Yafahamu magonjwa 20 ya mlipuko mabaya zaidi katika historia ya dunia

Yafahamu magonjwa 20 ya mlipuko mabaya zaidi katika historia ya dunia

Ahsante! Nadnai labda kun akity hujaelewa,,,Fuatilia vizuri kaka smallpox ilikuwepo tangu zamani sana na imekua ikipewa majina kulingana na ni wkt gani ilitokea ama jina gani litafaa zaidi. Kwa taarifa yako watu wa kwanza kuanza kufanyavaccination na smallpox ni China mnamo 1,500 na hapo iliishakuwepo kitambo sana kabla ya kuanza kufanyika hayo majaribio ya kinga.......
Unasemaje ya juzijuzi tena...

Anyway ahsante kwa kuendelea kufuatilia zaidi
Mkuu, nakubali kabisa kuwa smallpox ilikuwepo tangu zamani za kale. Lakini ilianza kushambulia kwa Kasi hivi juzi juzi tu, Kama nukuu kutoka Wikipedia inavyosema - iliua watu millioni 500 miaka 100 zilizopita kabla ya kidhibitiwa 1980.

Halafu smallpox ilikuwa si inauwa tu, ukipoona inakuacha mlemavu na kuharibu maumbile kabisa!!! Ilikuwa ni ugonjwa mmoja hatari kabisa na hoja yangu ni kwamba inastahili kupewa namba yake maalum (pamoja na majina yake tofauti) kwenye listi ya magonjwa ya mlipuko!
 
Mkuu, nakubali kabisa kuwa smallpox ilikuwepo tangu zamani za kale. Lakini ilianza kushambulia kwa Kasi hivi juzi juzi tu, Kama nukuu kutoka Wikipedia inavyosema - iliua watu millioni 500 miaka 100 zilizopita kabla ya kidhibitiwa 1980.

Halafu smallpox ilikuwa si inauwa tu, ukipoona inakuacha mlemavu na kuharibu maumbile kabisa!!! Ilikuwa ni ugonjwa mmoja hatari kabisa na hoja yangu ni kwamba inastahili kupewa namba yake maalum (pamoja na majina yake tofauti) kwenye listi ya magonjwa ya mlipuko!
OK nashukuru kwa kwenda sawa kwenye historia kwamba smallpox sio ya juzijuzi it is dated as far from 3rd century BC........
Sasa tusonge mbele kwenye swala lao kwamba kwa nn baujapewa upekee wa kulielezea?
Ukiingia mitandaoni kuna quite different classifications za pandemics na epidemics. Hiyo orodha yangu imejiweka zaidi kwenye time sequence tangu mlipuko wa zamani zaidi mpaka mlipuko wa sasa..... Sababu moja wapo ya kutoiweka smallpox ni historia yake kua ugonjwa ulianza lini hivo kuwa mgumu kuuweka kwenye orodha yangu....

Check👇👇
Thousands of years ago, variola virus (smallpox virus) emerged and began causing illness and deaths in human populations, with smallpox outbreaks occurring from time to time. Thanks to the success of vaccination, the last natural outbreak of smallpox in the United States occurred in 1949. In 1980, the World Health Assembly declared smallpox eradicated (eliminated), and no cases of naturally occurring smallpox have happened since.


Ndio maana pia hujaona historia ya ugonjwa km Hepatitis ambao uliathiri zaidi ya watu milioni 500 na kuua watu milioni 1 kila mwaka
 
OK nashukuru kwa kwenda sawa kwenye historia kwamba smallpox sio ya juzijuzi it is dated as far from 3rd century BC........
Sasa tusonge mbele kwenye swala lao kwamba kwa nn baujapewa upekee wa kulielezea?
Ukiingia mitandaoni kuna quite different classifications za pandemics na epidemics. Hiyo orodha yangu imejiweka zaidi kwenye time sequence tangu mlipuko wa zamani zaidi mpaka mlipuko wa sasa..... Sababu moja wapo ya kutoiweka smallpox ni historia yake kua ugonjwa ulianza lini hivo kuwa mgumu kuuweka kwenye orodha yangu....

Check👇👇
Thousands of years ago, variola virus (smallpox virus) emerged and began causing illness and deaths in human populations, with smallpox outbreaks occurring from time to time. Thanks to the success of vaccination, the last natural outbreak of smallpox in the United States occurred in 1949. In 1980, the World Health Assembly declared smallpox eradicated (eliminated), and no cases of naturally occurring smallpox have happened since.


