Wizi mkubwa kwa njia ya Mizani kwenye Butcher

Wizi mkubwa kwa njia ya Mizani kwenye Butcher

Lengo la mteja ni kununua nyama sio mifupa, sasa hana uhakika kwenye hiyo nusu kilo aliyouziwa kapata nyama kiasi gani na mifupa kiasi gani, shombo tu, watoto wanaramba mifupa.
Nunua steki
 
Nunua steki
mabutcher mengi hawataki kuuza steki, wanakwambia mifuta tutaipeleka wapi? Nadhani kuna haja ya kujenga viwanda vinavyotumia mifupa kama malighafi
 
Mkuu.. Ng'ombe hasimami kwa msaada wa upepo, anatumia mifupa..

Mbona kuna butcher zinasema kabisa kuwa ukitaka stake tupu kuna bei yake na ukitaka mchanganyiko kuna bei yake.

Ni wewe tuu na suala la kuchagua
 
hoja nzuri mno kuhusu mada hii,ila umefika wakati nasi tusogee mbele ,turuhusu hizi super markets zetu kama Game or shoprite ziwe zinauza nyama ambayo imeshapimwa na kufungwa vizuri na itakuwa inaonyesha uzito wake na bei yake,hii itasaidia kuongeza ushindani na kuwafanya hawa wafanya biashara ya mabucha nao kuboresha huduma zao.
Shoppers Plaza Mikocheni wako vizuri kabisa, wameshafika huko unakokutamani mimi na familia yangu tunanunua nyama (sio mifupa) kule, na ukitaka kiungo kama mkia, chicken wings, breasts, figo, nk nenda kule bhana ukajionee mwenyewe.
 
Mkuu.. Ng'ombe hasimami kwa msaada wa upepo, anatumia mifupa..

Mbona kuna butcher zinasema kabisa kuwa ukitaka stake tupu kuna bei yake na ukitaka mchanganyiko kuna bei yake.

Ni wewe tuu na suala la kuchagua
Mchanganyiko wa aina gani, nyama na mifupa au mifupa na nyama? mtume mtoto au house girl uone atakuletea mchanganuiko wa aina gani
 
mabutcher mengi hawataki kuuza steki, wanakwambia mifuta tutaipeleka wapi? Nadhani kuna haja ya kujenga viwanda vinavyotumia mifupa kama malighafi
Huwa ina bei y@ juu zaidi
 
Mkuu, naomba ufafanue zaidi hapo, ninapoingia filling station, nikakuta kwenye dispenser inasoma 2000, kwamba mteja aliyetoka ndo aliwekewa mafuta ya pesa hiyo, mimi nikitaka aweke ya 15000 na nikaona pale kwenye display ameandika 15000 na litres ikaanzia 0, bado nitakuwa nimepigwa???
Hapo unakuwa umepigwa inatakiwa upande wa hela pale afutee aanze na zero
 
Lengo la mteja ni kununua nyama sio mifupa, sasa hana uhakika kwenye hiyo nusu kilo aliyouziwa kapata nyama kiasi gani na mifupa kiasi gani, shombo tu, watoto wanaramba mifupa.
Si wanatuzuga nao wana bundle la steak na mixer
 
Hasa hizi mizani za digital,wanazichezea sana,bora za mawe
 
Hasa hizi mizani za digital,wanazichezea sana,bora za mawe
Siku hizi nikifikani kitu cha kwanza kabla sijaagiza ninachotaka kununua nakimbilia kuondoa mawe kwenye mizani, nikifika petrol station nashuka kabisa kwenye gari na kuangalia pump inaanzaje na kuishiaje
 
Siku hizi nikifikani kitu cha kwanza kabla sijaagiza ninachotaka kununua nakimbilia kuondoa mawe kwenye mizani, nikifika petrol station nashuka kabisa kwenye gari na kuangalia pump inaanzaje na kuishiaje
Kavulata, kwani si inawezekana pia hata pampu ikianza 0 mteja kupunjwa mafuta.
Au mzani kuwa balance lakini mteja kupunjwa?
 
Kavulata, kwani si inawezekana pia hata pampu ikianza 0 mteja kupunjwa mafuta.
Au mzani kuwa balance lakini mteja kupunjwa?
Ikoje hiyo mkuu, hebu tonya wengine
 
Kuna haja serikali itunge sheria kuzua uuzaji wa nyama ya ngombe pamoja na mifupa take kama VP nyama iuzwe peke take na mifupa peke take.

Nijuavyo mthibiti was vipimo huwa ni wakala was vipimo na wanafanya ukaguzi wao kila mwaka lkn kwenye mabucha watembeleaga mara kwa mara, mbinu ingine wanayotumia ni kugandisha nyama ya mafuta kwenye sahani ya mzani ambayo haitoki na pia na kufunga Uzi kwenye upande mwingine na kuukanyagia chini ili mzani uonekane umebalance
 
Mabilioni na mabilioni ya fedha za wananchi zinaibiwa kila siku na wafanyabiashara kwa njia ya Mizani zisizoweza kupima kile kinachotakiwa kupima. Mara zote Mizani yetu inapima pungufu ya kile mteja anachonunua na kupima zaidi kile mfanyabiasha anachotaka kununua kwa mwananchi.
Hatuwezi kuwa makini kupima makontena ya mchanga wa dhahabu kama tunashindwa kupima kwa usahihi kilo moja ya nyama anayouziwa mwananchi.

