Wivu wa Baba na Mama!

Kwanza nitaangalia ni dizaini gani ya jamaa amemleta..............then nitajua nini cha kufanya.
Broda,
Kitu ambacho sisi wazazi tunaoverlook ni hiki; Kuwa hadi binti anamleta Jamaa nyumbani, je ameshakuwa naye toka lini...hatujui hapo, yaani kwa hilo tunakuwa mapompompo!
Sasa unamkataa jama wakati ana miaka 3 na binti yako, matokeo binti anakamata ujauzito ule wa kukinga kwa makusudi ili akukomoe!
Mwisho wa siku unakua huna jinsi zaidi ya kuwakubalia wakaishi pamoja!
So tunapowakataa wacchumba wa wanetu tunapaswa kuwa na jicho la 3 la utambuzi!
 
PIIJEEY mi nadhani ni ''human nature'' hiyo...!

i mean ndo ubinadamu wenyewe huo...!yani hutokea tu kwamba baba anawapenda mno binti zake kiasi kwamba anahisi huyo anaeoa atamuumiza moyo mwanae..!nimeiona sana hiyo hata home...!mjomba angu alikataa kabisa hata kupokea mahari za binti zake wote..!akiamini maamuzi yao ya kuolewa hayakuwa sahihi..!lakin ndo hao hao waaliomuolea wanae ndo waliomuuguza kwa very special care hadi mungu anaichukua roho yake(r.i.p)...!ni kitu ambacho huwezi kukielezea kwa mtizamo wa kawaida...lakin naamini ''in a connection of love and care to the kids''..katika extent ambayo huwezi kabisa mpa mtu mwingine trust...!may be baba yuko sawa...au may be yuko wrong...!lakin maisha lazima yaendelee!

na kwa wakina mama ni hivo hivo kabisa kwa watoto zao wa kiume...!tena wakina mama ni wabaya zaidi...!kwa weakness zao wanaweza kutengeneza hata ''hate'' kwa wakamwana zao!i mean you know women..!unaweza letewa ''majungu'' kwamba unapendelea sana ndugu na wazaz wa upande wa mkeo...!lakin yote huanzia huko...!sijui niiwekeje lakin labda ninakosea pia...!nadhani labda kizazi hichi kije kibadilike kitakapokuwa kinaoza na kuozesha uzao wake...!

hongera piijeey kwa thread nzuri
 
Uzuri binti akipigwa mimba hata thamani inashuka kama alikuwa na thamani ya 1m mahari inashuka mpaka 150,00/= hii kwa mujibu wa uzoefu wangu mi nikija kumuoa Matesha unaleta za kuleta napiga mimba kisha nakuja kulipa uchafuzi.
Broda,
Umeshusha mno thamani aisee!!
Huu ni udhalilishaji wa binti pamoja na wazazi wake!..Fanya angalau Nusu-BEI!
 
Broda,
Umeshusha mno thamani aisee!!
Huu ni udhalilishaji wa binti pamoja na wazazi wake!..Fanya angalau Nusu-BEI!

Utake usitake hii ndo ulivyo binti akipigwa mimba nyumbani thamani yake inaporomoka mkuu kwa mujibu wa uzoefu wangu wa haya mambo ya ushenga ndo ilivyo unabeba mzigo kiulainiiiiiiiiiii
 
Teamo,
Kwanza karibu sana majamvini!...kupotea kwako majamvini kunaashiria kitu chema!...huenda soon tutakuwa na double G!
Back to yr post, umeongea maneno very touching mwanzo kati mwisho!

Nimeguswa zaidi na hapo kwenye blue!

Wazazi tuna nature ya too much protectionism kwa watoto, na hii inapelekea kudhani kuwa huenda chochote anachoamua mtoto kinahitaji kuwa revised na mzazi!(mtoto kwa mzazi hakui)...
Lakini tunasahau kuwa Mungu ndiye Provider mkuu wa WANADAMU, NA KWAMBA NI LAZIMA WAKATI FULANI KATIKA MAISHA TUKUBALI KUWA WATOTO WAMEKUA, NA WANAHITAJI MAISHA YAO WENYEWE.
Lakini Pamoja na hayo yote, lakini kuna wivu wa kawaida tu, usio na maelezo unaingilia suala hili!
 
mmmh hakunaga izo bwana pj?
huyo mzee ana yake si unajua wanaume wa dotcom hata makindayao wanarusha?
sket yeyote haikatizi kizazi hiki loh

Inaonekana Smile bado hujala chumvi nyingi, ni bora ungekaa kimya kwanza uwaachie wenye uzoefu wa kutosha na waliokula chumvi nyingi watuelezee kutokana na uzoefu wao.
 