Ndio maana pia hujaona historia ya ugonjwa km Hepatitis ambao uliathiri zaidi ya watu milioni 500 na kuua watu milioni 1 kila mwaka
Mkuu, kama historia ya smallpox haijaeleweka, kwa nini usiiweke kwenye prehistoric kama ulivyoweka ile Nr.1 ya China au kwenye fungu ya magonjwa yenye utata kihistoria? Kumbuka maada inazungumzia "Yafahamu magonjwa 20 ya mlipuko mabaya zaidi katika historia ya dunia"
 
Mkuu, kama historia ya smallpox haijaeleweka, kwa nini usiiweke kwenye prehistoric kama ulivyoweka ile Nr.1 ya China au kwenye fungu ya magonjwa yenye utata kihistoria? Kumbuka maada inazungumzia "Yafahamu magonjwa 20 ya mlipuko mabaya zaidi katika historia ya dunia"
Ahsante kwa mawazo ndio maana pia nimezunhumzia Hepatitis ambayo ilikua so deadly lkn haipo kwenye orodha yangu kwa mujibu wa muktadha wa namna niliyochagua kuwasilisha. Huwezi kuweka prehistoric km ilivo kwa PREHISTORIC EPIDWMIC:3000B.C. Kumbuka kua miaka ya B.C inahesabika kurudi nyuma which means 3000B.C is from 1B.C to 3000B.C hayo sio makadirio bali ni exact years. Sasa smallpox hizo thousands of years B.C utaandika ilianza 1B.C mpaka lini hapo ndipo shida ilipo mkuu....
 
Hivi kati ya Ebola na corona mpaka sasa kipi kilichokua na athari zaidi mpaka sasa?

Sent using Jamii Forums mobile app
Covid-19 ina athari zaidi lkn bado hatujafikia kufanya angalau conclusion ya maambukizi na vifo yaani tunavoongea ndio imepemba moto....huko ulaya na marekani ni vifo vya kutisha kila siku......
 
Ahsante kwa mawazo ndio maana pia nimezunhumzia Hepatitis ambayo ilikua so deadly lkn haipo kwenye orodha yangu kwa mujibu wa muktadha wa namna niliyochagua kuwasilisha. Huwezi kuweka prehistoric km ilivo kwa PREHISTORIC EPIDWMIC:3000B.C. Kumbuka kua miaka ya B.C inahesabika kurudi nyuma which means 3000B.C is from 1B.C to 3000B.C hayo sio makadirio bali ni exact years. Sasa smallpox hizo thousands of years B.C utaandika ilianza 1B.C mpaka lini hapo ndipo shida ilipo mkuu....
Bado nipo tu, samahani kwa kuchosha!

Unasema "Sasa smallpox hizo thousands of years B.C utaandika ilianza 1B.C mpaka lini hapo ndipo shida ilipo mkuu", lakini mbona kwenye historia wamegawa timeline kabla ya BC vizuri tu katika Stone Age, Bronze Age, Iron Age, nk. Kwa hiyo kama umeweka listi yako kwenye timeline, unaweza kusema smallpox ilianza kwenye Bronze Age na inaeleweka kuwa ni zamani sana.

Hepatitis sio ugonjwa wa mlipuko, lakini kama imeuwa watu wengi, inatakiwa kuorodheshwa kwenye listi ya magonjwa hatari!
 
Bado nipo tu, samahani kwa kuchosha!

Unasema "Sasa smallpox hizo thousands of years B.C utaandika ilianza 1B.C mpaka lini hapo ndipo shida ilipo mkuu", lakini mbona kwenye historia wamegawa timeline kabla ya BC vizuri tu katika Stone Age, Bronze Age, Iron Age, nk. Kwa hiyo kama umeweka listi yako kwenye timeline, unaweza kusema smallpox ilianza kwenye Bronze Age na inaeleweka kuwa ni zamani sana.

Hepatitis sio ugonjwa wa mlipuko, lakini kama imeuwa watu wengi, inatakiwa kuorodheshwa kwenye listi ya magonjwa hatari!
Ok sawa Kaka na ahsante kwa mawazo Ila unalazimisha sn kitu ambacho sio sahihi..........km kuna kitu unataka ni ruhusa kuandaa orodha nyingine km ipo na kwa muktadha utakaokua umeuzingatia.....hiyo hapo huwezi kuchomekea km ww unavoshauri....
 
Conspiracists watasema yalikiwa ni bio weapons au yalisababishwa na Babu yake Bill Gates.
 
Swali: Vipi kuhusu lockdown kipindi hicho....Hayo maradhi yaliondokaje duniani....Athari zake kwa Afrika ilikuaje?
 
Awali ya yote napenda kutoa pole nyingi kwa Watz walioathirika na hili gonjwa kwa namna moja ama nyingine huku wakiendelea kupambana na Ugonjwa wa Corona kila mtu kwa staili yake tukiwa tumepoteza mwelekeo hasa baada ya wataalamu na wanasiasa nchini kutofautiana katika mbinu za kukabiliana na janga hili. Mungu aendelee kutunusuru na kadhia hii. AMINA.

Leo nawaletea orodha ya magonja ya mlipuko yaliyowahi kutikisa eneo Fulani la dunia ama dunia nzima (yaani Epidemics and Pandemics). Nyakati za nyuma inaonesha mababu zetu walishambuliwa mara kwa mara na ugonjwa wa Tauni. Hii ni kukumbushana na kutiana moyo kua haya tunayopitia yamewahi kuikumba dunia huko nyuma kwa hiyo Corona sio ugonjwa wa kwanza hatari wa mlipuko.

1. Prehistoric epidemic: Circa 3000 B.C
Huu ni ugonjwa hatari wa TAUNI uliotokea huko Kaskazini Mashariki mwa China na kuangamiza kijiji kizima cha Prehistoric. Inasemekana ugonjwa ulikuja ghafla yaani kwa haraka sana kiasi kwamba haikuwezekana hata kufanya taraibu nzuri za mazishi kwa waliofariki, wengi wao wakizikwa katika makaburi ya pamoja.

2. Plague of Athens: 430 B.C
Huu ni ugonjwa mwingine wa Tauni uliolipuka huko Athens Ugiriki na kutesa kwa miaka 5 ukiua zaidi ya watu 100,000. Watu wenye afya zao walishambuliwa na joto kali la ghafla, macho kuwasha sana, na kujaa na kutoka damu kwenye koromeo na mdomoni,

3. Antonine Plague: A.D. 165-180
Hii ni Tauni nyingine iliyojitokeza na kujizolea umaarufu wa kuua watu wengi wakati wanajeshi waliporejea kwenye Himaya ya Rumi wakitoka vitani. Inasemekana hili gonjwa liliua zaidi ya watu milioni 5.

4. Plague of Cyprian: A.D. 250-271
Tauni ya wakati huu ilitikisa kiasi cha kuwaibua viongozi mbalimbali wakiwemo wa dini. Hapa ndipo Askofu huyu Cyprian wa Tunisia (Hatimaye jina lake kupewa ugonjwa) aliuelezea ugonjwa wa Tauni kama dalili za wazi za MWISHO WA DUNIA. Inaaminika uliua watu 5,000 kila siku kwa mji wa Roma pekee.

5. Plague of Justinian: A.D. 541-542
Hii Tauni ilipewa jina la Justinian Mtawala wa Himaya ya Byzantine. Hili lilikua ni eneo mashariki mwa Roman Empire ambayo ni maeneo ya Instanbul ya sasa. Inakadiriwa kua 10% ya watu duniani kote walikufa wakati huo.

6. The Black Death: 1346-1353
Ugonjwa huu uliosababishwa na bacteria na ulisambaa kutoka bara la Asia mpaka Ulaya. Inasemekana uliua 60% ya watu wote Ulaya yaani iliua takribani watu milioni 65 Ulaya nzima ndani ya muda huo wa miaka 7.

7. Cocoliztli epidemic: 1545-1548
Huu ni ugonjwa uambao dalili zake zilikua homa kali, homa ya matumbo na kutokwa damu. Hii ilitokea huko Mexico na Amerika ya kati ikiua watu zaidi ya milioni 15.

8. American Plagues: 16th century
Ni Tauni inayosemekana ililetwa na Wapelelezi kutoka Ulaya. Inakadiriwa kua 90% ya Wamarekani asili upande wa magharibi walipoteza maisha.

9. Great Plague of London: 1665-1666
Baada ya Black Death ikaja tauni nyingine iliyoshambulia England. Vijidudu vya Ugonjwa huu inasemekana vilibebwa na panya huku takataka na uchafu hasa maeneo ya watu masikini ikiwa ndio chanzo kikuu cha kusambaa kwa ugonjwa. Mji wa Landon ukiwa ndio kitovu cha maambukizi walikufa watu wengi sana na kupelekea wale wenye uwezo km Madaktari, Wanasheria, Wafanyabiashara akiwemo Mfalme Charles waliikimbia London wakiwaacha watu masikini. Huu ugonjwa uliua 15% ya watu wa London huku jumla kuu ya vifo ikiwa watu 100,000. (Hii ya kukimbia London imenifanya nimkumbuke MEKO).

10. Great Plague of Marseille: 1720-1723
Kumbukumbu za kihistoria zinaonesha kua ugonjwa huu ulijitokeza pale meri iliyokuwa ikiitwa Grand-Saint-Antoine ilipotua pwani ya mji wa Marseille Ufaransa ikiwa imebeba shehena ya mizigo kutoka mashariki mwa Mediterania. Kwa haraka kabisa Tauni ikasambaa kwa kasi ya ajabu na nadni ya miaka 3 ikawa imeuma watu takribani 100,000 huku mji wa Marseille pekee ukirekodi 30% ya raia wa mji huo walikua wamefariki.

11. Russian plague: 1770-1772
Hii Tauni ilishika moto kwa kasi zaidi katika mji wa Moscow baada ya watu waliowekwa karantini kuanzisha vurugu na kukimbilia nje. Hii ikapelekea hadi kuuwawa kwa Askofu mkuu Ambosius ambaye alikuwa akishawishi watu kutokukusanyika kwa ajili ya sala. Mpaka ugonjwa unakoma ulikua umeua takribani watu 150,000.

12. Philadelphia yellow fever epidemic: 1793
Wakati homa ya manjano ikiwa imeisha pale Philadelphia Marekani, viongozi walifikia hatua ya kudhani kua watumwa hasa weusi walikua na kinga imara dhidi ya magonjwa. Kutokana na Imani hiyo wakawaita watu wenye asili ya Afrika ili kufanya kazi ya kuuguza wagonjwa. Hii ilikua kama kuwasha moto wa petroli. Ugonjwa huu uliokuwa unasambazwa na mbu ukalipuka kwa kasi sana na kuua watu 5,000.

13. Flu pandemic: 1889-1890
Visa vya awali kabisa vya haya mafua viligundulika Russia. Ugonjwa ukasambaa kuanzia St Petersburg kabla ya kusambaa kwa haraka kuelekea Ulaya na dunia nzima. Hii ni pamoja na ukweli kwamba usafiri wa anga ulikua haupo kipindi hicho. Ndani ya miezi michache tu ukawa umepiga dunia nzima na ilichukua wiki 5 tu kufikia kilele cha maambukizi ukiua watu milioni 1 dunia nzima.

14. American polio epidemic: 1916
Ugonjwa wa Polio uligundulika katika jiji la New York City ukisababisha watu 27,000 kuugua huku vifo vikiwa 6,000 ndani ya U.S. Huu ni ugonjwa ambao wahanga wakuu ni watoto. Polio iliendelea kuwatesa Wamarekani mpaka chanjo ilipopatikana mnamo mwaka 1954.

15. Spanish Flu: 1918-1920
Inasemekana huu ni moja kati ya milipuko ya magonjwa mibaya zaidi kuwahi kuikumba dunia ambapo inakadiriwa kuwa watu milioni 500 waliathirika kuanzia Bahari ya kusini mpaka kizio cha kaskazini huku ikikadiriwa kua 1/5 ya watu walioathirika walipoteza maisha.

16. Asian Flu: 1957-1958
Hii Flu ilikua ni aina nyingine ya ugonjwa hatari ukiiathiri dunia. Ulioanzia huko Asia hususani nchini China ambapo zaidi ya watu milioni 1.1 waliuawa na ugonjwa huu huku vifo 116,000 vikitokea Marekani pekee.

17. AIDS pandemic and epidemic: 1981-present day
Tangu UKIMWI ulipogundulika kwa mara ya kwanza unakadiriwa kua umeshaua zaidi ya watu milioni 35 mpaka sasa. Inaaminika kwamba ugonjwa huu ulitengenezwa kutoka kwa nyani na kupandikizwa kwa binadamu huko Afrika Magharibi mnamo mwaka 1920. Kwa sasa 64% ya watu milioni 40 ambao wanaishi na virusi vya ukimwi wanatokea kusini mwa jangwa la Sahara.

18. H1N1 Swine Flu pandemic: 2009-2010
Hii flu ya 2009 ilisababishwa na H1N1 (H na N ni aina mbili za protini zinazounda kirusi kinachoshambulia cell za mwili) ambayo iligundulika huko Mexico kabla ya kusambaa sehemu nyingine za dunia. Ndani ya mwaka mmoja ilikua imeathiri jumla ya watu milioni 1.4 duniani huku ikiua watu takribani 500,000 kwa mujibu wa CDC.

