Yadhihirika: Nyama choma inasababisha kansa

Yadhihirika: Nyama choma inasababisha kansa

Hivi huwa najiuliza kama hivi vyakula vina madhara kwa nini mungu alitupa? Nyama majanga , mchele matunda mengine nayo majanga sasa tule nini.

MKuu, mwanzoni Mungu alipoumba nyama haikuwa sehemu ya chakula cha binadamu. Baadaye akaruhusu, lakini akakataza nyama kama kiti moto nk, na baadaye kabisa akaamua kila nyama ruksa!

Ila nimesoma sehemu wali unaleta kitambi, labda kweli, - naona Wanyakyusa wengi wanavyo!
 
mababu zetu zamani waliishi kwa miziz na uwindaji
hzo nyama zilikuwa zinachomwa na walikuwa wanaishi miaka mingi tu
 
140122_MEDEX_GrilledPork.jpg.CROP.promo-mediumlarge.jpg


Kwa wale tuliozoea na kupenda sana nyama choma, iwe ni ya kuku, mbuzi, ng'ombe au nyama aina nyingine, habari mbaya zinazoenea kwa kasi katika ulimwengu wa vyakula ni kwamba wanasayansi wanasema wamethibitisha kwamba uchomaji nyama unasababisha kansa ya ngozi, ini, tumbo na nyinginezo kutokana na kemikali zijulikanazo kama polycyclic aromatic hydrocarbons, moto uunguzapo nyama.

Wanasayansi wanasema huu ukweli umejulikana toka miaka ya 1960, na kwamba inatia ndani nyama za kukaushwa kwa moshi, kama vile samaki, nk.

Habari yenyewe ndiyo hiyo. Iliyobaki ni kuchagua kusuka au kunyoa.

Source:
Cancer risk from grilled meat: Is it time to give up smoked and fried foods?

Mimi naona kila chakula ni hatari hizi research nyingine bwana, sasa wameacha gout wemekuja kwenye cancer. ukila samaki sana gout, ukila nyama, gout na cancer sasa, chinese gout, utaacha kula nini? Wacha tule tu tukifa ni wakati kwani nani hatakufa?
 
Back
Top Bottom