Wizara ya Maendeleo inaomba Maoni yako kuhusu Muswada wa Sheria za Ulinzi wa Watoto

Wizara ya Maendeleo inaomba Maoni yako kuhusu Muswada wa Sheria za Ulinzi wa Watoto

Dkt. Gwajima D

Minister
Joined
Nov 28, 2015
Posts
966
Reaction score
6,019
Wasaalam,

Tafadhali ikikupendeza soma maelekezo ya kiambatisho hapa chini SEHEMU YA PILI (b).

Kisha tafadhali tenga muda wako usome utoe maoni yako kama ilivyoelekezwa kwenye tangazo lililoambatishwa.

Natanguliza shukrani.

Source insta @bunge.tanzania

IMG-20240814-WA0018.jpg
IMG-20240814-WA0019.jpg
 
Tunaomba itungwe sheria iwe ni kosa la jinai mzazi au mlezi kutompeleka mtoto shule ama kufanya njama mtoto aache shule.

Iwe ni kosa la jinai mtoto kutopatiwa mahitaji yake muhimu, yakiwemo ya shule.
 
Adhabu za viboko ni kudhalilisha na kuutweza utu wa mtoto nashangaa ulimwengu wa leo bado kuna watu wanaamini kwenye vipigo kama njia ya kutatua kosa.

Ingekuwa viboko/ vipigo ni njia ya kurekebisha mtoto basi Afrika hususan Tanzania ingekuwa mbali sana kiteknolojia lakini ni kinyume chake.

Watoto wamekuwa wakiadhibiwa hadi kupelekea ulemavu wa kudumu ama vifo lakini serikali haina muda kabisa juu ya kuwalinda watoto dhidi ya ukatili huu mashuleni na majumbani sijui hadi aje afe mtoto wa waziri ndiyo adhabu hizi za kikatili zifutwe.
 
Adhabu za viboko ni kudhalilisha na kuutweza utu wa mtoto nashangaa ulimwengu wa leo bado kuna watu wanaamini kwenye vipigo kama njia ya kutatua kosa.

Ingekuwa viboko/ vipigo ni njia ya kurekebisha mtoto basi Afrika hususan Tanzania ingekuwa mbali sana kiteknolojia lakini ni kinyume chake.

Watoto wamekuwa wakiadhibiwa hadi kupelekea ulemavu wa kudumu ama vifo lakini serikali haina muda kabisa juu ya kuwalinda watoto dhidi ya ukatili huu mashuleni na majumbani sijui hadi aje afe mtoto wa waziri ndiyo adhabu hizi za kikatili zifutwe.
Viboko na adhabu ziwepo ila kwa kiasi na kuzingatia utu na maadili kutokuwepo kabisa madhara yake ni makubwa.
 
1. Itungwe Sheria, Wenza wanapotengana, mwenye uwezo wa Kumtunza Mtoto kihuduma, ndîo apewe Mtoto.
Mwingine awe na Haki tuu ya kumwona Kwa utaratibu utakaowekwa.
Kwa sababu kûna weñye tàbia ya kung'ang'ania Watoto huku uwezo wa kuwatunza Hawana. Hii inapelekea Watoto wengi kukosa Haki ya Malezi Bora na wengi Ndoto zào huishia Njiani.

2. Mtoto asikae Kwa ndugu kama Wazazi wake wawili wàpo.
Ima akae Kwa Babaake au Kwa Mamaake.

3. Mtoto anahaki ya kumjua mzazi wake halisi.
Masuala ya kusema kitanda hakizai haramu humnyima Mtoto Haki ya kujua Wazazi wake halisi na hiyo kumharibia Maisha take yote na kizazi chake.
Hivyo sheria ya Kupima DNA ísiwe na mlolongo ili kuwapa Haki Watoto na wenye Mtoto.
Hii Sheria NI kama kweli Haki inahitajika, lakini kama NI geresha siô lazima.

4. Mtoto awe na Haki ya kuchagua Ûkoo íwe wa Mama au wa Babaake. Ikiwa kutatokea utengano.
Masuala ya kulazimisha ûkoo unatoka Kwa Baba au Mwanaume ni Haki endapo kuna Ndoa au Mtoto kalelewa na Baba au Mwanaume. Lakini Mtoto aliyelelewa Kwa upande wa Mama awe na Haki ya kuchagua majina na kuwa ûkoo wa ujombani, kiukeni.

