Ya NEC, ZEC au Jecha si ndiyo haya ya IEBC?

Ya NEC, ZEC au Jecha si ndiyo haya ya IEBC?

Nikitazama vizuri hapa naona kama kuna mgogoro/kutoaminiana kati ya Chebukati na Raila, na hii inakuwa mbaya sana kwasababu inaenda kutengeneza matabaka baina ya wale watendaji wa IEBC, ni kama vile wale wajumbe walikuwa na wagombea wao hii kitu inaharibu sifa ya IEBC kutakiwa kuwa chombo huru.

Hii si ndiyo maana ya uhuru sasa? Kwamba kama mbwai na iwe mbwai? Kwa uhuru kabisa na kila mtu aeleze alikopeleka mboga.

Hatishiwi mtu hapa!

Umoja wa IEBC wa nini mkuu kama ule ukimya wa ZEC ya Jecha nao ulifuzu kuitwa umoja?

Tabia hizi za kamati za ulinzi na usalama kuja na matokeo yao ya kutangazwa na tume ni lazima zikomeshwe.

Yatokeayo Kenya na yatufungue macho haswa!
 
Tume za uchaguzi dunia nzima huwa zina mikono ya watu wa pembeni. Hata Trump alilalamikia Radical left wamemuibia kura na kubadili matokeo. China tu ndiko hamna wizi wa kura.
China sio kwamba hakuna bali huwezi kuhoji
Changamoto kwenye uchaguzi wa kenya zitawafanya huko mbele wastabilize
 
Kenya walishakataa kwa vitendo 2007,Leo hayo yanaendelea Kama kawaida.''THIS IS AFRICA''

Sent from my TECNO KB8 using JamiiForums mobile app

Ni kweli Kenya walikataa kwa vitendo 2007 lakini walipo leo wanawajua wabaya wao kwa majina yao.

IGP Hilary Mutyambai kokote aliko anapumulia mashine. Bado yule CDF na yule mkurugenzi wa ile TISS yenyewe ya huko.

Hiiiiii bagosha!
 
Nimesoma hiyo link naona Raila nae analalamikia hao Venezuelans kuingilia uchaguzi, hapa bado naona kuna ushindani usio wa lazima utakaoenda kuamuliwa mahakamani tu, kuziamini hizi pande mbili kwa sasa ni kudanganyana, kila upande utakuja na lake.

Kwa vile kinachohitajika ni haki. Zipo sababu za kuamini ukweli wote utafahamikq kwenye hii tapa tapa ya wafa maji.

Four commissioners say Chebukati asked them to approve unverified results

Kwa hakika hii ngoma inogile.
 
Matumizi ya neno "indicate" hapo yananipa ukakasi kumuelewa Chebukati, kwangu mimi kama angesema "they ask me"

Hapo ningemuelewa vizuri zaidi na ningekubaliana na jibu lake kwamba " I told them I could meet them in the presence of all commissioners"

Otherwise, kwangu hilo jibu alilotoa Chebukati ni kama amejihami, anajilinda yeye na yule ampendaye, kwanini?

1. Why haya ameyaleta leo, alikuwa wapi siku zote?

2. Shahidi wake wakati akikutana na hao jamaa walikuwa wakina nani?

Chebukati atulie aiachie mahakama yao iamue hatma ya hiyo kesi, huku kuzungumza kwake jambo lililo nje ya mahakama kwa sasa ni sawa na kuingilia uhuru wa mahakama.
Haya unayoleta wewe ni mapenzi kwa Mtu wako. Yeye ndo aliyefuatwa sirini. Kwa Mtu mwenye dhamana kubwa kama ile ulitaka atoke kesho yake atangaze, "watu wa state wamenifuata usiku tuongee kuhusu tallying". Huku ikijulikana state iko na nani?
 
Tume za uchaguzi dunia nzima huwa zina mikono ya watu wa pembeni. Hata Trump alilalamikia Radical left wamemuibia kura na kubadili matokeo. China tu ndiko hamna wizi wa kura.
China ni Tanzania ya mashariki ya mbali. Tume inaweza kukupa kura ukiziweka kwenye asilimia inatoka 116%.
 