Maduka mengi mitaani yanatumia mizani za mawe, beam balance ambazo ama zimechezewa au zimeharibika.

Nyama mchanganyiko ni wizi mkubwa kwa wananchi, kwakuwa mwananchi hajui anauziwa nyama kiasi gani na mifupa kiasi gani. Ukimtuma mtoto mdogo butchani ndo kBisA atauziwa mifupa mingi kuliko nyama.

Sheria ya kupiga marufuku kuuza nyama mchanganyiko itungwe ili mlaji apate uhalisia wa kile anachokinunua kwa kilo. Kama anataka mifupa anunue mifupa, kama anataka nyama anunue nyama na kama anataka mchanganyiko aende akachanganye mwenyewe nyumbani kwake baada ya kununua.
Wafanyabiashara woote Lazima watumie digital mizani katika kuuza na kununua bidhaa.

Hili nalo linahitaji mpaka Rais Magufuli aseme?
Sa tunaibiwaje..nlitegemea utatililika madini ya maana..kumbe maoni tu.
 
Hii iko hv mfano bodaboda kaja kaweka mafuta ya 2000 we unaenda na gari unatak mafuta ya elf kumi na 5 pale utakuta ubao unasoma elf 2 aliyotok kuweka kweny bodaboda hata futa ile elf mbili ataanza kuandka kiwango cha hela yako ya mafuta elf 15 hapo kwenye hesabu itasomeka ameweka mafuta ya elf kumi tatu yaan inakua kama umenunua mafuta ya elf mbili then ukanunua ya elf 13 ndo ikatimia elf kumi na 5 so elf mbili anatia mfukoni
Inatakiwa utakapoenda sheli ukikuta mteja katok waambie waanze na sifuri...
Hapo kuanzaje Na sifuri...?
 
Wauza nyama wana njia kadhaa za kukuibia. Mbali ya kukujazia mifupa, hawa jamaa wanaiba kwa kukupunja uzito. Kwenye uzito njia tatu ambazo nilishawabaini wauzaji na kutaka kuwaweka ndani
1. Wakati wanakupimia nyama, kwenye ile bakuli huwa kunakuwa na nyama mbovu au mfupa. Na muda wote hawa hawatoi jiwe kwenye mzani. Wanakujazia nyama kwenye chombo wakati kulikuwa na nyama mbovu. Kwa wale hawana mashine za kukatia, pale kwenye gogo Kunakuwa na nyama mbovu au mfupa, wanakusanya na nyama ulioiona nzuri bila kujua.
2. Pale katika ya mzani kunakuwa na kibati akiwa anapima anasogeza na kidole, mzani unakula kwako.
3. Yale mawe hayajafika uzito unao hitajika. Kunasiku walijichanganya,,walinipimia nyama kg 2, wakati anahangaika kutafuta chenji nikaona jiwe lingine la kg 2 lipo chini. Nikalichukua nikaweka ndani ya bakuli la kupimia (nina maana nikayapima mawe yenyewe). . Duuh ziito kuliko alilotumia kunipimia. Aliporudi akakuta hilo zoezi jamaa akakimbia, mwenzake akaja kunituliza na kunipa chenji yangu na rushwa ya nyama ya kutosha.

Ushauri: nunua nyama kwenye maduka ya nyama yenye mizani ya kielektroniki
 
Wauza nyama wana njia kadhaa za kukuibia. Mbali ya kukujazia mifupa, hawa jamaa wanaiba kwa kukupunja uzito. Kwenye uzito njia tatu ambazo nilishawabaini wauzaji na kutaka kuwaweka ndani
1. Wakati wanakupimia nyama, kwenye ile bakuli huwa kunakuwa na nyama mbovu au mfupa. Na muda wote hawa hawatoi jiwe kwenye mzani. Wanakujazia nyama kwenye chombo wakati kulikuwa na nyama mbovu. Kwa wale hawana mashine za kukatia, pale kwenye gogo Kunakuwa na nyama mbovu au mfupa, wanakusanya na nyama ulioiona nzuri bila kujua.
2. Pale katika ya mzani kunakuwa na kibati akiwa anapima anasogeza na kidole, mzani unakula kwako.
3. Yale mawe hayajafika uzito unao hitajika. Kunasiku walijichanganya,,walinipimia nyama kg 2, wakati anahangaika kutafuta chenji nikaona jiwe lingine la kg 2 lipo chini. Nikalichukua nikaweka ndani ya bakuli la kupimia (nina maana nikayapima mawe yenyewe). . Duuh ziito kuliko alilotumia kunipimia. Aliporudi akakuta hilo zoezi jamaa akakimbia, mwenzake akaja kunituliza na kunipa chenji yangu na rushwa ya nyama ya kutosha.

Ushauri: nunua nyama kwenye maduka ya nyama yenye mizani ya kielektronia
Tunahangaika kupima inayotoka na kwenda nje ya Tanzania lakini tunasahau mizingo inayokwenda kwa wananchi wetu wa kawaida kabisa.
 
Back
Top Bottom