rodrick alexander
JF-Expert Member
- Feb 12, 2012
- 16,784
- 23,312
Mechi hii iliyofanyika Jumamosi ilikuwa na matukio mengi ya uwanjani na nje ya uwanja lakini wakati washabiki wengi wakijikita kwenye mjadala wa penati ya Kagere kama ni halali au siyo halali na wengine kujikita kumjadili Aishi Manula juu ya magoli yaliyofungwa huku nje kabla ya kuingia kulikuwa na mtafaruku mkubwa kwa waliokuwa wakiingia baada ya mashine za Selcom kukataa kuzitambua tiketi zao kwa kushindwa kusomeka kwenye mashine.
Cha ajabu watu wamenunua tiketi zaidi ya moja sehemu moja nyingine zinasomeka huku nyingine hazisomi kama sio busara za kuamua watu wote wenye tiketi waingie bila shaka kungetokea maafa makubwa kwani hakuna mtu ambaye angekubali azuiliwe kuingia uwanjani na hali amelipia pesa ili aone mpira.
Kwa haraka haraka unaweza kuchukulia ni tatizo la kimfumo lakini ukweli ule ni wizi ambao ulipangwa kistadi kwa kuiibia mamlaka ya mapato na club kwa kushirikiana na watendaji wa club na ndiyo maana labda mpaka leo wamekuwa na kigugumizi cha kutangaza mapato yaliyopatikana.
Cha ajabu watu wamenunua tiketi zaidi ya moja sehemu moja nyingine zinasomeka huku nyingine hazisomi kama sio busara za kuamua watu wote wenye tiketi waingie bila shaka kungetokea maafa makubwa kwani hakuna mtu ambaye angekubali azuiliwe kuingia uwanjani na hali amelipia pesa ili aone mpira.
Kwa haraka haraka unaweza kuchukulia ni tatizo la kimfumo lakini ukweli ule ni wizi ambao ulipangwa kistadi kwa kuiibia mamlaka ya mapato na club kwa kushirikiana na watendaji wa club na ndiyo maana labda mpaka leo wamekuwa na kigugumizi cha kutangaza mapato yaliyopatikana.