu wivu au kujiepusha na wivu.
 
Kumpenda mtu bila kumuamini ni kujiweka kitanzi mwenyewe. Hivyo dawa pekee ya kutokuwa na wivu ni kumuamini huyo umpendaye. Na kama humwamini achana naye usije ukapata ugonjwa wa moyo bure.
 
Kumuonea wivu mtuusiye na mahusiano naye ni dalili kabisa kuna kemia au jografia kwake.
Na wivu hauzuiliki, unakuja bila hata wewe kujua.

Ila cha muhimu, ni kujizuia usifanye au ropoka maneno mabaya
tena hasa kwa mtu ambaye huna ahusiano naye
atakushangaa, waweza sababisha hata huo urafiki uliopo kuvunjika
 
Kumpenda mtu bila kumuamini ni kujiweka kitanzi mwenyewe. Hivyo dawa pekee ya kutokuwa na wivu ni kumuamini huyo umpendaye. Na kama humwamini achana naye usije ukapata ugonjwa wa moyo bure.
tatizo ukiamini sana baadaye ukaja kugundua ndo utakufa kwa presha kabisa
 
achana na huyo ambaye huna uhusiano naye,je ambaye unauhusiano naye?
 
Kwanza jiulize ni kitu gani kinakufanya umuonee wivu?
Anazungumza na watu wengine wa jinsia tafauti?
Unaelewa uhusiano wake na hao anaozungumza nao?
Wewe je, una uhusiano na watu hao? Ikiwa ndio, huwaamini
au unahisi mwenzako anakusaliti?

Kwa upande wako, wewe hufanyi anayofanya yeye?
Ikiwa unafanya hayo hayo, kwa nini basi "anye kuku tu
bata akinya uchafu?

Dawa ya kutooana au kupunza wivu:
Jiamini na mwamini mwenzako!
Usitende usilotka utendewe!
Kila mtu hana hatia mpaka itakapothibitika kuwa ni mkosaji.
 
Wivu ni moja ya hisia za kiasili za kibinadamu. Huwezi ukazuia vitu au mambo asilia. Kama huwezi kujizuia kuny.a au kukojoa baada ya kula au kunywa, basi hutaweza kujizuia kusikia wivu kwa yule uliye na hisia za mapenzi kwake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…