HIMARS
JF-Expert Member
- Jan 23, 2012
- 70,791
- 98,334
Mie kuna mtu wangu ni mpenzi sana wa Brazil, basi mechi inaanza akanitumia text kufurahia game na kudai ushindi ni kama kawa nami nikafanya hivyo baada ya goli la tatu nikamtumia text kumwambia sielewi nini kinaendelea hakujibu, halftime nikamtumia text kimya nikaamua kumpigia simu kimya, hii si kawaida yake nikaanza kuingiwa na wasi wasi mpira ulivyoisha nikampigia simu kimya. Ndiyo nimempata sasa hivi anadai baada ya goli la nne akaamua kulala, kaamka kakuta text messages 200 zikimpa pole kwa kipigo, na missed calls 120. Nafurahi kwamba yuko poa kabisa.
Mie kiukweli baada ya magoli mengi ndani ya dakika chache niliona kabisa its game over sina sababu ya kujiuliza why, kulia au kuhuzunika. Nikatulia zangu maana usingizi ulikuwa hauji kabisa