5. Adhabu za Mtoto zilenge dhamiri ya Mtoto.
Mtoto àmbaye hajakusudia kufanya Kosa asiadhibiwe na Yule aliyedhamiria kufanya Makosa apewe adhabu inayolingana na Kosa lake.

6. Mtoto akiwa Yatima tangu kuzaliwa, au chini ya Miaka mitano. Apewe Haki ya Kurithi kwèñye familia atakayolelewa. Na atakayemlea apewe Haki ya kumfanya huyo Mtoto kuwa Mtoto wake Kwa njia ya adaptation hata kama ni ndugu yake.

Ikiwa Mtoto NI Yatima Kwa Mzazi mmoja, na Mzazi aliyebaki Hai akamtelekeza Mtoto huyo Kwa namna Moja ama ñyiñgine. Na kusababisha Mtoto huyo kulelewa na Kukuzwa na familia ñyiñgine isiyo ya ukoo wa huyo Mzazi aliyehai. Mtoto huyo atakuwa chini ya ukoo wa alikolelewa, ingawaje Sheria haitakataza mtoto kuambiwa ukweli kuhusu mzazi wake halisi.

Mzazi hatakuwa na Mamlaka ya kumchukya Mtoto huyo isipokuwa Kwa makubaliano na hiyari ya Mlezi WA huyo Mtoto.

Sheria hiyo itafaa zaidi kama Mtoto atalelewa Kwa zaidi ya Miaka Kumi,

7. Mtoto akishakuwa Mkubwa hatakuwa na wajibu wa Kumtunza Mzazi àmbaye hakumlea akiwa Mtoto.
Isipokuwa Kwa hiyari ya mtoto mwenyewe .
Mzazi àmbaye hakumlea Mtoto hatakuwa na Haki ya kumsumbua Mtoto wake na kumfanya Mtoto ataabike kwaajili yake isipokuwa atasubiri hiyari ya mtoto mwenyewe.
Hiyo ndîo HAKI.

8. Mtoto endapo atakufa atakuwa na haki ya kuzikwa upande aliolelewa Ikiwa hakutoa maelekezo Mengine.
Mtu yeyote ikiwemo Mzazi ambaye hakuhusika na Malezi ya mtoto aliyekufa hatakuwa na Haki ya kudai Mwili WA Mtoto na kwenda kuuzika atakako. Isipokuwa Kwa hiyari ya waliomlea Mtoto huyo.

9. Mtoto akikua na kufikisha Umri wa kuoa au kuolewa weñye mamlaka ya kuratibu shughuli nzima ya Ndoa íwe upande alipokuzwa na kulelewa.
Au Kwa hiyari ya waliomlea wanaweza kufanya vinginevyo

10. Mtoto akishakua atakuwa na haki ya kuchagua mwenza wake wa Maisha atakayemridhia pasipo kuingiliwa.

11. Ikitokea Mwanamke kudanganya na kumbambikia Mumewe Mtoto ambaye siô wake. Mtoto ataendelea kuwa Mtoto wa huyo Mwanaume wa kambo kisheria mpaka atakapofikisha Umri wa kujitegemea. Ikiwa Mtoto akataka kwenda Kwa Babaake halisi, huyo Baba halisi itampasa atoe fidia ya Pesa Kulingana na Maisha ya kipindi husika
 
1. Itungwe Sheria, Wenza wanapotengana, mwenye uwezo wa Kumtunza Mtoto kihuduma, ndîo apewe Mtoto.
Mwingine awe na Haki tuu ya kumwona Kwa utaratibu utakaowekwa.
Kwa sababu kûna weñye tàbia ya kung'ang'ania Watoto huku uwezo wa kuwatunza Hawana. Hii inapelekea Watoto wengi kukosa Haki ya Malezi Bora na wengi Ndoto zào huishia Njiani.

2. Mtoto asikae Kwa ndugu kama Wazazi wake wawili wàpo.
Ima akae Kwa Babaake au Kwa Mamaake.

3. Mtoto anahaki ya kumjua mzazi wake halisi.
Masuala ya kusema kitanda hakizai haramu humnyima Mtoto Haki ya kujua Wazazi wake halisi na hiyo kumharibia Maisha take yote na kizazi chake.
Hivyo sheria ya Kupima DNA ísiwe na mlolongo ili kuwapa Haki Watoto na wenye Mtoto.
Hii Sheria NI kama kweli Haki inahitajika, lakini kama NI geresha siô lazima.

