Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sio 2 mkuu,inabidi ziwe 3 kabisa hapa namaanisha Egypt, Morocco na hawa Algeria. Hlf hizo nafasi mbili zilizobaki moja iwe ya Ghana ingawa sometimes nao wanakera but at least. Then nafasi 1 iliyobaki ndo wangine waigombee. Hapo nafikiri akili zitakaa sawa
Jamaa mwishoni walikomaa wakarudisha goli 2 na Algeria wakaongeza 1, kidogo warudishe yoteFirst Round,.
Algeria 3
Korea O
GOD Bless Algeria GOD Bless Africa.
Kwani Wahindi, wajapan, wakorea hawatoki bara moja?Kwani hawa jamaa ni waafrika au waarabu? Algerians are Arabs not Africans!
Hivi mnadiriki kweli kulinganisha Ghana na Algeria!!!? Ghana ni level za juu sana kinachowatokea ni matokeo ya kisoka tu. Algeria hawana kitu jana wamekutana na vibonde hivyo mnahisi kama wako vizur.
Tuna haki ya kusema hivyo but Korea hana mpira wa kutiisha angekutana na wa-Mexico saiz tungekuwa tunaongea vingine.acha tu watufariji.
Ngoja leo Waafrika tuanze na Brazil ndiyo wataamini tunaweza....hahahahahaaa....umdhaniaye ndiye, siye!
hata wangekutana na mexico ingekuwa sawa tu. mpira wa ALGERIA mzuri sana, spidi, usahihi wa pasi zao na malengo mazuri..:hail:
USA beats or ties Germany: USA
Advances
USA loses and Portugal ties Ghana: USA
Advances
USA loses and Portugal beats Ghana by
less than 4 (very likely): USA Advances
USA loses and Ghana beats Portugal by
1: USA Advances
USA loses and Ghana beats Portugal by
more than 1: Ghana advances
This is all assuming that if the USA loses
by 1. If we lose by more, mark the goal
differentials down 1 as well (so Portugal
beats Ghana by 3 if we lose by 2, etc.)
Waimba vigodoro bana.......Gerrard na Hodgson ni wapuuzi tu, wanatafuta namna ya kujipunguzia lawama kwa kutolewa mapema kwenye World Cup, tena kama Gerrard angekaa kimya tu maana magoli yote ya Uruguay yalipitia kwake, la ushindi akitoa 'assist to his pal'
Cha muhimu si kumlaumu Redknapp kwa kusema the obvious, ila kujua kwanini waingereza hasa damu changa hawana morali wa kuichezea nchi yao? mbona hata Callagher kwenye kitabu chake alisema alikua anapenda sana kuichezea Liverpool kuliko England, kwanini wasianze na huyo kama si unafiki tu.
Itakuwaje ikiwa Cameron ataifunga Brazil kisha mexico na croatia wakatoka suluhu ya magoli mengi?...
Na mara nyingi huwa anafungisha magoli ya ajabu ajabu, hata juzi goi la pili la Uruguay alipiga kichwa acha ajabu ajabu wakati anaokoa mpira kuelekea golini kwake na Uruguay kunasa mpira na kufunga kirahisi.....WAINGEREZA WAMEJIUA WENYEWE.
1. wakati ligi kuu inaendelea vyombo vingi vya habari vya UINGEREZA(mfano Daily Mail) vilikuwa vinasema kwamba LIVERPOOL FC ikichukua ubingwa ni faida kwa timu ya taifa. Wakaanza mkakati wa kuzichukia timu nyingine na kuandika habari nyingi za LIVERPOOL na wachezaji wake. Ikumbukwe LIVERPOOL FC ndio timu yenye wachezaji wengi kwenye kikosi cha kwanza cha timu ya taifa ya UINGEREZA.
2. Waingereza waliwapuuza ASHLEY COLE na TERRY na hata kipenzi chao WAYNE ROONEY.
3. Kabla mashindano hayajaanza kocha mkuu alitaja hadharani mbinu zake, kwa kusema DAN STURRIDGE ndo mshambuliaji wake # 1, Wayne Rooney alilalamika kiasi fulani lakini akatulia.
4. Waingereza waliacha kutumia wachezaji wabunifu; kwenye sehemu ya kiungo. Berckley na Wilshere.Badala yake kocha akapendelea zaidi HENDERSON anayepiga pasi za pembeni tu.
5. Muunganiko wa Garry Cahill na Jagielka haukuwa mzuri; walipaswa kuutafutia dawa mapema. Garry Cahill ni beki mzuri; lakini Jagielka anacheza timu ambayo haijazoea sana kukaba.(i.e.Everton).
6. Roy ni kocha wa kawaida; kwa hiyo huwezi kutegemea alete mapinduzi makubwa kwenye timu ya taifa. Pia Roy amewahi kufanya kazi Fulham na Liverpool(walimfukuza lakini); hajawahi kuwa kocha mwenye mafanikio makubwa kulinganishwa na uzito wa mashindano yenyewe.
7. Kapteni wa Uingereza hakuwa imara kwenye mashindano haya; ili ushinde lazima uwe na kiungozi ambaye ni imara kwa maneno na hata kiwango chake uwanjani. Yaani anaongoza kwa mfano. Sasa bila ushabiki wowote wala chuki binafsi wa LFC, Gerrard alikuwa chanzo cha kuzorota kwa timu nzima.:angry: