Ya moto moto kabisa kutoka Manchester United inasema ya kwamba wiki ijayo huenda Jose Mourinho ' akafukuzwa ' rasmi!

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Mmoja wa Mfanyakazi Mwandamizi kabisa wa Klabu ya Manchester United ametoa Siri ya kwamba kuna dalili zote na za kutosha kuwa Wiki ijaya Kocha ' Mbwatukaji ' na mwenye ' Nyodo, Ujivuni pmoja na Dharau ' nyingi Jose Mourinho anaenda Kutemeshwa Kibarua ( Kufukuzwa Kazi )

Ngoja Mimi GENTAMYCINE nibaki tu na Liverpool FC yangu na kama mwaka huu hatutochukua Ubingwa wa EPL nitaogelea kutoka Bugolora hadi Bwisya chini kwa chini bila ' Kuibuka ' kwenda na kurudi ng'ambo zote.

Source ya taarifa ni BBC Sports.

Nawasilisha.
 
Alishawahi kuiharib chelsea twice. Na hapa anafanya the same kwa united. Pattern ni zile zile, kiburi kugombana na wachezaji.

Kama ataendelea na tabia hii. Hata akienda na psg hatadumu
 
Zizzou anakuja pale tupumue kidogo maana....
 
Huoni kama gardiola anaongoza lig, wiki ijayo mtakipata cha motoo man city oyeeee
 
Zizzou anakuja pale tupumue kidogo maana....

Siku zingine ukijua unataka Kumzungumzia Zinedine Zidane ' Sharti ' Kuu unatakiwa Kwanza uanze na ' Title ' yake ' tukuka ' kabisa ya ' Midfield Maestro Zinedine Zidane ' sawa? Huyu Mtu mwaka 1998 wakati wa Kombe la Dunia huko Ufaransa ndiyo alikuwa akinifanya ' nitoroke ' usiku ' Bwenini ' Shuleni Upili ( Secondary ) huku nikikatiza ' Majaruba ' ya Watu, Kulowana na Mvua, Kukanyaga Nyanya za Watu Usiku hadi kuna Siku nikafumwa na Mmoja wa Walimu wangu na kupewa ' bonge ' la adhabu lakini bado sikuacha kwenda kumuangalia kila Ufaransa yake ilipokuwa inacheza. Ni Mchezaji ambaye ana kila Kitu ambacho ' Play maker ' anatakiwa awe nacho na kikubwa cha ziada ambacho anacho ni kwamba Mpira haumlazimishi Yeye bali Yeye ndiye alikuwa anaulazimisha Mpira jinsi atakavyo huku Mpira nao ukimkubalia na kumwambia ' Shikamoo Fundi Zidane '. Kuna Watu Mwenyezi Mungu kawapa Shani / Tunu zao na ' Midfield Maestro Zinedine Zidane ' ni mmoja wao hakyanani.
 
Midfield maestro zinedine zidane"zizzou" fundi.

Unaonaje akija pale OT anaweza kufua dafu kama alivyofanya santiago?
 
yule mzee mpaka dakika hii haikuaaswa kuwa kocha wa Man u....nashangaa bado ni manager wetu
 
Manchester United hawana tabia ya kufukuza makocha Kati Kati ya msimu, hili haliwezekani
 
Ee Mwenyezi uliye mkuu wa yote na unaesikiliza maombi ya waja wako naomba kwa moyo wa dhati usaidie kunusuru kibarua cha Mourinho kwakuwa nayeye ana familia inayomtegemea.

Naomba hawa wote wanaomuombea Mourinho afukuzwe kazi washindwa kwa Jina la Yesu alie juu. Napinga roho za kinyama na kikatili kama hizo kwakuwa Mourinho nae ni mtu wako uliyemleta duniani na anayopitia ni mipango yako ee Mungu baba.

Amen.
 
Manchester United hawana tabia ya kufukuza makocha Kati Kati ya msimu, hili haliwezekani
Lolote linaweza tokea. Kwa hali ilivyo. Mou hana siku nyingi. Ukisha chukiwa na wachezaji, haba members wa bodi. Huna muda mrefu.
 
Lazima aende tu maana hakuna namna. Kila timu anayotoka lizamw awe na ugomvi na wachezaji.
Na hili klab kubwa kama man hawawez kuvumilia. Makocha wazur wako wengi tu..
 
Manchester United hawana tabia ya kufukuza makocha Kati Kati ya msimu, hili haliwezekani

Miswahili bhana! Wewe uko Tandale hii taarifa kaitoa Mtu ambaye ni Mfanyakazi wa Manchester United na yupo huko huko Uingereza na Klabu husika tofauti na Wewe ambaye Klabu hiyo unaijua Kupitia tu Runinga huko ' Vibanda Umiza ' Kwenu unataka Kubisha.
 
Tuwe na utulivu tu


Jose Mourinho: "I'm not leaving this team today. Not tomorrow. Some players Will leave this club but i Will still be here. Some(players) think they are bigger than this club but i Will say no. They act like Hip hop or rap stars" #MUFC
 
Mpaka nimejiuliza au mchawi hadi mpaka sasa mabosi wanamwangalia tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…