Katika kile kinachoonyesha wizara ya elimu haina imani na walimu wa kiswahili,English,Biology na kiswahili,wameandaa mitihani ya wizara katika masomo hayo.Mtihani utafanywa na wanafunzi wa kidato cha nne tar 27 mwezi huu kwa shule zitakazoteuliwa.Baada ya mitihani hiyo wizara itafanya tathmini ya mitihani hiyo kisha walimu wa masomo hayo watapewa semina ili kuboresha taaluma zao.Hayo yapo kwenye barua iliyoandikwa na kusainiwa na katibu mkuu wa wizara ya elimu Paulina Mkonongo,kwenda kwa makatibu tawala wa mikoa.Kichwa cha habari cha barua hiyo ni PROGRAMU YA KUBORESHA TAALUMA YA WALIMU NA WANAFUNZI WA SHULE ZA SEKONDARI.Habari za ndani zinasema wizara ina wasiwasi na ubora wa walimu katika masomo hayo