Xplasters, Nini dhambi kwa mwenye dhiki?

Xplasters, Nini dhambi kwa mwenye dhiki?

Mwanakili90

JF-Expert Member
Joined
Nov 24, 2010
Posts
1,568
Reaction score
245
(Faza Nelly)

From the album 'Maasai hip
hop' (Out Here records, 2004) Swahili lyrics (English intro): All my people
East Africa
Tanzania, Uganda and Kenya
Dar es Salaam, A town
Wherever you are
Piga magoti, tuombe Mungu Hii ni siasa, dini, vita, ubwana,
utwana, au kiama ghalika,
sodoma na gomora?
Simama imara, zunguka kila
kona, kila anga angaza
Kushoto, kulia, mbele, nyuma kote pitia

Na hapo ulipojishikiza
g'ang'ania, sikilizia, vumilia
baadae usije jutia Hii ni mahususi na maalum
kwa watu wangu
Walemavu, vipofu, zeruzeru na
wendawazimu
Watoto wa mitaani, fukara,
masikini na wenye akili zao timamu

Hii kamba ngumu
Mjue tunavutana na wenye
nguvu
Vitambi na mashavu
Hakuna tena fair game Refarii kauzu
Uwanja wenyewe mkavu
Ujira mgumu, malipo finyu
Kilichobaki kucheza rafu
Tumechoshwa na ukabaila,
ubepari na ubeberu

Wakati ndo huu
Ukombozi ndo huu
Na sasa naamuru mliopo chini
wote mpate divai ya vinibu
Mtetezi wenu nikaze gidamu

Nimwage sumu ya ----- juu yao
Wajikune bila aibu
Kwanza saluti kwa
waliyotangulia kuzimu
Pili tuombe Mungu
Baba yetu, utupe mkate wetu wa kila siku
Utujaze nguvu
Tupate kudumu ndani ya game
Tutakapofika kuzimu siku ya
hukumu
Utupe nafasi tupate kutubu Kwani tunajua tunatenda
maovu
Tunakula haramu
Tunatumia kila mbinu
Juju, uhalifu, upanganyifu
Ili tuweze kujikimu Lakini isiwe kisingizio kwa
wanadamu wengine
kunyimwa haki zetu
Kutuzibia riziki zetu
Kutuita makafiri, dharau na
kutukashifu Kwani nini dhambi

Chorus :
Nini dhambi kwa mwenye
dhiki,
Kipi haram, kipi halali,
Kila mmoja anaitaka hii riziki
Kitendawili, vurugu mechi Huwezi tabiri Kwa nini ?

Uliza swali, kama
sote tungekuwa wasomi,
matajiri
Ni nani angelifanya kazi za
kutisha na hatari mfano ya
mochwari Kila mmoja wetu hapa mjini
kaja kwa dili
Kila kitu, kila mahali
Na hata ngozi ya mtu dili
Wengine wachawi, waganga
feki Matapeli, wasafiri ------
Wakati wengine wapole kama
walokole

Mchana pirika nyingi maofisini
Kumbe night kali, kahaba
Shuga, jambazi, mengine ya kusitiri
Ah!
Wapo waliopoteza maisha
katika kufight life
Kumbukumbu zao zimebaki
makaburini Na wapo waliopoteza kabisa
tumaini la kuwini
Hao roho zao utadhani
wamezitoa rehani
Wakikutight mahali fulani
Inabidi uwakabidhi mshahara wote wa mwisho wa mwezi

(Chorus)

Kweli Bongo kutafuta braza
Utajajuta utakapojikuta huna
hata bukta
Shauri yako we tegesha tu
kama golikipa
Na hao unaowategemea mwishowe watakutosa
Huna elimu, hun fani
Lakini nguvu, hulimi, uchumi
unao unaukalia
Kumbuka
Kupata au kukosa yote ni kawaida
Sometimes unalala unaota
unakula
Unakunywa, unapiga denda
Na kula uroda na demu bomba
Ukikurupuka tu unakuta patupu
Hakuna kitu

(Chorus, Yamat singing a
traditional Maasai song)
 
(Faza Nelly)

From the album 'Maasai hip
hop' (Out Here records, 2004) Swahili lyrics (English intro): All my people
East Africa
Tanzania, Uganda and Kenya
Dar es Salaam, A town
Wherever you are
Piga magoti, tuombe Mungu Hii ni siasa, dini, vita, ubwana,
utwana, au kiama ghalika,
sodoma na gomora?
Simama imara, zunguka kila
kona, kila anga angaza
Kushoto, kulia, mbele, nyuma kote pitia

Na hapo ulipojishikiza
g'ang'ania, sikilizia, vumilia
baadae usije jutia Hii ni mahususi na maalum
kwa watu wangu
Walemavu, vipofu, zeruzeru na
wendawazimu
Watoto wa mitaani, fukara,
masikini na wenye akili zao timamu

Hii kamba ngumu
Mjue tunavutana na wenye
nguvu
Vitambi na mashavu
Hakuna tena fair game Refarii kauzu
Uwanja wenyewe mkavu
Ujira mgumu, malipo finyu
Kilichobaki kucheza rafu
Tumechoshwa na ukabaila,
ubepari na ubeberu

Wakati ndo huu
Ukombozi ndo huu
Na sasa naamuru mliopo chini
wote mpate divai ya vinibu
Mtetezi wenu nikaze gidamu

Nimwage sumu ya upupu juu yao
Wajikune bila aibu
Kwanza saluti kwa
waliyotangulia kuzimu
Pili tuombe Mungu
Baba yetu, utupe mkate wetu wa kila siku
Utujaze nguvu
Tupate kudumu ndani ya game
Tutakapofika kuzimu siku ya
hukumu
Utupe nafasi tupate kutubu Kwani tunajua tunatenda
maovu
Tunakula haramu
Tunatumia kila mbinu
Juju, uhalifu, upanganyifu
Ili tuweze kujikimu Lakini isiwe kisingizio kwa
wanadamu wengine
kunyimwa haki zetu
Kutuzibia riziki zetu
Kutuita makafiri, dharau na
kutukashifu Kwani nini dhambi

Chorus :
Nini dhambi kwa mwenye
dhiki,
Kipi haram, kipi halali,
Kila mmoja anaitaka hii riziki
Kitendawili, vurugu mechi Huwezi tabiri Kwa nini ?

Uliza swali, kama
sote tungekuwa wasomi,
matajiri
Ni nani angelifanya kazi za
kutisha na hatari mfano ya
mochwari Kila mmoja wetu hapa mjini
kaja kwa dili
Kila kitu, kila mahali
Na hata ngozi ya mtu dili
Wengine wachawi, waganga
feki Matapeli, wasafiri kafiri
Wakati wengine wapole kama
walokole

Mchana pirika nyingi maofisini
Kumbe night kali, kahaba
Shuga, jambazi, mengine ya kusitiri
Ah!
Wapo waliopoteza maisha
katika kufight life
Kumbukumbu zao zimebaki
makaburini Na wapo waliopoteza kabisa
tumaini la kuwini
Hao roho zao utadhani
wamezitoa rehani
Wakikutight mahali fulani
Inabidi uwakabidhi mshahara wote wa mwisho wa mwezi

(Chorus)

Kweli Bongo kutafuta braza
Utajajuta utakapojikuta huna
hata bukta
Shauri yako we tegesha tu
kama golikipa
Na hao unaowategemea mwishowe watakutosa
Huna elimu, hun fani
Lakini nguvu, hulimi, uchumi
unao unaukalia
Kumbuka
Kupata au kukosa yote ni kawaida
Sometimes unalala unaota
unakula
Unakunywa, unapiga denda
Na kula uroda na demu bomba
Ukikurupuka tu unakuta patupu
Hakuna kitu

(Chorus, Yamat singing a
traditional Maasai song)
Asante mkuu,hawa jamaa nimebahatika kuwa nao karibu kipindi bado nipo Arusha! Faza Nelly alikuwa anaaminika ndio the best Hiphop Artist ever in Arusha! Binafsi mpaka kesho naamini hivyo na ndio alikuwa kichwa wa kundi! Mafanikio ya kundi lao hayajawahi kuvunjwa rekodi na kundi lolote Tanzania hii! Ndio wasanii wa kwanza wa Hiphop video yao kurusha Channel O! At that time our video quality was extremly poor lakini hawa jamaa walikuwa level nyingine! Walikuwa wanaitwa kupiga shows Senegal,SA,USA,Holland etc while hapa Bongo walikuwa hawaitwi sababu wanyonyaji walikuwa hawawezi kuwalipa wanavyotaka! Hawa jamaa walikuwa wanakutana na kuheshimiwa na Ma legend kibao wa Mbele! Na amini usiamini hawa ndio waliofanya huko duniani kujua Tanzania kuna Hiphop! Jamaa style yao ilikuwa ni hiphop masai na walifunika sana tu ila tatizo Faza Nelly ndio alikuwa mtunzi na mbunifu sana ndio maana kama alikufa na kundi.Muulize mwanahiphop yeyote wa Arusha kuhusu Faza Nelly uambiwe! Msiba wake ni moja ya misiba iliyopata mahudhurio makubwa mno Arusha.RIP FAZA NELLY!
 
R. I. P Father Nelly kwa kwel huyu jamaa na Kundi lao la Xplastaz ni icon nzur sana kwa Hip Hop ya Bongo nawakumbuka sana na Hip Hop Masaai yao....Wimbo kama USHANTA, HAAAA HAAAAA na kadhalika kadhalika..naona sasa hivi kuna Madogo wanaliendeleza vizur kundi..
 
naomba mwenye kujua jina la albam yao ya kwanza. nimeshindwa nipateje nyimbo zao hawa jamaa. Msaada jamani. Mia
 
naomba mwenye kujua jina la albam yao ya kwanza. nimeshindwa nipateje nyimbo zao hawa jamaa. Msaada jamani. Mia

Kwa kwel hata mie sikumbuk Albam yao ila nakumbuka baadhi ya nyimbo zao za wakati ule Miaka ya 90 kama vle USHANTA, HAAA, MSIMU KWA MSIMU, NINI DHAMBI KWA MWENYE DHIKI na BAMIZA...
 
nilikuwa nakisaka kinasa,sasa nimekipata,raffu....raffu nelly ...na mneli....
wakuu hawa ndio artists wa ukweli tanzania.
 