Huyu dogo naona anataka kuwa chakula cha ANACONDA ODM. We mwache tu!

Hahahahahaha ukiwa mzazi na unatubinti kadhaa maskani kazi ipo tayari povu. Inabidi ukubali matokeo aidha unawashawishi mabinti waende usista au waolewe kwa kuangalia 3 credit ya C C C
 
Wapo wanaosema kuwa natutally mama yuko more connected and protective kwa mtoto wake wa kiume, baba hivyo hivyo kwa mtoto wa kike. Opposite sex attraction. Kuna wakati mwingine unakuta hata mtoto wa kike anataja jina la baba yake mara nyingi zaidi ya jina la mama. Na kwa mtoto wa kiume ni hivyo hivyo pia.

Wengine wanadai hii inatokana na pressure toka kwa jamii. Kwamba baba ndiye anayekuwa na jukumu zaidi la linapokuja suala la kumfunza mtoto wa kiume. Jamii inategemea kuwa baba atamfundisha kijana wake wa kiume tabia nzuri na kumwonyesha jinsi ya kuwa "mwanaume." Jamii inategemea mwanaume kuwa "mwanaume wa ukweli". Baba ana-pass hiyo expectation kwa mtoto wake wa kiume. Baba pia angetaka mtoto wake wa kiume afanikiwe sio lazima kwa kuendesha biashara ya familia yake bali kwa kuendeleza jina la familia na kukaa mahali na kusema "yes, that's my son".

Hivyo hivyo inatokea kwa mtoto wa kike. Mara nyingi kwenye jamii yetu, mtoto wa kike anakuzwa na mama yake, ambaye atamfundisha jinsi ya kuwa "mwanamke". Mtoto wa kike ana standards pia ambazo mama yake analinganisha and hold her to.

Muhimu ni kuwa bado baba na mama wanawapenda watoto wao wa kiume na kike a lot. Lakini kwa haraka mtoto wa kiume anajifunza kuwa mama anasemehe zaidi kuliko baba anbaye saa zote yuko strict akimtaka ajifunze ili aje aliendeleze jina la familia baadae. Mama naye anaona discipline ya mtoto wa kiume ni kazi ya baba. Hivyo hivyo, mtoto wa kike ana-learn kuwa she can get away with more with daddy kwa sababu sio jukumu lake kumfunza na mwenye jukumu hilo (mama) ambaye anamkosoa tuu (actually inasemekana ukosoaji wa mama ndio unawafanya mabinti wengi kuwa insecure hasa pale unapokuta confort zone yaani baba hayupo).

Uhusiano huu unaendelea hata watoto wakiwa wakubwa na kufikia umri wa kuoa/olewa. Sometimes, unakuta kijana as if he is in relationship with two women (mke na mama yake). Kwa situation kama yako, nafikiri huyo mwanaume na mwanamke wanaotaka kuoana ndio wana jukumu zaidi la kuwaondolea mashaka wazazi wao. Sio rahisi kwa mwanaume kum-ditch mama yake baada ya ndoa lakini la muhimu ni zaidi ni jinsi atakavyoweza ku-manage both of them and the two women live happily thereafter. Inawezekana.

The fact kwamba kuna baadhi ya mothers are so possessive, they don't want to cut that virtual umbilical cord and let her son go, ni kazi ya mtoto to put his mother to order. Kwa baba anajua dangers zinazomkabili binti yake ahead. So, he tries to keep her away from the wolves in man skins. Hapa ni pagumu lakini ndio uhalisia wenyewe. Itakuwa vigumu kwa binti kumdhibitishia baba kuwa everything will be fine hasa kama baba has been there, done it, na ameretire or possibly is still doing it.

