Shebbydo
JF-Expert Member
- Feb 12, 2015
- 1,174
- 1,937
Habari Wana JF,
Katika website ya wizara ya viwanda na bishara, kuna kipengele ambacho huwa wanaweka taarifa za bei za mazao hasa ya vyakula. Hii huwa ni madhumuni ya kumsaidia mfanyabiashara kujua bei katika mikoa mbalimbali zipoje. Lakini katika utafiti wangu nimegundua taarifa hizi hazina ukweli, mfanyabiashara ukizifuata utaumia.
Nimefikia kulijua hili ni baada ya kufuatilia bei ya ngano Mwanza. Katika taarifa yao ya tar 5 Dec 2016, wanasema bei ya jumla ya ngano kwa kilo mia ni shilingi za Kitanzania laki moja na sabini(170,000). Jambo hili si kweli. Bei ya ngano kwa jumla, kwa mfuko wa kilo 25 ni Tsh 28,000 hadi 30,000. Kwa maana hiyo kilo mia ni Tsh 120,000, hiyo 170,000 imetoka wapi? Haya kwa bei ya rejareja ngano kilo moja ni Tsh 1,400, kilo mia kwa bei ya rejareja itakuwa ni Tsh 140,000 bado hiyo 170,000 haifiki. Hilo soko wao wamelitoa wapi? Huo ni upotoshaji, hasa wa taarifa muhimu ambazo mfanyabiashara anazihitaji.
Rai yangu kwao hawa wahusika, kama kweli wanataka kutoa taarifa za kuwasaidia Watanzania, watafute habari zenye ukweli ili watoe bei zilizopo sokoni na si kukaa ofisini na kutunga bei za kufikirika.
Katika website ya wizara ya viwanda na bishara, kuna kipengele ambacho huwa wanaweka taarifa za bei za mazao hasa ya vyakula. Hii huwa ni madhumuni ya kumsaidia mfanyabiashara kujua bei katika mikoa mbalimbali zipoje. Lakini katika utafiti wangu nimegundua taarifa hizi hazina ukweli, mfanyabiashara ukizifuata utaumia.
Nimefikia kulijua hili ni baada ya kufuatilia bei ya ngano Mwanza. Katika taarifa yao ya tar 5 Dec 2016, wanasema bei ya jumla ya ngano kwa kilo mia ni shilingi za Kitanzania laki moja na sabini(170,000). Jambo hili si kweli. Bei ya ngano kwa jumla, kwa mfuko wa kilo 25 ni Tsh 28,000 hadi 30,000. Kwa maana hiyo kilo mia ni Tsh 120,000, hiyo 170,000 imetoka wapi? Haya kwa bei ya rejareja ngano kilo moja ni Tsh 1,400, kilo mia kwa bei ya rejareja itakuwa ni Tsh 140,000 bado hiyo 170,000 haifiki. Hilo soko wao wamelitoa wapi? Huo ni upotoshaji, hasa wa taarifa muhimu ambazo mfanyabiashara anazihitaji.
Rai yangu kwao hawa wahusika, kama kweli wanataka kutoa taarifa za kuwasaidia Watanzania, watafute habari zenye ukweli ili watoe bei zilizopo sokoni na si kukaa ofisini na kutunga bei za kufikirika.