Wizi wa Bank ya CRDB Part II

Status
Not open for further replies.
Nahisi watu wamegoma kuekewa kwan wanadhan we unahamisisha huduma ziwe za buree.
Mweee wa Tz ni wa bishi kuekewaaa ingawa wanaelewaaa
 
Ila kweli charge zimekuwa too much. Ukitoa million moja kwenye atm unakatwa 2,100. Naona wanataka kurudisha foleni ndani tu hawa.
 
Kumbe wizi wa CRDB part II ni Kimei must go

you sound like a disgraced former CRDB employee


Mleta uzi huu juu ya charges za CRDB ana hoja nzito ambayo hata BOT wanatakiwa kuifanyia kazi. Benki nyingi hapa Tanzania na hasa za kibongo hazifanyi kazi za kibenki kwa ufanisi na hivyo faida wanayoipata kila mwaka inatokana na TOZO[ charges] ambazo nyingine kusema kweli hazina maana; kwa nmfano charges za kutoa pesa kutoka kwenye akaunti ya mteja ni unyonyaji wa dhahili kabisa ukifahamu kuwa wateja tunalipa ledger fees kila mwezi!!! Sioni mantiki ya mteja kulipa tozo kwa kutoa pesa yake benki!!
 
Mtoa hoja una hoja japo watu wengi hawajakuelewa. Tujiulize hivi ni kwa nini benki zetu mfano CRDB hazijitanui ktk nchi za SADC na EAC. huenda ni Sera au sheria au kukosa uthubutu. Suala la kuhama benki ni ushauri mzuri Lakini hauna mantiki. Kwenye jamii lazima baadhi ya watu wajigeuze reli ili treni ipite. Huko kwenye nchi za dunia ya kwanza wateja huwa wanajihami kwa kuanzisha vyama Imara ili kulinda maslahi yao. Mfano chama cha wateja wa taasisi za fedha, chama cha wavuta sigara n.k. Waingereza husema "for every effect there is a cause"
 
Mleta mada uko sahihi sasa hivi mabenki yanatoza gharama ambazo hazieleweki wala hazina maelezo maalumu.

Tena benk nyingi zinamakato yanayoelekeana , Sema watanzania wengi sio wafuatiliaji wa benki statement.

Ila siku ukiamua kufuatilia makato ya ki benk unaweza kuondoka na Pesa yako ukaenda kuichimbia nyumbani.

Mimi sio mteja wa CRDB, ila nina account benk tatu tofauti.

Watanzania tujenge mazoea ya kuomba benk statement walau kila mwezi kama huwezi dai hata baada ya miezi mitatu.

Naamini wengi mtakuja kuungana na mleta mada, uendeshaji wa benk Tanzania Hauna tofauti na mitandao ya simu.
 

CRDB hawafai kabisa mie nimetoka kabisa. Nimefunga akaunti yangu hivi majuzi japo walinibembeleza sana kwa nini unachota hela na kufunga akaunti nikawadanganya naenda kusoma Masters Norway. Walikoamaa kwamba hata huko nje naweza tumia huduma zao kwa kutumia viza yangu nikawaambia NO. Naenda kuanza mambo yangu yote upya wakaufyata nikachomao changu na kusepaaaaaaaa. kiukweli charges zao zipo juu sana. hakuna benk yoyote ya kawaida inacharrge sh 1500 ya kuendesha akaunti kwa mwezi zaidi ya CRDB
 

nakubakiana na wewe
 

Ulikuwa na sh. ngapi mkuu kama hiyo 1500 unaiona kubwa.
 
Equity bank hawana charges za kutunza hela
 
Yaaani Kuna Siku Nilidata Mwenyewe
nilideposit 50,000 kwa simu mwisho wa mwezi nikaenda kuangalia nikakutana na 11,000 nikaomba bank statement baada ya hapo kilichofuatia nikaenda kufungua account bank nyingine.

Pesa ya kwangu halafu ninyanyasike mwenyewe, aaaaarrrrrrrrrrg akuuu siwezi kwakweli
 
...0 nikaenda kuangalia nikakutana na 11000 nikaomba bank statement baada ya hapo kilichofuatia nikaenda kufungua account bank nyingine
Hongera sana kaka, mfumo wa soko huria unalengo la kuchochea ushindani ili upatikane unafuu kwa wateja/walaji.

Kwa kiasi kikubwa huduma za benki zetu nyingi hasa zile ambazo tunazimiliki wenyewe(watz) na kwenye menejimenti tupo wenyewe zinakuwa na uendeshaji wenye kukwaza wateja.

Jambo la msingi ni kuhakikisha tunaishi kwa ku-reason
 
CRDB,
Afisa Mahusiano wa CRDB/ Customer Manager,
Hakikisha unachukua hizo hoja na kuziwasilisha kwenye vikao vya Management, myafanyie kazi na kuonyesha kujali hasa mnapopewa dukuduku kama hizi, hata kama zingine siyo sawa lakini kiujumla kuna wachangiaji wameonyesha kuumizwa na makato yenu.

Mimi ni Mteja wenu tena mwenye Account 5, Ya Co. na za binafsi na ni Premium Member, Nimeona makato yenu ni makubwa ukilinganisha na uhalisia wenyewe, Kukua kwenu kutategemea mnajisahihisha vipi kwenye makosa mnayoambiwa au mnayoyagundua wenyewe.

Kwa sisi ambao hatujasomea Accounting & Finance, we look blindly on charges..kwahiyo ni vizuri mtutendee haki kwa kuorodhesha charges zenu zote kwenye vipeperushi na kwenye website yenu ili itupe picha halisi tunapofanya transaction zetu tunakatwa kiasi gani..Kwa mfano Premium member tunaambiwa tu kwa mdomo utakatwa 17,000 kwa mwezi, lakini utakuta unakatwa 22,300 kwa mwezi, kwanini msiyaweke wazi hayo kwenye vipeperushi vyenu.

Ni kweli bila ubishi mnahudumia wateja vizuri lakini muwe wepesi wa kujibu hoja kama hizi tena kwa uwazi.

Msilazimishe wateja waanze kufikiri kuhamia bank nyingine kwa mamabo ambayo yako ndani ya uwezo wenu, Yafanyieni kazi na kama hayana majibu kwenye Management yapelekeni kwenye Bodi na Kwenye Vikao vya Wanahisa.

Ndaga.
 
Haiwezekani, CRDB wanasema kila mwaka wanapata faida in billions of money kumbe ni kuwakata wateja wao charges tena za kutoa pesa kwenye ATMs. Wezi wakubwa hawa.
Natoa Hoja!
ATM wamekodi ...! I Guess.
 
Mkuu

Maajabu Haya ya wizi ni Bongo tu, UKi withdraw unachajiwa, wakati nchi za we zetu ni free, unless uchange atm current.
 
Aisee kwahiyo yjayo hayafurahishi kabisa humo CRDB! Nmefungua account mpya juzi kwao ina maana pesa zangu zitakatwa bila sababu ya msingi
 
Ukitosha watandike nyundo Vodacom , vifurushi vya chuo wanawabana mno watu wa chini.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…