R. I. P Father Nelly kwa kwel huyu jamaa na Kundi lao la Xplastaz ni icon nzur sana kwa Hip Hop ya Bongo nawakumbuka sana na Hip Hop Masaai yao....Wimbo kama USHANTA, HAAAA HAAAAA na kadhalika kadhalika..naona sasa hivi kuna Madogo wanaliendeleza vizur kundi..
USHANTA! Umenikumbusha mbali sana mkuu! Wakati Arusha ikiwa Arusha kweli na machizi wa Mbuguni!
 
Kuna rapa kutoka Xplastaz ivi karibuni alipafomu kwenye tuzo za BET ile sehemu ya freestyle battle,simpati jina..huwezi amini hawa jamaa wanafahamika nje zaidi ya bongo.
 
Kuna rapa kutoka Xplastaz ivi karibuni alipafomu kwenye tuzo za BET ile sehemu ya freestyle battle,simpati jina..huwezi amini hawa jamaa wanafahamika nje zaidi ya bongo.

bongo(hasa dar) wanapenda porojo sana.ile freestyle alikuwepo KRS ONE!
 
Kuna rapa kutoka Xplastaz ivi karibuni alipafomu kwenye tuzo za BET ile sehemu ya freestyle battle,simpati jina..huwezi amini hawa jamaa wanafahamika nje zaidi ya bongo.


Ni kweli Matumbo hata Me nliiona hyo kwenye zle segments za BET freestyles, kama nakumbuka vzur atakuwa anaitwa GSAN..
 
Taften Wimbo mpya wa XPlastaz unaitwa AFRICA wamemshirikisha Fid Q na Mshikaji mwingine cjui wa Marekani yule, hauna cku nying sana nadhan umetoka Mwez wa 9 au 10, 2011..
 
Dar imefanywa ipende kile wanyonyaji wanapenda! Hawataki watu wenye misimamo mikali ili wawatumie! Fikiria mtu kama Dogo Hashim anapotea!
 
Ukweli huu wimbo kwangu mimi ndio bora kwa Hip Hop ya Tanzania,siwapendi sana Xplastaz but hii track ndio bora kwangu hata Video yake iliendana na mazingira ya Tanzania
R.I.P Nelly
 
Asante mkuu,hawa jamaa nimebahatika kuwa nao karibu kipindi bado nipo Arusha! Faza Nelly alikuwa anaaminika ndio the best Hiphop Artist ever in Arusha! Binafsi mpaka kesho naamini hivyo na ndio alikuwa kichwa wa kundi! Mafanikio ya kundi lao hayajawahi kuvunjwa rekodi na kundi lolote Tanzania hii! Ndio wasanii wa kwanza wa Hiphop video yao kurusha Channel O! At that time our video quality was extremly poor lakini hawa jamaa walikuwa level nyingine! Walikuwa wanaitwa kupiga shows Senegal,SA,USA,Holland etc while hapa Bongo walikuwa hawaitwi sababu wanyonyaji walikuwa hawawezi kuwalipa wanavyotaka! Hawa jamaa walikuwa wanakutana na kuheshimiwa na Ma legend kibao wa Mbele! Na amini usiamini hawa ndio waliofanya huko duniani kujua Tanzania kuna Hiphop! Jamaa style yao ilikuwa ni hiphop masai na walifunika sana tu ila tatizo Faza Nelly ndio alikuwa mtunzi na mbunifu sana ndio maana kama alikufa na kundi.Muulize mwanahiphop yeyote wa Arusha kuhusu Faza Nelly uambiwe! Msiba wake ni moja ya misiba iliyopata mahudhurio makubwa mno Arusha.RIP FAZA NELLY!



Rest In Peace Faza Nelly.

Hawa jamaa ndio wa kwanza (na ninafikiri haijawahi tokea mwingne) kuwa kwenye album collection na wana hip hop wa marekani kama kina 50 Cents. Nazungumzia collections za west huko.
 
Kuna rapa kutoka Xplastaz ivi karibuni alipafomu kwenye tuzo za BET ile sehemu ya freestyle battle,simpati jina..huwezi amini hawa jamaa wanafahamika nje zaidi ya bongo.


anaitwa G SAN alifanya cypher na kina KRS 1
 
kwa ambao hawakufanikiwa kuwaona Xplasters wakiperform live wakiwa wamekamilika na Faza Nelly nawasikitikia kwa kukosa burudani ambayo usingeamini kama jamaa ni wabongo!
 
Back
Top Bottom