kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 13,778
- 14,214
Mabilioni na mabilioni ya fedha za wananchi zinaibiwa kila siku na wafanyabiashara kwa njia ya Mizani zisizoweza kupima kile kinachotakiwa kupima. Mara zote Mizani yetu inapima pungufu ya kile mteja anachonunua na kupima zaidi kile mfanyabiasha anachotaka kununua kwa mwananchi.
Hatuwezi kuwa makini kupima makontena ya mchanga wa dhahabu kama tunashindwa kupima kwa usahihi kilo moja ya nyama anayouziwa mwananchi.
Maduka mengi mitaani yanatumia mizani za mawe, beam balance ambazo ama zimechezewa au zimeharibika.
Nyama mchanganyiko ni wizi mkubwa kwa wananchi, kwakuwa mwananchi hajui anauziwa nyama kiasi gani na mifupa kiasi gani. Ukimtuma mtoto mdogo butchani ndo kBisA atauziwa mifupa mingi kuliko nyama.
Sheria ya kupiga marufuku kuuza nyama mchanganyiko itungwe ili mlaji apate uhalisia wa kile anachokinunua kwa kilo. Kama anataka mifupa anunue mifupa, kama anataka nyama anunue nyama na kama anataka mchanganyiko aende akachanganye mwenyewe nyumbani kwake baada ya kununua.
Wafanyabiashara woote Lazima watumie digital mizani katika kuuza na kununua bidhaa.
Hili nalo linahitaji mpaka Rais Magufuli aseme?
Hatuwezi kuwa makini kupima makontena ya mchanga wa dhahabu kama tunashindwa kupima kwa usahihi kilo moja ya nyama anayouziwa mwananchi.
Maduka mengi mitaani yanatumia mizani za mawe, beam balance ambazo ama zimechezewa au zimeharibika.
Nyama mchanganyiko ni wizi mkubwa kwa wananchi, kwakuwa mwananchi hajui anauziwa nyama kiasi gani na mifupa kiasi gani. Ukimtuma mtoto mdogo butchani ndo kBisA atauziwa mifupa mingi kuliko nyama.
Sheria ya kupiga marufuku kuuza nyama mchanganyiko itungwe ili mlaji apate uhalisia wa kile anachokinunua kwa kilo. Kama anataka mifupa anunue mifupa, kama anataka nyama anunue nyama na kama anataka mchanganyiko aende akachanganye mwenyewe nyumbani kwake baada ya kununua.
Wafanyabiashara woote Lazima watumie digital mizani katika kuuza na kununua bidhaa.
Hili nalo linahitaji mpaka Rais Magufuli aseme?