XAVI Umepiga Kazi Mitaa ya Wapenda Soka Haitokudharau Imekuheshimu

XAVI Umepiga Kazi Mitaa ya Wapenda Soka Haitokudharau Imekuheshimu

THE FIRST BORN

JF-Expert Member
Joined
Apr 24, 2019
Posts
2,224
Reaction score
4,472
Mpira ni Mchezo ambao unafanya watu wasahau Maumivu ya Gharama kubwa za Maisha ndani ya dakika 90.
Mpira ni Mchezo ambao unafanya watu wa Dini Tofauti wasahau Imani zao kwa Mda, na wote wanakua na Dini Moja kwa dakika 90. Mpira ni Mchezo ambao unafanya wapinzani kisiasa waungane kwa dakika 90.
Mpira ni Mchezo unaofanya watu walio na shida za kimahusiano katika Familia zao wazisahau kwa dakika 90.

XAVI anaposema Anaondoka It Means amefikiri yote haya..Barcelona ni kubwa kuliko Spain,Barcelona ni Kubwa Kuliko Marekan na China. XAVI Alikua anaongoza Jeshi la watu wengi zaidi Dunian.

XAVI Anavyosema anaondoka Maana yake anataka kuponya Mioyo ya hawa Watu...Anatambua kua Mpira ni kiunganishi cha Mambo yote yaliyoharibika Dunian,akiendelea kukalia kiti atakua anaumiza Mioyo ya wapenda Soka hasa wana Familia ya Barca Dunian Kote ambao naamini ni Wengi kuliko Hata Nchi ya Tanzania.

Mitaa itakuheshimu (XAVI).

IMG-20240128-WA0003.jpg


#Football Addicts Street

#Mitaa ya Wapenda Soka hua hatumdharau Msela Mpambanaji.
 
Kwanini paka mwisho wa msimu? Kama anaipenda Barca aondoke sasa hivi, maana kwa mwenendo huu huko mwisho wa msimu timu si itakuwa ishashuka daraja
Ulaya sio Bongo kwamba unafukuza au kocha uondoke katikat ya msimu kuna mambo yanatakiwa uyamalize then aje kocha aanze na project yake na yeye.

Saiv hakuna kocha anaweza kuja katikati ya msimu
 
Kabisa.

Mimi nafkri angesepa sasa.

Asisubiri mwisho wa msimu.
Unaondokaje unadhani Barca kama Gwambina..Kwamba kocha anajitokeza tu aje wakat Team haiko vizur?

Akiondoka saiv kuna uwezekano mkubwa wa Team kuyumba zaid ya hapo.

Ulaya ndio maana mambo mengi kwenye Team zao hua yananza na Msimu Mpya sio katikati ya msimu.
 
Team imemshinda. Kuiishi history kazi sana.

Kufika juu sawa ila kuendelea kuwa juu ni swala gumu zaidi.
 
Kwanini paka mwisho wa msimu? Kama anaipenda Barca aondoke sasa hivi, maana kwa mwenendo huu huko mwisho wa msimu timu si itakuwa ishashuka daraja

Barca imeanza kufanya vibaya kabla hata ya uwepo wa Xavi, tena tumshukuru sana Xavi maana kwa kiasi kikubwa ameweza rudisha japo nusu ya DNA ya Barca...
 
Yaani yale mabao matano ya Jumamosi, yaliniumiza sana, hasira zote sikaishia kwenye konyagi, kwa mbali Nigeria walipoza kidogo
 
Unaondokaje unadhani Barca kama Gwambina..Kwamba kocha anajitokeza tu aje wakat Team haiko vizur?

Akiondoka saiv kuna uwezekano mkubwa wa Team kuyumba zaid ya hapo.

Ulaya ndio maana mambo mengi kwenye Team zao hua yananza na Msimu Mpya sio katikati ya msimu.
Mbona Roma wamemtimua Mourinho katikati ya msimu, au Italy sio ulaya? Hata uko ulaya Kocha anatimuliwa muda wowote ule hakuna cha mwisho wa msimu wala katikati.
 
Back
Top Bottom