DOKEZO Wizara ya Afya ifuatilie ubora wa nyama inayouzwa Mitaa ya Mpemba – Tunduma pia wauzaji hawazingatii usafi

DOKEZO Wizara ya Afya ifuatilie ubora wa nyama inayouzwa Mitaa ya Mpemba – Tunduma pia wauzaji hawazingatii usafi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Mwanongwa

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2023
Posts
611
Reaction score
567
Kero yangu kubwa ni kwa mamlaka inayosimamia huduma za Afya katika Halmashauri ya Tunduma Mkoani Songwe, kumekuwa na tatizo la wauzaji wa Nyama kuuza nyama zenye mashaka ya ubora na baadhi wanauza zikiwa zimeharibika.

Nimefuatilia na kubaini kuwa mara nyingi nyama hizo zimekuwa zikiweka kwenye friji muda mrefu na nyingine hazitunzwi vizuri matokeo yake zinaharibika.

Pia baadhi ya vyumba vya kuuzia nyama havina viwango, ni kawaida kukuta chumba kimezungukwa na nzi wa kila aina pamoja na wadudu wengine kadhaa, na hata unapowauliza wahusika wengi wao wanaonekana kutojali hilo.

Tunaomba mamlaka inayohusika kufuatilia, kuchukua hatua kwa kuwa afya za walaji zipo hatarini, na inavyoonesha hata Mamlaka za Afya huku ni kama nazo zinachukulia poa tu hali hiyo.
 
Afya ni muhimu kuliko hizo nyama. Funga mala moja hizo bucha na machinjio hadi hali itakapokaa vema. Waziri wa afya
 
Kero yangu kubwa ni kwa mamlaka inayosimamia huduma za Afya katika Wilaya ya Tunduma Mkoani Songwe, kumekuwa na tatizo la wauzaji wa Nyama kuuza nyama zenye mashaka ya ubora na baadhi wanauza zikiwa zimeharibika.

Nimefuatialia na kubaini kuwa mara nyingi nyama hizo zimekuwa zikiweka kwenye friji muda mrefu na nyingine hazitunzwi vizuri matokeo yake zinaharibika.

Pia baadhi ya vyumba vya kuuzia nyama havina viwango, ni kawaida kukuta chumba kimezungumzwa na nzi wa kila aina pamoja na wadudu wengine kadhaa, na hata unapowauliza wahusika wengi wao wanaonekana kutojali hilo.

Tunaomba mamlaka inayohusika kufuatilia, kuchukua hatua kwa kuwa afya za walaji zipo hatarini, na inavyoonesha hata Mamlaka za Afya huku ni kama nazo zinachukulia poa tu hali hiyo
mwaka jana mwezi wa kwanza nikaa hapo wiki tatu aise hao jamaa hawazingatii usafi kabis mpak naondoka hapo sikuwah kula nyama..s kwa nzi hzo utadhani mkutano wa CCM..Nyama nilienda kula Kayanga.
 
Back
Top Bottom