Wizi na ufisadi unaonaofanywa na dstv. Serikali mtusaidie wanyonge kwa kuondoa ukiritimba.

Wizi na ufisadi unaonaofanywa na dstv. Serikali mtusaidie wanyonge kwa kuondoa ukiritimba.

UDENYE

JF-Expert Member
Joined
Mar 17, 2016
Posts
318
Reaction score
201
Wadau kwa mara nyengine tena jana tarehe mosi ya mwezi June 2024, kampuni ya DSTV inayomiliki haki ya kipekee ya kuonyesha matangazo ya moja ya mashindano ya ligi barani ulaya ,na khususan Uingereza na ligi ya mabingwa wa ulaya, wamefanya tena wizi wao dhidi ya walala hoi wa Tanganyika na Zenj.

Mtanange wa fainali baina ya magwiji kutoka Madrid na Dortmund ukiwa unaendelea, kati kati ya sherehe, wadau hao kwa makusudi waliamua kukata matangazo hayo kwenye vin'gamuzi kadhaa bila kujali maokoto ambayo washakusanya kama malipo ya vinga'amuzi hivyo wala kujali kuwa muda wa maongezi uliosalia wa wananzego. Kana kwamba haitoshi wajuba hao walipopigiwa simu na wadau kadhaa wa mabanda ya kuonyesha burudani hiyo ya kandanda walitowa majibu mepesi ya kiwango cha huduma katika ofisi za sirikali.

Baadhi ya majibu nayanukulu hapa "Huu sasa hivi sio muda wa kazi hivyo mtutafute Jumatatu ya tarehe 3 mwezi huu",Mwisho wa kunukulu,

Sasa kwa niaba ya kina ujugu na kwa niaba ya watanganyika na wazenj wanaolazimika kutumia huduma hiyo mbovu kwa miaka kadhaa sasa, tunaomba Mama Samiya Raisi wetu msikivu aingilie kati na ikiwezekana waziri muhusika wa tasnia hiyo ajambishwe kidogo ili ashughulikie kero hii ya muda mrefu sasa. kama vipi wananzengo wapewe ruksa kujipachikia madishi yao ya magumashi kunasa mubashara mitanange hiyo, kuondokana na ugaigai wa hawa makaburu.

Kwa wadau kama kina ujugu, mechi kama hizi za fainali ndo wanazofunga hesabu na ada za watoto, pango za kumbi na nyumba zao ndio zinapopatikana, achilia mbali wadau waliopatwa na taharuki ya kukatishwa kwa matangazo hayo ghafla tena bila sababu za msingi kama umeme wa Tanesco.
Kwa taarifa za ndaaani zilizopo ni kuwa wajuba hao wa DSTV ambao hutumia mbinu hiyo hata kwenye zile mechi za dabi na magiant ya soka huko Ungereza kujiongezea kipato cha haraka cha Dhulma hasa kutoka kwa wale wadau wasiopenda ngonjera.

Chonde chonde wizara husika tunaomba ukiritimba huu mtuondelee, leteni kampuni zaidi ya mbili za kurusha matangazo ya soka mibashara, ili kuleta ushindani na kuboresha huduma, ama mruhusu vishoka watupachikie midishi ya Arabuni tujinafasi mubashara kutoka duniani.

DSTv Wameshashindwa zamani wamebaki na vioja badala ya hoja.

Naomba kuwasilisha

Mwananzego kutoka pande za Vikindu.
 
