Wizara ya Maendeleo inaomba Maoni yako kuhusu Muswada wa Sheria za Ulinzi wa Watoto

Wizara ya Maendeleo inaomba Maoni yako kuhusu Muswada wa Sheria za Ulinzi wa Watoto

Wasaalam,

Tafadhali ikikupendeza soma maelekezo ya kiambatisho hapa chini SEHEMU YA PILI (b).

Kisha tafadhali tenga muda wako usome utoe maoni yako kama ilivyoelekezwa kwenye tangazo lililoambatishwa.

Natanguliza shukrani.

Source insta @bunge.tanzania

View attachment 3069439View attachment 3069440
Yeyote atakaye mtendea mtoto ukatili
  1. Kingono - apigwe risasi/ akatwe uume
  2. Kipigo kinyume na sheria au kumuumiza mtoto - jela maisha
  3. 3 lugha chafu - 30 years jela
 
Kwahiyo wewe bakora ndizo zilikufanya ukajua kusoma na kuandika?

Hivi nyie Waafrika mmelogwa na nani lakini? Kiukweli Waafrika ni binadamu walioishia njiani kwenye uumbaji ndiyo maana akili ni mgando.

Mimi nimesoma moja ya shule ambazo viboko ni marufuku na nilifaulu ufaulu wa kiwango cha juu pamoja na wenzangu.

Shule nyingi zinazoongoza kwa ufaulu mzuri na watoto wenye furaha muda wote ni zile zisizotoa adhabu za viboko mfano Shamsiye, Feza na nyingine nyingi.
Mimi bila bakora ningetoka kapa
 
Wewe viboko vilikusaidia nini? Hivi hizi akili za utumwa bado zingali vichwani vya Mwafrika?

Ama kweli Mwafrika sio banadamu kamili aliyekamilika bali ameishia hatua fulani tu.

Nchi zilizoendelea hazina adhabu za kikatili za viboko lakini ndiyo wagunduzi wa teknolojia mbalimbali duniani.
Nonsensical , nchi zilizoendelea na bongo sio sawa nature ya vijana na watoto ni tofauti.
 
Wasaalam,

Tafadhali ikikupendeza soma maelekezo ya kiambatisho hapa chini SEHEMU YA PILI (b).

Kisha tafadhali tenga muda wako usome utoe maoni yako kama ilivyoelekezwa kwenye tangazo lililoambatishwa.

Natanguliza shukrani.

Source insta @bunge.tanzania

View attachment 3069439View attachment 3069440
Yani mheshimiwa hata kabla sijasoma kilichomo, waheshimisheni kwanza wazazi wa kiume katika suala zima la malezi ya mtoto. Kama ilivyo kumleta mtoto duniani ni jukumu la wawili, basi hata kama wazazi.hawa wametengana, pawepo na usawia katika malezi.
 
Waziri wangu suala la ulawiti na ubakaji watoto imekua mbaya mbaya zaidi na hii imetokana na kuwepo na mazingira tatanishi juu ya ufuatiliaji na rushwa katika taasisi za utoaji haki

Imefikia hatua mtu analawiti watoto na bado anadunda mitaani kutokana tu na sheria kupindishwa,

Nashauri ikibainika wazazi wenyewe wameyamaliza kienyeji kwa kudhania kuharibu ujirani/ undugu wote wafungwe miaka 30, idara ya upelelezi ikipewa jukumu la ufuatiliaji na kwa makusudi kabisa wakapindisha ushahidi ili tu wapate rushwa nao wapigwe 30 keshi na mtuhumiwa halisi aliyethibitika kabisa afungwe maisha,


KUBWA KABISA, serikali ihakikishe kesi zinazohusu unyanyasaji wa kijinsia hususani kwa watoto zishughulikiwe haraka sana na haki itendeke,...Muheshimiwa hali ya ulawiti watoto mitaani inatisha inatisha inatisha vibaya mno mno yani
 
Nonsensical , nchi zilizoendelea na bongo sio sawa nature ya vijana na watoto ni tofauti.
Endelea kuamini kwenye ukatili eti ndiyo njia ya kuwafunza watoto wako.

Mimi tangu niwe na watoto sijawahi kumchapa mtoto hata kwa bahati mbaya lakini chochote ninachoongea wananisikiliza kwa makini na kukifanyia kazi ipasavyo.

Watoto wenzao wanaocheza nao hapa home wamezoea vipigo kutoka kwa wazazi wao lakini ndiyo wamezidi kuwa manunda wala hawajabadilika kwa chochote.
 
Tunaomba itungwe sheria iwe ni kosa la jinai mzazi au mlezi kutompeleka mtoto shule ama kufanya njama mtoto aache shule.

Iwe ni kosa la jinai mtoto kutopatiwa mahitaji yake muhimu, yakiwemo ya shule.
Iwe ni kosa kumnyanyasa mtu anayetaka kumsaidia mtoto ambaye mzazi wake amesahau kumsaidia.
 
