Yabainika Wakenya wanawasajili Jamaa zao katika Bima kisha kuwaua ili wajitajirishe

Yabainika Wakenya wanawasajili Jamaa zao katika Bima kisha kuwaua ili wajitajirishe

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Imefichuka kuwa baadhi ya wakenya wanawaandikisha jamaa zao katika bima za bei ghali na kisha kuwaua ili kupokea mamilioni ya pesa zinazolipwa kama fidia na kampuni ya bima.

Ni visa ambavyo vimewashangaza wapelelezi ambao waligundua wakati wakichunguza kundi la walaghai waliovamia sekta hiyo ya bima.

Maafisa wa Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Bima (IRA) wa kuchunguza ulaghai pamoja na wapelelezi wa kibinafsi ambao wamekodishwa na wadhamini, waligundua msururu wa visa ambapo watu waliandikisha jamaa zao katika bima mbalimbali za maisha pasipo kuwafahamisha, na kisha kupanga njama ya kuwaua ili kulipwa mamilioni ya pesa za fidia kutoka kwa kampuni ya bima hizo.

Katika kisa kimoja kilichowaacha wapelelezi vinywa wazi, meneja mmoja wa zamani wa bima alimwandikia mpwa wake maskini katika bima mbili, lakini inadaiwa kuwa alipanga mauaji ya kijana huyo na kisha mwili kutupwa barabara ya Kangundo kabla ya kukimbilia kudai fidia.

Wachunguzi hao waliozungumza na TaifaLeo Jumapili, walisema Mwanamume huyo aliibua tashwishi alipotoa shinikizo chungu nzima kutaka alipwe fidia hiyo akisema alihitaji pesa za kusafiri kuelekea Australia.

Afisa huyo wa zamani wa bima, alikuwa amemchukua mpwa wake mwenye umri wa miaka 27 bima ya Sh 10 milioni na nyingine ya Sh 1milioni katika kampuni mbili tofauti. Alikuwa ametoa mchango mmoja pekee kabla ya mauaji hayo kutokea.

Mwanamume huyo alikuwa amefanikiwa kukamilisha utaratibu wa kupewa fidia ya bima ya kwanza yenye kitita kinono na alikuwa katika jitihada za kusaka idhini ya kulipwa fidia ya pili tashwishi zilipoibuka.

Kumuua mpwa wake

Ripoti ya wapelelezi ambayo Swahilihub iliona, ilimhusisha mshukiwa huyo katika mauaji ya mpwa wake, ambaye rekodi za simu zilionyesha kuwa wawili hao walikuwa pamoja muda mfupi kabla kijana kutoweka licha ya mshukiwa kukana hayo katika taarifa za kiapo.

Ripoti ya upasuaji maiti iliashiria kijana huyo alifariki kutokana na jeraha mbaya la kichwa lililosababishwa na maumivu yaliyoletwa na kifaa butu.

"Kutokana na uchunguzi, ni bayana kuwa ushahidi wa kuashiria kuwepo kwa mauaji ya kujitajirisha yanayoendelezwa na wafadhiliwa", wachunguzi hao walihitimisha katika ripoti yao ya Juni.

Jamaa huyo mshukiwa anasekana kunaswa na vyeti viwili vya kifo vya nambari mbili tofauti za usajili, ambavyo alinuia kutumia kudai fidia zingine.

Chanzo: TaifaLeo
 
Sasa hapo dawa ni kuzifutilia mbali kabisa hizo bima.

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Sasa hapo dawa ni kuzifutilia mbali kabisa hizo bima.

Post sent using JamiiForums mobile app
Hatari sana.. Unaandikishwa bila kujua na Unauliwa bila kujua kosa lake
 
Ni mtu mpumbavu tu ndiyo anaweza kujiingiza kwenye madai batili ya bima. Ulaya na America wameendelelea sana katika upelelezi wa haya mambo. Usithubutu kujiingiza kwenye madai batili. Utaumia!


Sent from my Siemens c35 dole-gumba using JamiiForums app.
 
Wakenya mkiambiwa mna roho mbaya mnatokwa povu na kuanza kuandika kiingereza hapa utadhani ndo lugha yenu.
Nyie ni zaidi ya manyang'au

Nothing is easier than blaming others for your own problems
 
Kweli wakenya ni watu lakini sio Binadamu.

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Mbona tz tupo jamaa
Rafki yangu alifungwa hogo mkononi akacheza na bima mkwanja ukatoka
Milion 1 Ye akapewa laki6
Tena hii ilikua bado awam ya benny loooong time
 
Haya mambo nayaona sana ID kwenye crime and investigation.
Moja ya motive kubwa ya watu kufanyiana mauaji uwa ni Bima na mara nyingi ukitazama IDx utakuta mme anamuua mke kwasababu ya bima au mke anamuua mme kwasababu ya bima.
Wazungu wanauna sana kwasababu ya bima
 
Ndio, ila beyond ya zinapoishia akili zenu wakenya!





Fyuuuuuuuuuuuuuu![emoji57] [emoji57] [emoji57]

Post sent using JamiiForums mobile app
Basi siwezi kukulaumu. Ndo upeo wako ulipoishia. Ila tu nikuongezee ufahamu kidogo, kwanza mimi sio mkenya. Na kusema vile nilivyosema haina maana kuwa natukuza watu wa mbele wala nini. Nilitaka tu watu wajue si kenya peke yake mambo haya yanafanyika. Zipo sehem kibao duniani.
 
Basi siwezi kukulaumu. Ndo upeo wako ulipoishia. Ila tu nikuongezee ufahamu kidogo, kwanza mimi sio mkenya. Na kusema vile nilivyosema haina maana kuwa natukuza watu wa mbele wala nini. Nilitaka tu watu wajue si kenya peke yake mambo haya yanafanyika. Zipo sehem kibao duniani.
Ukubari kuwa Kenya wamekubuhu kwa ujinga ujinga

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom