Wizara ya Elimu tafadhali chunguzeni ratiba za masomo katika Vyuo vya Kati na Juu

Wizara ya Elimu tafadhali chunguzeni ratiba za masomo katika Vyuo vya Kati na Juu

Chendembe

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2019
Posts
444
Reaction score
488
Nawasalimu kwa kutoa maoni yangu katika upangaji wa ratiba katika vyuo mbalimbali hapa nchini.

Naomba Wizara ya Elimu na wahusika kupitia ratiba za masomo vyuoni. Imekuwa kawaida sasa kuona ratiba hizo kupangwa kutokana na nafasi za walimu wa masomo vyuoni kuelekea vipindi vingine kuanzia usiku.

Kwangu naona vipindi vya usiku vinahatarisha maisha ya watoto wetu hususani katika majiji yetu. Pia, inashawishi vijana wengi kujihusisha na tabia chafu.

Kwa hali ya kuongezeka kwa udahili vyuoni na upungufu wa mabweni kwa sasa, ni hatari kwa maisha kwa wanaosoma vipindi hivyo ukizingatia baadhi ya maeneo ambayo wanachuo wengi upanga vyumba.

Nashauri ratiba iendane na muda wa kazi wa Serikali na sio nafasi ya mwalimu.

Nawasilisha
 
UDSM ratiba zilianza 0700 to 2000 hrs! Unataka chuo kikuu iwe kama sekondari?
 
Udsm ratiba zilianza 0700 to 2000 hrs! Unataka chuo kikuu iwe kama sekondari?
Nimetazama hali ya makazi ya wanachuo wengi na mtindo wa maisha Yao ni huruma kwa kweli. Jiulize tu katika kipindi kile Cha panyaroad hofu ilikuwaje kwao.
 
Lakini wa Tanzania kwa kulalamika hawajambo, hapo wataka wizara iwapangie ratiba nyie wazazi kwanini msikutane na uongozi wa chuo mtowe maoni yenu, au mhamishe watt wenu.
 
Kuna watu wako makazini wanaongeza visomo vyao na hivyo kuwalazimu kuingia madarasa ya usiku....wakipeleka mapendekezo ya ratiba za darasani wawe na valid reason why muda upunguzwe....suala la usalama sio issue ni watu wazima hao from 18yrs....kwanza wanakesha maclub wanarudi mida mibaya na hawalalamikii usalama how come wanalalamika kipindi cha saa2 useless! Ingekua hata wanafunzi wanajiongeza basi waseme wanafanyaga kazi hyo mida hakuna...ni darasani hostel mapenzi na ulevi wacha dawa iwaingie
 
Back
Top Bottom