Wasaalam,

Tafadhali ikikupendeza soma maelekezo ya kiambatisho hapa chini SEHEMU YA PILI (b).

Kisha tafadhali tenga muda wako usome utoe maoni yako kama ilivyoelekezwa kwenye tangazo lililoambatishwa.

Natanguliza shukrani.

Source insta @bunge.tanzania

View attachment 3069439View attachment 3069440
Binafsi naomba wizara ishirikishe walimu wa ushauri na unasihi tangu ngazi za shule ya awali hadi vyuo vikuu. Walimu wapewe mafunzo yatakayowawezesha kuzungumza na jamii inayowazunguka hasa kuhusu malezi.

Wazazi/walezi wengi wako busy sana kutafuta kipato na wamesahau kabisa jukumu la malezi. Walezi pekee wanajitahidi kwa sasa ni walimu.
Na ndio maana case nyingi huanzia shuleni.

Muhimu zaidi: wizara itoe tamko la kupiga marfuki nyimbo zinazohamasisha ngono na pombe. Watoto hujifunza zaidi kwa kuona kuliko hata kufunzwa kwa maelezo mengi na maonyo yasiyoendana na uhalisia katika jamii.

Zaidi naipongeza wizara hasa waziri Dkt. Gwajima D kwa kuonesha nia na ari ya kupambana na ukatili dhidi ya watoto. Tusaidiane zaidi kwenye kuzuia kuliko kusubiri hadi watoto, jamii iaathirike.
 
Sheria ya kuzuia wazazi kuwachapa viboko ndo sheria itayosaidia kuboresha malezi.
 
Ikitokea Mwanamke kudanganya na kumbambikia Mumewe Mtoto ambaye siô wake. Mtoto ataendelea kuwa Mtoto wa huyo Mwanaume wa kambo kisheria mpaka atakapofikisha Umri wa kujitegemea. Ikiwa Mtoto akataka kwenda Kwa Babaake halisi, huyo Baba halisi itampasa atoe fidia ya Pesa Kulingana na Maisha ya kipindi husika
NAKAZIA
 
Wasaalam,

Tafadhali ikikupendeza soma maelekezo ya kiambatisho hapa chini SEHEMU YA PILI (b).

Kisha tafadhali tenga muda wako usome utoe maoni yako kama ilivyoelekezwa kwenye tangazo lililoambatishwa.

Natanguliza shukrani.

Source insta @bunge.tanzania

View attachment 3069439View attachment 3069440
Ile taasisi ya Athumani kapuyanga ifungwe kwa vitendo na sii kwa maneno,maeneo ya vichochoro vya Dar es salamu hii NGO inaonekana na mabango yake bila kificho,mfamo wa kifremu cha biashara,ninazo taarifa za uwepo wake eneo la kwamzala,karibu na shule inaitwa mackenzie hii ni chekechea.Kumbukeni ilitolewa agizo la kufungwa shughuli zake,kwa waliyofanya tabora.
 
Adhabu za viboko ni kudhalilisha na kuutweza utu wa mtoto nashangaa ulimwengu wa leo bado kuna watu wanaamini kwenye vipigo kama njia ya kutatua kosa.
...

Siungi mkono kufuta viboko, bali naunga mkono kupunguza viboko mashuleni

Kinachotokea sasa hivi tuna kopy taratibu za ulimwengu wa kwanza ambao wapo mbele yetu pengine kwa miaka 60 na kuendelea, unaweza kujiuliza wao walizuia hizo fimbo lini?

Nina mifano michache hapa; Marekani walizuia 1977, Ufaransa walizuia 2014, Australia walizuia 1985, Uingereza walizuia 1986 - unaweza kuona kabisa ni majuzi tu)

Wanao piga kelele sana kufuta viboko ni wale wazazi ambao watoto wao wanatumia mabasi ya njano ambao pengine ni 15% ya watoto wote wanaosoma ILA kwa sababu wao ndio wenye access na social media kelele zinaonekana ni nyingi. Ila ni ukweli pia hao watoto wa mabasi ya njano hata tukifuta vikobo wao hawata adhirika au hawata adhirika sana

Vijijini bado kabisa, huwezi kufuta fimbo; watoto watoro shule, wanapigana mitaani, wanaiba miwa, maembe, korosho, machungwa, mwingine leo sijui wa darasa gani kavunja kioo cha basi kwa jiwe nk nk nk unawezaje kuwarekebisha bila fimbo? hata Biblia imetuambia kuwa, tusiwanyime watoto fimbo

Kwa mtazamo wangu tukiingia huo mkenge wa kufuta fimbo; miaka 30 ijayo tutajutia na hatutaweza tena kurudi nyuma

Ifike mahala tutumie akili zetu kufikiri vitu vinavyo endana na mazingira yetu; Utafikiri wasomi wetu wanakwenda vyuoni kusomea kukopy na kupaste...kila kitu ukiuliza Msomi anakujibu wenzetu (ulaya) wanafanya hivi.... badala ya kujibu, mimi naona hivi........
 
Back
Top Bottom