Wote wanaotumia na wanaopokea ruzuku ya haramu ni haramu

Wote wanaotumia na wanaopokea ruzuku ya haramu ni haramu

Ivan said

Member
Joined
Feb 14, 2021
Posts
83
Reaction score
107
Kama hawa wabunge wanaoitwa COVID -19 ni haramu ni kwa nini Chama kinapokea (kama kinapokea) ruzuku inayotokana na watu haramu wanaovunja ibara ya 78(e) ya Katiba ya JMT inayotabanaisha kuwa ili mtu awe mbunge ni lazima atokane na chama cha siasa?

Bila shaka hii ni danadana tu ilihali akina Mh. Freeman Aikael Mbowe na timu yake wanafahamu ukweli wa jambo lenyewe ila wameamua kuwazuga akina mama/ wanawake wa CHADEMA na kwa kutokufahamu akina mama hawa wameanza kupiga yowe wasilofahamu chanzo chake ni nini!

Pamoja na mapungufu ya kibinadamu, nimemsikia Mh. Job Ndugai - Spika wa bunge la JMT akiomba vielelezo rasmi ili aweze kuwatimua wale watu wanaoitwa COVID - 19 mle bungeni.

Ni kwa nini CHADEMA wasipeleke hivi vielelezo (Muhtasari wa kikao kilichoaziamia kuwavua uanachama, katiba ya chama (kifungu cha kumfukuza mwanachama) na maamuzi ya kamati/baraza kuu la chama) ili kuthibitisha kuvuliwa uanachama kwa hao watu na ivo kupoteza sifa ya kuitwa wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

Muda ni mwalimu mzuri, ama Mbowe anawazuga wanachama wake au Spika Job Ndugai ameamua kuwakingia kifua watu haramu huku akifahamu kufanya hivyo ni kwenda kinyume ibara ya 78(e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Mdogo wangu Ivan hebu sikia, anachohitaji spika wa bunge ili kumthibitisha au kumfukuza mbunge ni barua tu, unanielewa? Kisheria chama kinamtambulisha mbunge kwa spika kwa kutumia barua na si rejea za vikao na ushahidi wa mabaraza. Anachotakiwa kuhoji spika ni uhalisia wa barua iliyotumwa kwake baaasi!

Hoja yako ya ruzuku kuwa haramu unajibiwa na tamko la chadema kuwa hawajawahi kupokea ruzuku toka serekalini tangu baada ya uchaguzi mkuu uliopita.

Usicheze mziki usiona maana mkuu. Hapa ni kuchagua tu kuendelea kuvunja katiba au kujirudi na kuheshimu katiba. Tusitafute justification zisizo na maana yoyote.
 
Mdogo wangu Ivan hebu sikia, anachohitaji spika wa bunge ili kumthibitisha au kumfukuza mbunge ni barua tu, unanielewa? Kisheria chama kunamtambulisha mbunge kwa spika kwa kutumia barua na si rejea za vikao na ushahidi wa mabaraza. Anachotakiwa kuhoji spika ni uhalisia wa barua iliyotumwa kwake baaasi!

Hoja yako ya ruzuku kuwa haramu unajibiwa na tamko la chadema kuwa hawajawahi kupokea ruzuku toka serekalini tangu baada ya uchaguzi mkuu uliopita.

Usicheze mziki usiona maana mkuu. Hapa ni kuchagua tu kuendelea kuvunja katiba au kujirudi na kuheshimu katiba. Tusitafute justification zisizo na maana yoyote.
Asante Mkuu, hata mie sikusema 100% kuwa wanapokea ruzuku kama ukinukuu kwa ufasaha. Hakuna mwenye akili timamu anayefurahia kuona watu haramu wakiwa bungeni na kutumia kodi zetu isivyo sahihi.
 
Asante Mkuu, hata mie sikusema 100% kuwa wanapokea ruzuku kama ukinukuu kwa ufasaha. Hakuna mwenye akili timamu anayefurahia kuona watu haramu wakiwa bungeni na kutumia kodi zetu isivyo sahihi.
Na ruzuku haihusiani na wabunge kuwa au kutokuwa Bungeni!!??
 
Mdogo wangu Ivan hebu sikia, anachohitaji spika wa bunge ili kumthibitisha au kumfukuza mbunge ni barua tu, unanielewa? Kisheria chama kunamtambulisha mbunge kwa spika kwa kutumia barua na si rejea za vikao na ushahidi wa mabaraza. Anachotakiwa kuhoji spika ni uhalisia wa barua iliyotumwa kwake baaasi!

Hoja yako ya ruzuku kuwa haramu unajibiwa na tamko la chadema kuwa hawajawahi kupokea ruzuku toka serekalini tangu baada ya uchaguzi mkuu uliopita.

Usicheze mziki usiona maana mkuu. Hapa ni kuchagua tu kuendelea kuvunja katiba au kujirudi na kuheshimu katiba. Tusitafute justification zisizo na maana yoyote.
Sure
 
Unajua ruzuku inalipwa kwa kutumia vigezo gani bwashee?
Uchaguzi ule ni "batili". As such, kura alizopewa Lissu ni batili as well, na RUZUKU ni batili. Hatuwezi kukataa viti maalumu 19 ila tukazikubali kura za Lissu.

Kura alizopewa Lissu (hence Ruzuku), ubunge aliopewa Aida na nafasi 19 vyote ni batili maana vyote common denominator ni process ya uchaguzi ule. Unless of course tunakubaliana na uchaguzi ule.

Kama tunazikubali kura alizotupiwa Lissu (RUZUKU) na kuukubali ubunge wa Aida, kwanini tukatae nafasi 19 za viti maalumu? Au tunazikubali ila shida ilikuwa/ni nani haswa ateuliwe kwenda kule mjengoni?
 
Mmeshaambiwa mulete ushahidi wa bank slip kuwa CHADEMA wanapokea ruzuku lakini hakuna mwenye huo udhubutu, itaendelea kuwa propaganda za ccm kuwa CHADEMA inapokea ruzuku
 
Mdogo wangu Ivan hebu sikia, anachohitaji spika wa bunge ili kumthibitisha au kumfukuza mbunge ni barua tu, unanielewa? Kisheria chama kinamtambulisha mbunge kwa spika kwa kutumia barua na si rejea za vikao na ushahidi wa mabaraza. Anachotakiwa kuhoji spika ni uhalisia wa barua iliyotumwa kwake baaasi!

Hoja yako ya ruzuku kuwa haramu unajibiwa na tamko la chadema kuwa hawajawahi kupokea ruzuku toka serekalini tangu baada ya uchaguzi mkuu uliopita.

Usicheze mziki usiona maana mkuu. Hapa ni kuchagua tu kuendelea kuvunja katiba au kujirudi na kuheshimu katiba. Tusitafute justification zisizo na maana yoyote.
Ruzuku inaingia kwenye akaunti ya bodi ya wadhamini ya chama, kisha wao wanaitoa kupeleka kwenye akaunti ya kila siku ya chama, Chadema watoke waseme kama hiyo hela haijaingia

Wasije wadanganya kwamba wanaenda kusaini ili ziingie
 
Back
Top Bottom