4. Mtoto awe na Haki ya kuchagua Ûkoo íwe wa Mama au wa Babaake. Ikiwa kutatokea utengano.
Masuala ya kulazimisha ûkoo unatoka Kwa Baba au Mwanaume ni Haki endapo kuna Ndoa au Mtoto kalelewa na Baba au Mwanaume. Lakini Mtoto aliyelelewa Kwa upande wa Mama awe na Haki ya kuchagua majina na kuwa ûkoo wa ujombani, kiukeni.

5. Adhabu za Mtoto zilenge dhamiri ya Mtoto.
Mtoto àmbaye hajakusudia kufanya Kosa asiadhibiwe na Yule aliyedhamiria kufanya Makosa apewe adhabu inayolingana na Kosa lake.

6. Mtoto akiwa Yatima tangu kuzaliwa, au chini ya Miaka mitano. Apewe Haki ya Kurithi kwèñye familia atakayolelewa. Na atakayemlea apewe Haki ya kumfanya huyo Mtoto kuwa Mtoto wake Kwa njia ya adaptation hata kama ni ndugu yake.

Ikiwa Mtoto NI Yatima Kwa Mzazi mmoja, na Mzazi aliyebaki Hai akamtelekeza Mtoto huyo Kwa namna Moja ama ñyiñgine. Na kusababisha Mtoto huyo kulelewa na Kukuzwa na familia ñyiñgine isiyo ya ukoo wa huyo Mzazi aliyehai. Mtoto huyo atakuwa chini ya ukoo wa alikolelewa, ingawaje Sheria haitakataza mtoto kuambiwa ukweli kuhusu mzazi wake halisi.

Mzazi hatakuwa na Mamlaka ya kumchukya Mtoto huyo isipokuwa Kwa makubaliano na hiyari ya Mlezi WA huyo Mtoto.

Sheria hiyo itafaa zaidi kama Mtoto atalelewa Kwa zaidi ya Miaka Kumi,

7. Mtoto akishakuwa Mkubwa hatakuwa na wajibu wa Kumtunza Mzazi àmbaye hakumlea akiwa Mtoto.
Isipokuwa Kwa hiyari ya mtoto mwenyewe .
Mzazi àmbaye hakumlea Mtoto hatakuwa na Haki ya kumsumbua Mtoto wake na kumfanya Mtoto ataabike kwaajili yake isipokuwa atasubiri hiyari ya mtoto mwenyewe.
Hiyo ndîo HAKI.

8. Mtoto endapo atakufa atakuwa na haki ya kuzikwa upande aliolelewa Ikiwa hakutoa maelekezo Mengine.
Mtu yeyote ikiwemo Mzazi ambaye hakuhusika na Malezi ya mtoto aliyekufa hatakuwa na Haki ya kudai Mwili WA Mtoto na kwenda kuuzika atakako. Isipokuwa Kwa hiyari ya waliomlea Mtoto huyo.

9. Mtoto akikua na kufikisha Umri wa kuoa au kuolewa weñye mamlaka ya kuratibu shughuli nzima ya Ndoa íwe upande alipokuzwa na kulelewa.
Au Kwa hiyari ya waliomlea wanaweza kufanya vinginevyo

10. Mtoto akishakua atakuwa na haki ya kuchagua mwenza wake wa Maisha atakayemridhia pasipo kuingiliwa.

11. Ikitokea Mwanamke kudanganya na kumbambikia Mumewe Mtoto ambaye siô wake. Mtoto ataendelea kuwa Mtoto wa huyo Mwanaume wa kambo kisheria mpaka atakapofikisha Umri wa kujitegemea. Ikiwa Mtoto akataka kwenda Kwa Babaake halisi, huyo Baba halisi itampasa atoe fidia ya Pesa Kulingana na Maisha ya kipindi husika
Kweli mdau umedhamiria kumlinda Mtoto. Safi.

“Get them while they are Young.”
 
Moto asitumwe dukani kununua chochote mwsho iwe saa 12jioni,2mtoto asitumwe kununua bia Wala sigara3Ni wajibu wa mzazi kumpa mahitaji ya muhimu mtoto 4Mtoto ana haki ya kucheza michezo na wenzake mwisho iwe saa 12jioni kutegemeana na jua linavyozama.Nawasilisha.
 
Suala la watoto kushinda mashuleni mda mwingi litolewe muongozo! Mtoto anatoka sa12 asubuhi na kurudi usiku na Watoto wengi siku hizi mpaka jumapili wanaenda shule kusoma hili nalo imekua kero kwa baadhi yetu wazazi!.

Watoto wanashindwa kupata malezi ya wazazi kwa uhakika na matokeo tutashindwa kujenga jamii iliyo bora kwa vizazi vyetu! Hivyo tungeomba elimu yetu iendane na malezi ya wazazi!
 
Kwa heshima na taadhima
Nawaomba wahusika hili suala la kupiga watoto kila leo ni unyanyasaji na uonezi kwa watoto
Kwa kuwa hawawezi kujitetea sisi tutapaza sauti mpaka mfute kabisa
Wanaotengeneza madawa na kuvumbua vitu kila leo hawachapwi ila nyie mnapiga halafu hata bakuli hawawezi kutengeneza
Sasa huwa mnawapiga ili iweje?

Tatizo hili mnaliangalia waalimu wanapiga mpaka wanauwa na watoto wengine kuachiwa ulemavu
Mnaruhusu fimbo 3 mwalimu anapiga 10 na adhabu juu, kwanini?
Kwa sababu mmeruhusu kupiga
Ila mkisema marufuku kipiga kutapungua sana labda mwafunge watakao kaidi
Mfano ni kama wale walioambiwa ni hela ya kubrashi, leo tunaona takwimu zao zilivyo kwa kupokea na kuchukua
Ukiruhusu kitu maana yake umehalalisha
Futeni kabisa upigaji watoto kuanzia nyumbani mpaka shuleni
 
Wasaalam,

Tafadhali ikikupendeza soma maelekezo ya kiambatisho hapa chini SEHEMU YA PILI (b).

Kisha tafadhali tenga muda wako usome utoe maoni yako kama ilivyoelekezwa kwenye tangazo lililoambatishwa.

Natanguliza shukrani.

Source insta @bunge.tanzania

View attachment 3069439View attachment 3069440
1. Itungwe Sheria kwamba ni kosa la jinai kwa wazazi/walezi kumtumia Mtoto kufanya biashara hususan ya kutembeza bidhaa yoyote kuuza e.g. vitafunwa, karanga n.k. au mtoto kuokota na kuuza takataka Plasitiki, vyuma chakavu, nguo mnadani n.k.
2. Iwepo Sheria itakayolinda haki ya Mtoto kupumzika/kuwa free. Hapa itamkwe muda wa masomo(Shuleni) muda wa kukaa na wazazi/walezi nyumbani kusaidia/kujifunza kazi ndogondogo kadri ya umri wake, Muda wa Mtoto kujichagulia afanye nini e.g. kucheza,na Muda wa kulala kitandani hata kama hana usingizi.
3. Iwepo sheria itakayowakataza i.e. Iwe ni Marufuku esp. Wazazi(Ke) Walezi(Ke) kuwapa simu Smartphone watoto kama kitu cha kuwabembeleza wasilie au kitu cha kuchezea.
4.Watoto chini ya 14yrs wawe chini ya Uangalizi maalum na mtoto aweze kuulizwa na mtu mzima yeyote kwamba yuko na nani, anaenda wapi na kwa ruhusa ya nani majira kuanzia saa 12 jioni. Tofauti na hapo Taarifa itolewe Kituo cha Polisi kilicho jirani au Kwa Mtendaji kijiji au Kitongoji (VEO).
5.Iwe ni kosa la jinai kwa mzazi/mlezi ikiwa mtoto wake kuonekana maeneo ya Nyumba za starehe au vilabuni au groceries muda wowote.
 
1. Watoto wawe na haki ya kuhakikishiwa ajira pindi wamalizapo masomo. Hili linawezekana na lipo ndani ya uwezo wetu kama nchi. Nchi yetu ni changa sana bado haijajengwa. Je, nani atajenga kama sio watoto wetu?

Kuna ajira nyingi sana nchi hii changamoto kubwa ni mifumo yetu na usimamizi wa mifumo yetu.

Hii itawafanya watoto wetu waone elimu ina manufaa kwao kuliko hali ilivyo sasa. Na pia itainua life standard za watoto wa Taifa letu.