Wadau kwa mara nyengine tena jana tarehe mosi ya mwezi June 2024, kampuni ya DSTV inayomiliki haki ya kipekee ya kuonyesha matangazo ya moja ya mashindano ya ligi barani ulaya ,na khususan Uingereza na ligi ya mabingwa wa ulaya, wamefanya tena wizi wao dhidi ya walala hoi wa Tanganyika na Zenj.
Mtanange wa fainali baina ya magwiji kutoka Madrid na Dortmund ukiwa unaendelea, kati kati ya sherehe, wadau hao kwa makusudi waliamua kukata matangazo hayo kwenye vin'gamuzi kadhaa bila kujali maokoto ambayo washakusanya kama malipo ya vinga'amuzi hivyo wala kujali kuwa muda wa maongezi uliosalia wa wananzego. Kana kwamba haitoshi wajuba hao walipopigiwa simu na wadau kadhaa wa mabanda ya kuonyesha burudani hiyo ya kandanda walitowa majibu mepesi ya kiwango cha huduma katika ofisi za sirikali.
Baadhi ya majibu nayanukulu hapa "Huu sasa hivi sio muda wa kazi hivyo mtutafute Jumatatu ya tarehe 3 mwezi huu",Mwisho wa kunukulu,
Sasa kwa niaba ya kina ujugu na kwa niaba ya watanganyika na wazenj wanaolazimika kutumia huduma hiyo mbovu kwa miaka kadhaa sasa, tunaomba Mama Samiya Raisi wetu msikivu aingilie kati na ikiwezekana waziri muhusika wa tasnia hiyo ajambishwe kidogo ili ashughulikie kero hii ya muda mrefu sasa. kama vipi wananzengo wapewe ruksa kujipachikia madishi yao ya magumashi kunasa mubashara mitanange hiyo, kuondokana na ugaigai wa hawa makaburu.
Kwa wadau kama kina ujugu, mechi kama hizi za fainali ndo wanazofunga hesabu na ada za watoto, pango za kumbi na nyumba zao ndio zinapopatikana, achilia mbali wadau waliopatwa na taharuki ya kukatishwa kwa matangazo hayo ghafla tena bila sababu za msingi kama umeme wa Tanesco.
Kwa taarifa za ndaaani zilizopo ni kuwa wajuba hao wa DSTV ambao hutumia mbinu hiyo hata kwenye zile mechi za dabi na magiant ya soka huko Ungereza kujiongezea kipato cha haraka cha Dhulma hasa kutoka kwa wale wadau wasiopenda ngonjera.
Chonde chonde wizara husika tunaomba ukiritimba huu mtuondelee, leteni kampuni zaidi ya mbili za kurusha matangazo ya soka mibashara, ili kuleta ushindani na kuboresha huduma, ama mruhusu vishoka watupachikie midishi ya Arabuni tujinafasi mubashara kutoka duniani.
DSTv Wameshashindwa zamani wamebaki na vioja badala ya hoja.
Naomba kuwasilisha
Mwananzego kutoka pande za Vikindu.
Kwakweli DSTV wanakera sana. Na sasa hivi hii tabia yao ya kuonesha mpira kwenye Channel mbovu isiyo ya kimpira TV E nayo imekomaa.
Wanakera
 
Fateni utaratibu , kurusha hayo Matangazo Inacost billion of money, lipia kifurushi
 
Mkuu starehe ni gharama. Yani ulipie Tsh 10,000/= au Tsh 20,000/= kwa mwezi halafu utulie kwenye sofa lako huku ukicheki mechi ya Real Madrid vs Dortmund, upo serious?. Mimi nililipia kifurushi Cha compact Tsh 64,000/= nimekula hiyo mechi mwanzo mwisho bila zengwe. Hii Dunia jua kuwa usipokuwa na hela hakuna mtu atakuonea huruma.
 
Mkuu starehe ni gharama. Yani ulipie Tsh 10,000/= au Tsh 20,000/= kwa mwezi halafu utulie kwenye sofa lako huku ukicheki mechi ya Real Madrid vs Dortmund, upo serious?. Mimi nililipia kifurushi Cha compact Tsh 64,000/= nimekula hiyo mechi mwanzo mwisho bila zengwe. Hii Dunia jua kuwa usipokuwa na hela hakuna mtu atakuonea huruma.
Asante sana mkuu wa kazi.
Kwa mwezi binafsi nalipa 189,000. Na nilipoangalia salio kunako akaunti leo hii asubuhi lilikuwa linasoma 90,000 pesa ya kitanganyika na Zenj.
Hata hivyo wamerudishwa huduma hiyo leo mchana bila kushurutishwa.
Mechi muhimu ya kuingiza takriban laki 5 mpaka 7 wamenitia hasara.
Lakini ndio mambo ya kitanzania
 
Mimi sijaelewa hapa..ulilipia kifurushi halafu wakakata matangazo au imekuaje?
Kaka mkubwa nalipia kila tarehe 10 ya mwezi 189,000. Sasa jana kama ilivyo kawaida yao Mdstv walikata matangazo katikati ya mechi na king'amuzi kilikuwa kinasoma salio limekata.
Nilipowapigia ndio nikapata majibu hayo ya shombo.
Lakini kwa namna ya mazingaombwe leo walirudisha matangazo mchana na king'amuzi kinasoma salio ni 90,000 pesa ya kitanganyika na zenj.
Kwa uzoefu wangu wa kutumia huduma hii tangu mwaka 2003, mambo yanayofanan na haya yamekuwa mengi sana.
 
Back
Top Bottom