Mwanongwa
JF-Expert Member
- Feb 15, 2023
- 611
- 567
Kero yangu kubwa ni kwa mamlaka inayosimamia huduma za Afya katika Halmashauri ya Tunduma Mkoani Songwe, kumekuwa na tatizo la wauzaji wa Nyama kuuza nyama zenye mashaka ya ubora na baadhi wanauza zikiwa zimeharibika.
Nimefuatilia na kubaini kuwa mara nyingi nyama hizo zimekuwa zikiweka kwenye friji muda mrefu na nyingine hazitunzwi vizuri matokeo yake zinaharibika.
Pia baadhi ya vyumba vya kuuzia nyama havina viwango, ni kawaida kukuta chumba kimezungukwa na nzi wa kila aina pamoja na wadudu wengine kadhaa, na hata unapowauliza wahusika wengi wao wanaonekana kutojali hilo.
Tunaomba mamlaka inayohusika kufuatilia, kuchukua hatua kwa kuwa afya za walaji zipo hatarini, na inavyoonesha hata Mamlaka za Afya huku ni kama nazo zinachukulia poa tu hali hiyo.
Nimefuatilia na kubaini kuwa mara nyingi nyama hizo zimekuwa zikiweka kwenye friji muda mrefu na nyingine hazitunzwi vizuri matokeo yake zinaharibika.
Pia baadhi ya vyumba vya kuuzia nyama havina viwango, ni kawaida kukuta chumba kimezungukwa na nzi wa kila aina pamoja na wadudu wengine kadhaa, na hata unapowauliza wahusika wengi wao wanaonekana kutojali hilo.
Tunaomba mamlaka inayohusika kufuatilia, kuchukua hatua kwa kuwa afya za walaji zipo hatarini, na inavyoonesha hata Mamlaka za Afya huku ni kama nazo zinachukulia poa tu hali hiyo.