2. Shule zote za umma ziwe za 'English medium'. Hili lipo ndani ya uwezo wetu kama nchi.

Kwa hali ilivyo sasa tunajenga Taifa linalogawanya watoto. Wengine wanasoma fagio na kidumu na wengine wanasoma na school bus.

Hakuna ajuaye kwa nini viongozi wetu wanashindwa kuelewa impact ya suala kubwa kama hili.

Nyerere alikuwa anawachukua wanafunzi wa ukanda mmoja na kwenda kusoma mbali huko ili wachangamane....lakini leo nyie mnawatenganisha watoto kwenye elimu.

Watoto wa nyerere walisoma na watoto wa walalahoi....leo watoto wa viongozi hawawezi kusoma kayumba wanakosoma walalahoi.

Elimu ni basic need kwa kila mtoto tena ile elimu quality.
 
Adhabu za viboko ni kudhalilisha na kuutweza utu wa mtoto nashangaa ulimwengu wa leo bado kuna watu wanaamini kwenye vipigo kama njia ya kutatua kosa.

Ingekuwa viboko/ vipigo ni njia ya kurekebisha mtoto basi Afrika hususan Tanzania ingekuwa mbali sana kiteknolojia lakini ni kinyume chake.

Watoto wamekuwa wakiadhibiwa hadi kupelekea ulemavu wa kudumu ama vifo lakini serikali haina muda kabisa juu ya kuwalinda watoto dhidi ya ukatili huu mashuleni na majumbani sijui hadi aje afe mtoto wa waziri ndiyo adhabu hizi za kikatili zifutwe.
Lengo la viboko siyo kumfanya mtoto aelewe hesabu bali kumuweka kwenye msitari anapokengeuka,kama alikua akifanya fujo wakati mwalimu anafundisha,anyukwe ili ajue wakati mwalimu anafundisha anapaswa kuwa kimya na kumfuatilia,bakora zisizidi sita
 
Wasaalam,

Tafadhali ikikupendeza soma maelekezo ya kiambatisho hapa chini SEHEMU YA PILI (b).

Kisha tafadhali tenga muda wako usome utoe maoni yako kama ilivyoelekezwa kwenye tangazo lililoambatishwa.

Natanguliza shukrani.

Source insta @bunge.tanzania

View attachment 3069439View attachment 3069440
I wish ungelikuwa makamu wakati ule. Baada ya kupata nafasi umekuwa active sana kitu ambacho wengi hawawezi
 
1. Bar na nyumba za wageni zitengwe nakuwekwa mbali na makazi ambapo watoto wanalelewa na kukua.

2. Adhabu itolewe kwa watu wazima wanaotoa lugha chafu mbele ya watoto wadogo...matusi na lugha mbaya inafanya watoto wajifunze maneni na tabia chafu zisizofaa.
 
Viboko na adhabu ziwepo ila kwa kiasi na kuzingatia utu na maadili kutokuwepo kabisa madhara yake ni makubwa.
Wewe viboko vilikusaidia nini? Hivi hizi akili za utumwa bado zingali vichwani vya Mwafrika?

Ama kweli Mwafrika sio banadamu kamili aliyekamilika bali ameishia hatua fulani tu.

Nchi zilizoendelea hazina adhabu za kikatili za viboko lakini ndiyo wagunduzi wa teknolojia mbalimbali duniani.
 
Lengo la viboko siyo kumfanya mtoto aelewe hesabu bali kumuweka kwenye msitari anapokengeuka,kama alikua akifanya fujo wakati mwalimu anafundisha,anyukwe ili ajue wakati mwalimu anafundisha anapaswa kuwa kimya na kumfuatilia,bakora zisizidi sita
Kwahiyo wewe bakora ndizo zilikufanya ukajua kusoma na kuandika?

Hivi nyie Waafrika mmelogwa na nani lakini? Kiukweli Waafrika ni binadamu walioishia njiani kwenye uumbaji ndiyo maana akili ni mgando.

Mimi nimesoma moja ya shule ambazo viboko ni marufuku na nilifaulu ufaulu wa kiwango cha juu pamoja na wenzangu.

Shule nyingi zinazoongoza kwa ufaulu mzuri na watoto wenye furaha muda wote ni zile zisizotoa adhabu za viboko mfano Shamsiye, Feza na nyingine nyingi.
 
Back
Top Bottom