Pia soma huu utafiti hapa: Sons really are their mother's favourites as 88 per cent admit treating boys differently | Mail Online
 
Bora hata mabinti huwa hawasahau walikotoka
Wanamme wanahamia kutunza ukweni tu
Kwa nini roho isiume kwa mama mzazi?
Zamani ulikuwa unapigwa na wax, saa hivi hata vocha hakuna lol

Hahahaha kwa hiyo vijana wa kiume wanao oa mapenzi siku hizi wanazidisha kwa mama mkwe kuliko kwa mzazi aliye beba mimba kwa miezi 9 na kumlea na kuhangaika huku na huku kwa kuuza vitumbua kijana asome
 
Hahahaha kwa hiyo vijana wa kiume wanao oa mapenzi siku hizi wanazidisha kwa mama mkwe kuliko kwa mzazi aliye beba mimba kwa miezi 9 na kumlea na kuhangaika huku na huku kwa kuuza vitumbua kijana asome
Chezeiya watoto wa kiume, hawana muamana kabisa wakishaoa.
Mama mzazi anakuwa kama 3rd party companiy badala ya affiliate company.

Broda,
Umeshusha mno thamani aisee!!
Huu ni udhalilishaji wa binti pamoja na wazazi wake!..Fanya angalau Nusu-BEI!
 
Chezeiya watoto wa kiume, hawana muamana kabisa wakishaoa.
Mama mzazi anakuwa kama 3rd party companiy badala ya affiliate company.

Kwa hiyo malupulupu na masurufu yote ya mwanaume anakula mzaa chema mama wa mwanaume anapiga miayo tu
 

Mpaka sasa mzee wangu hapendi watu wafupi ingawa sababu yake huwa ni kama kichekesho kuwa familia itaanza kuwa na watu wafupi, pia huyo wa pili sikumwambia ilikuwa ni zile za wazee tuunganishe koo so baba wa kijana kaleta posa hata kijana sikuwahi kumjua hakuwa nchini kwa wakti huo.
 
Uzuri binti akipigwa mimba hata thamani inashuka kama alikuwa na thamani ya 1m mahari inashuka mpaka 150,00/= hii kwa mujibu wa uzoefu wangu mi nikija kumuoa Matesha unaleta za kuleta napiga mimba kisha nakuja kulipa uchafuzi.

mkuu!umeua vibaya sana!hiyo ni 15,000 enhe?maana ina zero 3 tu!
 

You said it all Asha Di. I always admire your contributions.
 
Inaonekana Smile bado hujala chumvi nyingi, ni bora ungekaa kimya kwanza uwaachie wenye uzoefu wa kutosha na waliokula chumvi nyingi watuelezee kutokana na uzoefu wao.
mKUU,
Haya mambo bila uzoefu magumu na yanaonekana kama michapo tu!
 
EMT,
This is a very useful post!
PHP:
Muhimu ni kuwa bado baba na mama wanawapenda watoto wao wa kiume na kike  a lot. Lakini kwa haraka mtoto wa kiume anajifunza kuwa mama anasemehe  zaidi kuliko baba anbaye saa zote yuko strict akimtaka ajifunze ili aje  aliendeleze jina la familia baadae. Mama naye anaona discipline ya mtoto  wa kiume ni kazi ya baba. Hivyo hivyo, mtoto wa kike ana-learn kuwa she  can get away with more with daddy kwa sababu sio jukumu lake kumfunza  na mwenye jukumu hilo (mama) ambaye anamkosoa tuu (actually inasemekana  ukosoaji wa mama ndio unawafanya mabinti wengi kuwa insecure hasa pale  unapokuta confort zone yaani baba hayupo).
Hapa ndipo penye siri yote ya hii kitu ya wivu, au labda tuite unaodhaniwa kuwa upendo..!
Mkuu umeenda kwenye mzizi wa jambo hili!
 
PJ umegusa penyewe...ni wivu uliochanganyika na uwoga juu. Nimeshuhudia mama ambae alimkataa rafiki wa kijana wake eti kwa sababu sio mtoaji, lakini akamkubali msichana mwingine ambae alikuwa haishi kumzawadia mama wa kijana kwa wax za hapa na pale. Mwisho wa siku kijana aliishia kumuoa huyu mtoa zawadi kwa ajili ya shinikizo la mama. Mtoa zawadi kaolewa lakini kijasho kinamtoka...
Nilipata pia kusikia kuhusu baba mmoja aliejaliwa mabinti watatu, baba huyo ni mchafuaji wa wake za watu hadi watoto wa watu....ma binti wawili (wakubwa) walishaolewa lakini ndio baba alikuwa shingo upande kwani alikuwa anatoa pingamizi kwa sababu zisizo na maana. Sasa ilipofika zamu ya last born...baba mtu akawa anatoa za "It cant be, she is still a baby"...ilibidi mama mtu akomae na kumpasha mume kuwa jamii haitamuelewa!..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…