Nikitazama vizuri hapa naona kama kuna mgogoro/kutoaminiana kati ya Chebukati na Raila, na hii inakuwa mbaya sana kwasababu inaenda kutengeneza matabaka baina ya wale watendaji wa IEBC, ni kama vile wale wajumbe walikuwa na wagombea wao hii kitu inaharibu sifa ya IEBC kutakiwa kuwa chombo huru.
Huu mgogoro una faida kubwa kwa Kenya kwa sababu ya nature yao ya kutumia migogoro kama fursa. Baada ya hapa watakaa na watatoka na kitu real.
Kuhusu Wavenezuela, ni namna tu ya kuifanya Mahakama itilie shaka matokeo. Watu wanaolalamikiwa walikamatwa na mpaka wakati wa uchaguzi haikuelezwa waliletwa na nani? Kama mwizi amekamatwa kabla ya kuiba, mnamtuhumu vipi baada ya tukio wakati mnaye mahabusu.
 
Huu mgogoro una faida kubwa kwa Kenya kwa sababu ya nature yao ya kutumia migogoro kama fursa. Baada ya hapa watakaa na watatoka na kitu real.
Kuhusu Wavenezuela, ni namna tu ya kuifanya Mahakama itilie shaka matokeo. Watu wanaolalamikiwa walikamatwa na mpaka wakati wa uchaguzi haikuelezwa waliletwa na nani? Kama mwizi amekamatwa kabla ya kuiba, mnamtuhumu vipi baada ya tukio wakati mnaye mahabusu.

Yawezekana upo ushahidi kuwa kuna wezi hawakukamatwa au madhara ya wengine wezi hata y walioko mahabusu, hayakuweza kudhibitiwa kwa wakati.
 
Hii si ndiyo maana ya uhuru sasa? Kwamba kama mbwai na iwe mbwai? Kwa uhuru kabisa na kila mtu aeleze alikopeleka mboga.

Hatishiwi mtu hapa!

Umoja wa IEBC wa nini mkuu kama ule ukimya wa ZEC ya Jecha nao ulifuzu kuitwa umoja?

Tabia hizi za kamati za ulinzi na usalama kuja na matokeo yao ya kutangazwa na tume ni lazima zikomeshwe.

Yatokeayo Kenya na yatufungue macho haswa!
Lakini pia hii hali inayotokea Kenya nikiitazama vizuri mwisho wa siku inaweza kuleta machafuko, makundi ya hao commissioners yanaweza kusababisha sintofahamu mwishowe warudie yale ya 2017.

Hapa kwetu bado tumelala, wajumbe wa tume hawana uwezo wa kuhoji yanayotokea kwenye tume ya uchaguzi, hii ni kwasababu M/kiti wa tume anateuliwa na Rais, nae mwenyekiti anateua wajumbe atakaoona wanamfaa, hawa hawawezi kugeukana.

Tofauti na Kenya, IEBC kuna wajumbe walioteuliwa na Kenyatta, ndio wale wanne waliogoma kukubali matokeo ya uchaguzi, na wakina Chebukati waliopatikana kwa utaratibu mwingine.
 
Huu mgogoro una faida kubwa kwa Kenya kwa sababu ya nature yao ya kutumia migogoro kama fursa. Baada ya hapa watakaa na watatoka na kitu real.
Kuhusu Wavenezuela, ni namna tu ya kuifanya Mahakama itilie shaka matokeo. Watu wanaolalamikiwa walikamatwa na mpaka wakati wa uchaguzi haikuelezwa waliletwa na nani? Kama mwizi amekamatwa kabla ya kuiba, mnamtuhumu vipi baada ya tukio wakati mnaye mahabusu.
Wale jamaa kukaa na kutoka na kitu real naona itategemeana na maamuzi ya mahakama kwenye hii kesi.

Kama Odinga akishinda kesi, anaweza kugomea kushiriki uchaguzi mwingine kwa madai hana imani na Chebukati, hii italeta kizungumkuti.

Ruto anaweza kurudi kwenye ushiriki mwingine kwa amani akijua Chebukati bado yupo kama M/kiti wa IEBC.

Nionavyo hiyo tume inatakiwa kuvunjwa wapatikane commissioners wengine neutral kabisa wasio na upande wowote ili kurudisha imani kwa Odinga na watu wake.
 
Hizi ndiyo zile nchi sasa akiziita Trump lile jina letu pendwa. Mola akawalinde ma commissioner hawa waliosimama imara na katiba ya nchi.

Yale yale ya kura pigeni mnakotaka ila washindi tutatangazwa sisi.

View attachment 2336941

"Chebukati names top govt officials who wanted to influence Presidential results outcome in favor of Raila » Capital News"

Kumbe wale wanaojinasibu kutokulala usiku kwa ajili yetu, kwa majina yao kutoka walikotoka hupelekaga matokeo yanayotakiwa kutangazwa?

