Milonji
Senior Member
- May 26, 2022
- 166
- 510
Nani atasikiliza sauti zao, watoto hawa wanaolia.
Nani atawafuta machozi yao yanayo sombwa na Maji.
Nani atayaona machozi yao ikiwa watabaki kulia ndani kwa ndani.
Chaliko ninawasilisha kilio chao na kupaza sauti zao ili Mamlaka zinazohusika zisikie Changamoto wanazopitia Wanafunzi hawa.
Tangu kufunguliwa kwa Shule Wanafunzi wa Shule hii wamekuwa wakisoma kwa kusuasua Sana.
Kuna wakati wanakaa siku zaidi ya tatu bila kusoma na Kuna masomo hawajasoma kwa muda mrefu.
Hawa Wanafunzi wa kidato Cha Nne na cha Pili watafanyaje MITIHANI yao ya Taifa kama hawakufundishwa.
Nina waonea Huruma Wanafunzi hawa ambao hawafundishwi kisa Mwenye Shule ameshindwa kuwalipa walimu Mishahara na Walimu wameweka mgomo wa Chini kwa Chini.
Ninawaonea Huruma kwa sababu wamelipa Ada ambayo Wazazi wameitafuta kwa Hali na Mali kwa ajili ya kuwapatia watoto maarifa amabayo hawapewi.
Ninawaonea huruma kwa sababu Elimu ni haki yao na hakuna anaye wajali.
Ninawaonea huruma kwa sababu hawa ni Ndugu zetu.
Wizara ya Elimu tusaidiane kulishughulikia hili haraka iwezekanavyo ili watoto wapate haki yao ya Msingi.
NCHI: TANZANIA
MKOA: DODOMA
WILAYA:. DODOMA CC
KATA:. NKUHUNGU
SHULE:. NKUHUNGU SEKONDARI
Ndugu zangu, Sikilizeni Sauti, Yaoneni na kuyafuta Machozi ya Wanafunzi wa NKUHUNGU SEKONDARI ili ndoto zao zipate Kutimia.
Taarifa kwa;
Wadau wa Elimu
Afisa Elimu Kata ya Nkuhungu.
Afisa Elimu Jiji la Dodoma.
Afisa Elimu Mkoa wa Dodoma.
Wizara ya Elimu.
TAMISEMI
Wenu Milonji.
Nani atawafuta machozi yao yanayo sombwa na Maji.
Nani atayaona machozi yao ikiwa watabaki kulia ndani kwa ndani.
Chaliko ninawasilisha kilio chao na kupaza sauti zao ili Mamlaka zinazohusika zisikie Changamoto wanazopitia Wanafunzi hawa.
Tangu kufunguliwa kwa Shule Wanafunzi wa Shule hii wamekuwa wakisoma kwa kusuasua Sana.
Kuna wakati wanakaa siku zaidi ya tatu bila kusoma na Kuna masomo hawajasoma kwa muda mrefu.
Hawa Wanafunzi wa kidato Cha Nne na cha Pili watafanyaje MITIHANI yao ya Taifa kama hawakufundishwa.
Nina waonea Huruma Wanafunzi hawa ambao hawafundishwi kisa Mwenye Shule ameshindwa kuwalipa walimu Mishahara na Walimu wameweka mgomo wa Chini kwa Chini.
Ninawaonea Huruma kwa sababu wamelipa Ada ambayo Wazazi wameitafuta kwa Hali na Mali kwa ajili ya kuwapatia watoto maarifa amabayo hawapewi.
Ninawaonea huruma kwa sababu Elimu ni haki yao na hakuna anaye wajali.
Ninawaonea huruma kwa sababu hawa ni Ndugu zetu.
Wizara ya Elimu tusaidiane kulishughulikia hili haraka iwezekanavyo ili watoto wapate haki yao ya Msingi.
NCHI: TANZANIA
MKOA: DODOMA
WILAYA:. DODOMA CC
KATA:. NKUHUNGU
SHULE:. NKUHUNGU SEKONDARI
Ndugu zangu, Sikilizeni Sauti, Yaoneni na kuyafuta Machozi ya Wanafunzi wa NKUHUNGU SEKONDARI ili ndoto zao zipate Kutimia.
Taarifa kwa;
Wadau wa Elimu
Afisa Elimu Kata ya Nkuhungu.
Afisa Elimu Jiji la Dodoma.
Afisa Elimu Mkoa wa Dodoma.
Wizara ya Elimu.
TAMISEMI
Wenu Milonji.