#COVID19 Wizara ya Afya yakanusha uvumi kwamba Waziri Mkuu alisema hakuna Wimbi la Nne la UVIKO-19

#COVID19 Wizara ya Afya yakanusha uvumi kwamba Waziri Mkuu alisema hakuna Wimbi la Nne la UVIKO-19

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA. WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO.


TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UPOTOSHAJI WA MATAMKO YA VIONGOZI JUU YA MWENENDO WA UVIKO-19 NCHINI

Dodoma, Tarehe 20 Disemba, 2021.

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, imebaini taarifa za upotoshaji kwenye mitandao ya kijamii, kati ya taarifa iliyotolewa na Waziri Mkuu kwamba hakuna wimbi la nne la UVIKO-19 na ile iliyotolewa na Katibu Mkuu Afya kuhusu kuongezeka kwa maambukizi ya UVIKO-19.

Kimsingi taarifa zote hizi ni sahihi na wala hazipingani kabisa. Hii ni kwa kuwa, kuongezeka kwa maambukizi au Visa hakumaanishi kuwa tayari ni wimbi jipya la maambukizi na kitaalamu hii hujulikana kama resurgence of new cases (kuongezeka kwa maambukizi mapya). Kwa tafsiri halisi iliyotolewa na Stephen X. Zhang et al kwenye Jarida la Risk Management Health Policy la tarehe 13 Septemba 2021 “wimbi ni tofauti na ongezeko linalotokea ghafla na kwa kipindi kifupi (resurgence); ili kusema kuna wimbi jipya ni lazima hali ya ongezeko iendelee kwa kipindi fulani (walau kati ya siku 14-21)”.

Hivyo, kwa maelezo haya ya kitaalamu wananchi wapuuze upotoshaji wa taarifa sahihi za viongozi wote wawili na zimetolewa kwa wakati tofauti kama mwendelezo wa Serikali kuwasiliana na Umma. Aidha, wananchi wanakumbushwa kuendelea kuchukua tahadhari na kujikinga kwani ugonjwa wa UVIKO-19 bado upo na maambukizi yamekuwa yakiongezeka. Wizara inaendelea kufuatilia mwenendo wa ugonjwa huu na itakuwa inatoa taarifa kulingana na mabadiliko kadri yanavyotokea kwa mujibu wa takwimu za kila siku.

Imetolewa na;

Prof Abel N. Makubi
Katibu Mkuu (Afya)
View attachment 2051611
Dah! Ngoja nitasoma tena wiki ijayo maana leo nimeishia kwenye kichwa cha habari tu.
 
Kama Mungu Jehova alivyotuvusha kwenye mawimbi yote yaliyopita ndio ametuvusha na hapa,na ndio atatuvusha na mawimbi yajayo km yapo
 
Uyo waziri mkuu hizo piko anazopakaa kichwani zimemuharibu ubongo, muongo muongo sana alafu hachagui pakuongopea yaani mpaka msikitini anaongea tu uongo
 
Anachapa kazi,mnataka aende wapi kariakoo?

IMG_20211221_134205_429.jpg
 
Covid 19 ni siasa na pia ni suala linalohusu uchumi wa nchi. Taarifa kwa umma kuhusu covid 19 waachiwe wanasiasa wenyewe ambao kwa wizara ya afya ni waziri wa afya pekee. Hao wengine kama katibu mkuu na mganga mkuu wa wizara ni washauri tu wa waziri wa afya ambaye ndiye msemaji wa wizara. Short of this itapelekea mkanganyiko ndani ya serikali na kwa umma. 'The boss is always right' should be the principle of governance. Tumeona wakina Polepole, Gwajima na Silaa wanavyopata taabu despite kwamba they were perfectly right!
 
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA. WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO.


TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UPOTOSHAJI WA MATAMKO YA VIONGOZI JUU YA MWENENDO WA UVIKO-19 NCHINI

Dodoma, Tarehe 20 Disemba, 2021.

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, imebaini taarifa za upotoshaji kwenye mitandao ya kijamii, kati ya taarifa iliyotolewa na Waziri Mkuu kwamba hakuna wimbi la nne la UVIKO-19 na ile iliyotolewa na Katibu Mkuu Afya kuhusu kuongezeka kwa maambukizi ya UVIKO-19.

Kimsingi taarifa zote hizi ni sahihi na wala hazipingani kabisa. Hii ni kwa kuwa, kuongezeka kwa maambukizi au Visa hakumaanishi kuwa tayari ni wimbi jipya la maambukizi na kitaalamu hii hujulikana kama resurgence of new cases (kuongezeka kwa maambukizi mapya). Kwa tafsiri halisi iliyotolewa na Stephen X. Zhang et al kwenye Jarida la Risk Management Health Policy la tarehe 13 Septemba 2021 “wimbi ni tofauti na ongezeko linalotokea ghafla na kwa kipindi kifupi (resurgence); ili kusema kuna wimbi jipya ni lazima hali ya ongezeko iendelee kwa kipindi fulani (walau kati ya siku 14-21)”.

Hivyo, kwa maelezo haya ya kitaalamu wananchi wapuuze upotoshaji wa taarifa sahihi za viongozi wote wawili na zimetolewa kwa wakati tofauti kama mwendelezo wa Serikali kuwasiliana na Umma. Aidha, wananchi wanakumbushwa kuendelea kuchukua tahadhari na kujikinga kwani ugonjwa wa UVIKO-19 bado upo na maambukizi yamekuwa yakiongezeka. Wizara inaendelea kufuatilia mwenendo wa ugonjwa huu na itakuwa inatoa taarifa kulingana na mabadiliko kadri yanavyotokea kwa mujibu wa takwimu za kila siku.

Imetolewa na;

Prof Abel N. Makubi
Katibu Mkuu (Afya)
View attachment 2051611
Kimsingi taarifa zote hizi ni sahihi na wala hazipingani kabisa. Hii ni kwa kuwa, kuongezeka kwa maambukizi au Visa hakumaanishi kuwa tayari ni wimbi jipya la maambukizi na kitaalamu hii hujulikana kama resurgence of new cases (kuongezeka kwa maambukizi mapya
Uongozi bora ni ule unaotoa kauli zisizo na mkaganyiko. Inapotokea mkaganyiko kwa kisingizio cha lugha ya kitaalam wakati unajua ujumbe unatolowa kwa watu wasio wataalam basi kuna shida.
 
Naomba Kuuliza kwa wataalam:
Hivi Kama Mtu hajachanjwa Mpaka sasa hivi,
1.Je akiugua Corona sasa hivi atakuwa ameugua corona ipi? Ile ya Kwanza,Ya Pili ya Tatu au hii Omicroni?
2.Je Ina Maana Zile Corona na Mwanzo Hazipo?Kama Zipo Zina Nguvu ya Kuwashambulia watu wasiochanjwa?
Kama Hazina Nguvu sasa Wasiochanjwa wamepata Kinga ya Mwili?
3.Hii Omicron na Yenyewe Kuna watu wamepata Mafua na Homa za Hapa na Pale na Wanaendelea Ku recover na Hawajachanjwa sasa Baadae Wakihitajika Kuchanjwa wanachanjwa kwa ajili ya wimbi lipi?
Kuanzia La Kwanza?Au hili la Sasa hivi?
Naomba Majibu wataalam
 
Back
Top Bottom