Kwa mwendo huu bila tume hizi kuwekewa ulinzi japo wa ma blackwater, bado sana!
Nilivyoona tu matokeo yatatangwazwa baada ya siku saba nikaona utoto uke ule tu
 
Haya unayoleta wewe ni mapenzi kwa Mtu wako. Yeye ndo aliyefuatwa sirini. Kwa Mtu mwenye dhamana kubwa kama ile ulitaka atoke kesho yake atangaze, "watu wa state wamenifuata usiku tuongee kuhusu tallying". Huku ikijulikana state iko na nani?
Kitendo chake kukaa kimya na kuja kuitoa hiyo siri wakati huu pakiwepo na mgogoro kuhusu ushindi wa Ruto hapo ndio ameharibu kabisa.

Muda wake wa kutoa hiyo siri ulikuwa ni kabla ya uchaguzi kufanyika, hii ingemjengea heshima na kuaminika kwa kiti anachokitumikia, lakini ukimya wake unaonesha Chebukati ni muoga.
 
Nilivyoona tu matokeo yatatangwazwa baada ya siku saba nikaona utoto uke ule tu

Chamsingi cha kujiuliza siku zote: "hivi pesa kwa idadi ya wapiga kura inamchukua mtu mzima masaa mangapi kuzihesabu?

Ulamba asali wa shithole countries hata chembe ya soni huwa hamna.
 
Lakini pia hii hali inayotokea Kenya nikiitazama vizuri mwisho wa siku inaweza kuleta machafuko, makundi ya hao commissioners yanaweza kusababisha sintofahamu mwishowe warudie yale ya 2017.

Hapa kwetu bado tumelala, wajumbe wa tume hawana uwezo wa kuhoji yanayotokea kwenye tume ya uchaguzi, hii ni kwasababu M/kiti wa tume anateuliwa na Rais, nae mwenyekiti anateua wajumbe atakaoona wanamfaa, hawa hawawezi kugeukana.

Tofauti na Kenya, IEBC kuna wajumbe walioteuliwa na Kenyatta, ndio wale wanne waliogoma kukubali matokeo ya uchaguzi, na wakina Chebukati waliopatikana kwa utaratibu mwingine.

Salama zaidi ya hawa jirani zetu mbona ukweli mzima na ukajulikane tu? Ubakaji huu wa demokrasia ukawe fundisho pia kwa walamba asali wa kwetu.

Kuweka mambo sawa zaidi kwenye bandiko lako, ma commissioner wote ni wateuliwa wa rais kutoka katika kundi linalokuwa limeidhinishwa na jopo huru. Hapa ndipo ilipo tofauti kuu baina yetu na wao.

Kwetu wajumbe wa tume hawawezi kuhoji. Kumbuka hata kama hatimaye itabidi, mahakama ya kukimbilia huko kuna Siyami au Tigatinga?

Kimsingi kwetu hawawezi kuhoji kutokana na mustakala mzima wa katiba yenyewe.

Hapa ndipo ZZK na Propesa Muka wanapofuzu kuitwa wasaliti. Kwamba udhaifu wa katiba yetu hawauoni kuwa hata kama tume ya uchaguzi ingekuwa huru bado ni kazi bure?

Tulipo tunahitaji viongozi wenye uthubutu wa vitendo vyenye kutoa matokeo. Kwa matokeo tutawa assess kufaa au kutokufaa kwao.
 
Kitendo chake kukaa kimya na kuja kuitoa hiyo siri wakati huu pakiwepo na mgogoro kuhusu ushindi wa Ruto hapo ndio ameharibu kabisa.

Muda wake wa kutoa hiyo siri ulikuwa ni kabla ya uchaguzi kufanyika, hii ingemjengea heshima na kuaminika kwa kiti anachokitumikia, lakini ukimya wake unaonesha Chebukati ni muoga.

Wanasema huu mchezo hautaki hasira. Wengine wakisema mambo mazuri hayataki haraka au kawia ufike.

Chebukati kwa yanayojiri utetezi wake ni cast iron. Yeye alitaka haki. Yao yote hayo kwake zilikuwa kelele za chura.

Aliwapuuza katika hatua zote na hapa anachofanya ni maelezo yake ya kilichojiri ambacho hakikumuathiri yeye wala matokeo ya uchaguzi aliosimamia kama mwenyekiti wa tume.
 
Back
Top Bottom