Wizi wa vifaa vya ujenzi, ishawahi kukutokea?

Wizi wa vifaa vya ujenzi, ishawahi kukutokea?

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Kuna kipindi nyumbani tulikuwa tunajenga nyumba ya familia, Ikaanza kila tukinunua sementi unakuta mifuko inapungua, kumbe kibarua akichanganya mchanga na sementi, anapakia mchanganyiko kwenye mifuko anaifukia chini kisha usiku anaibeba anaenda kuwauzia watu.

Sasa siku moja wakati akiwa kashafukia mfuko wa mchanga wenye sementi chini mvua ikanyesha, maji yakaondoa ule mchanga wa juu ambao ulikuwa umefunika mfuko mfuko ukaanza kuonekana, mmoja ya ndugu akauona mfuko akaufata kuutoa kwenye kishimo ndio kugundua ni mchanga wenye sementi.

Usipokuwa makini kwenye usimamizi mafundi wanakupiga mpaka utajuta.

kkoU-aGf_400x400.jpg
 
Sijaelewa, yani mchanga wenye sement anauza vipi?
 
Nini kifanyike kukomesha hili.

Kujua mfuko mmoja wa Sementi unapiga hatua fulani kwenye kujenga inaweza kusaidia?
 
Nini kifanyike kukomesha hili.

Kujua mfuko mmoja wa Sementi unapiga hatua fulani kwenye kujenga inaweza kusaidia?

Tofali 300 inajengwa kwa mifuko 4 ya sementi,ikizidi hapo pigana hadi ufe
 
Back
Top Bottom