Caller & msg app ni mhimu kuliko unavyofikiria, ndo huchangia kukufanya ufurahie simu au uione haina maajabu na ndo app zinazotumika zaidi kuliko zingine
Kuhusu caller sina information ya kutosha Kwa One UI caller ila kama unaongelea Message App basi Google message app ni bora kuliko Samsung messages
1. Kwenye Google message ukienda kwenye messages zako, unaweza ku-archive message kwa ku-swipe message hiyo kwenda kushoto au kulia. Kwa kufanya simple action kama hii pekee inakuwezesha kupeleka message kwenye Archive folder.
Kwenye Samsung messages hakuna archive folder na wala haiwezi ku-swipe message kwenda kulia wala kushoto.
2. Kwenye Google Message unaweza kutuma GIFs wakati kwenye Samsung Messages hauwezi kabisa kutuma GIFs.
3. Kwenye Google Message unaweza kutuma stickers kwa kutumia keyboard yoyote, kwenye Samsung messages hauwezi mpaka u-activate Samsung keyboard ndio utatuma stickers. Shame!
4. Feature ya Spam and Block ya kwenye Google Messages ina-function vizuri kuliko kwenye Samsung messages. Google Message inadetect spam messages kirahisi kuliko Samsung messages. Hata kama ukipigiwa simu na namba ngeni, taarifa kuhusu hiyo event inaenda moja kwa moja kwenye Spam folder. Hii ni feature nzuri sana ambayo Samsung messages inakosa
5. Kuhusu suala la Notifications bado Google Messages ipo vizuri kuliko Samsung Messages. Kwa mfano ukitumiwa notification yenye code ndani yake na ile notification ika pop up juu ya display yako, Google Message inatumia mfumo wa AI kutambua code kwenye notification hiyo kwa hiyo inakuruhusu ku-copy code hiyo papo hapo bila hata kuingia kwenye app. Yaani inakuruhusu ku-copy code hiyo kupitia palepale kwenye Notification bar kwa kuigusa tu code hiyo.
Samsung messages haiwezi kufanya hii kitu. Kwenye Samsung message haitumii mfumo wa akili bandia kwa hiyo ujumbe wenye code ukiingia inapata options tatu tu Call, Mark as Read na Reply, wala hakuna option ya "Copy code"
6. Bado kwenye suala la Notifications yenye code kuna feature ambayo Google Message app anayo na ni nzuri sana ila Samsung Messages haina.
Kwenye Google Messages kuna feature ambayo inaruhusu kufuta message hizi automatically baada ya saa 24 na ni useful sana kwa sababu codes hizi hu-expire ndani ya saa 24. Samsung Messages haina feature hii.
7. Kwenye searching Google Messages inafanya kazi nzuri na ipo organised kuliko kwenye Samsung Messages.
Ukitap sehemu ya ku-search kwenye Google Messages Inakuletea row mbili; row ya kwanza ni Recent conversation ambayo inakuonesha conversation ulizofanya hivi karibuni kuanzia most recent kwenda kwenye least recent.
Row ya pili ni Categories ambayo inakukusanyia categories kwenye very organized way. Categories hizo ni Starred, Images, videos, places, na links. Hii system ya arrangement kwenye Google Messages ni nzuri kuliko kwenye Samsung Messages
Kwenye Samsung Messages kuna row mbili pia, row ya kwanza ni pictures and videos na row ya pili ni Others ambayo inaonesha other attachments. Hii arrangement ni poor ukifananisha na Google Messages
8. Google Message ipo vizuri kwenye ku-receive iPhone emoji reactions. Kwa mfano mtumiaji wa iPhone akireact kwenye message yako na emoji mbalimbali ([emoji106][emoji3][emoji81][emoji1666][emoji8], etc.) Google Message inaonesha hizi reactions papohapo kwa hiyo utaweza kuona hiyo reaction
Kwenye Samsung Messages huoni hizo emoji reaction.
9. Google Messages ina feature ya Smart Reply. Hii feature inakuonesha suggestions za kureply kwenye keyboard yako kulingana na text uliyotumiwa. Pia Google Message inajifunza tabia zako za kureply text za watu hivyo Smart reply inaweza kukusaidia ku-suggest reply based on text uliyotumiwa.
Samsung Messages haina hiyo feature ya Smart Reply.
10. Google Message ina feature ya "Message for Web" ambayo inakuwezesha kutuma na kupokea message kwenye kompyuta bila requirement nyingine yoyote
Kwenye Samsung Messages unaweza kufanya hivi pia lakini ni mpaka utumie app yao ya Samsung SideSync au Microsoft Phone link app. Wastage of time!
11. Kuhusu feature ya kwenye Samsung Messages ya kurespond kwenye message in a small pop up window huku unaendelea na shughuli nyingine imekuwa replaced na feature unique sana ya Google Messages inayoitwa text bubbles inayofanya kazi kama chat head kwenye messenger. Unique ideas is what we need
Samsung Messages App bado sana kuifikia Google Message App. Hata Samsung wenyewe wameanza kuset Google Messages kuwa default message app kwenye flagship zao na wanaipa Samsung Messages second priority. Kampuni yenyewe imeona umuhimu wa Google Message App na ukweli ni kwamba Google Message App ni application nzuri mara mia ya Samsung Message App.
Lastly naweza kusema tumia Samsung Message App kama kazi yako ni kutuma na kupokea messages tu. Ila kama unataka Message App ambayo iko matured na ina useful features nyingi basi tumia Google Message App, full stop.