19. West African Ebola epidemic: 2014-2016
Ebola ilipiga Afrika kwa mara ya kwanza kati ya 2014 na 2016, ambapo watu 29,000 waliathirika huku 12,000 kati ya hao wakipoteza maisha. Kisa cha kwanza kabisa kiligundulika Guinea mnamo Desemba 2013, baadae ugonjwa ukasambaa kwa kasi na kiwango kikubwa kabisa kuelekea Liberia na Sierra Leone. Kiasi kikubwa cha maambukizi kilitokea katika hizo nchi tatu huku nchi zingine chache zikiwa na visa vichache vya maambukizi na vifo. Inasemekana asili ya virusi hivi ni kutoka kwa POPO.

20. Zika Virus epidemic: 2015-present day
Madhara ya mlipuko wa Zika huko Amerika ya Kati na Amerika ya Kusini bado hayajajulikana bayana mpaka sasa. Virusi vya Zika vinasambazwa na Mbu ambao wanapenda Zaidi hali ya hewa na joto na unyevunyevu mwingi na hivyo kuifanya Amerika Kusini, Kati na sehemu ya Kusini mwa Marekani kua kitovu cha maradhi haya.

JE, KUNA CHA KUJIFUNZA KATIKA HIZTORIA HII? NIAMBIE UMEJIFUNZA NINI.

Imeandaliwa na Jile79, Kwa msaada wa mtandao.

Note: Babu yangu angekuwa hai ningemshirikisha na kumhoji ili kupata angalau picha waliishije wakati wa majanga haya makubwa.

Nilichojifunza : Time interval ya ugonjwa mmoja kwenda mwengine inapungua kila miaka inavyozidi kupanda
(Uartificial unatutafuna)
 
Nilichojifunza : Time interval ya ugonjwa mmoja kwenda mwengine inapungua kila miaka inavyozidi kupanda
(Uartificial unatutafuna)
Asante kwa kutafiti......kwa hiyo ina maana miaka ya mbeleni tutaanza kupata mangonjwa ya mlipuko mara kwa Mara?
 
Ok sawa Kaka na ahsante kwa mawazo Ila unalazimisha sn kitu ambacho sio sahihi..........km kuna kitu unataka ni ruhusa kuandaa orodha nyingine km ipo na kwa muktadha utakaokua umeuzingatia.....hiyo hapo huwezi kuchomekea km ww unavoshauri....
Nia yangu ilikuwa si kukukwaza bali kuelimishana!
Unaleta mada isemayo "Yafahamu magonjwa 20 ya mlipuko mabaya zaidi katika historia ya dunia" na ina maelezo ambayo ni factually incorrect! Mara unasema :
"Kwa hiyo kwenye andiko langu ugonjwa wa hapo juu Antonine Plague na American Plagues yalikuwa related na smallpox...." na "Hiyo orodha yangu imejiweka zaidi kwenye time sequence tangu mlipuko wa zamani zaidi mpaka mlipuko wa sasa"!

Hakuna ugonjwa wa mlipuko hatari iliyowahi kutokea duniani kama smallpox, na haijatajwa kwenye orodha lako!

Samahani kama nimekukwaza! I'll ignore you from here on!
 
Nia yangu ilikuwa si kukukwaza bali kuelimishana!
Unaleta mada isemayo "Yafahamu magonjwa 20 ya mlipuko mabaya zaidi katika historia ya dunia" na ina maelezo ambayo ni factually incorrect! Mara unasema :
"Kwa hiyo kwenye andiko langu ugonjwa wa hapo juu Antonine Plague na American Plagues yalikuwa related na smallpox...." na "Hiyo orodha yangu imejiweka zaidi kwenye time sequence tangu mlipuko wa zamani zaidi mpaka mlipuko wa sasa"!

Hakuna ugonjwa wa mlipuko hatari iliyowahi kutokea duniani kama smallpox, na haijatajwa kwenye orodha lako!

Samahani kama nimekukwaza! I'll ignore you from here on!
JF ni sehemu ya kuelimishana na kujifunza mkuu japo sio ubishi sio wa lazima kwa hiyo usihofu tuendelee kujadili. Kuhusu swali lako tena maana wewe unaamini small pox ni mlipuko wa hatari uliowahi kutokea duniani. Kwa taarifa yako ili mlipuko uonekane ulikua hatari hauangaliwi kwa idadi ya watu waliokufa bali inaangaliwa rate ya kuua watu wengi kwa muda mfupi. Mfano wako wa wikipedia ni kua smallpox iliua watu 500mil kwa muda wa miaka 100 (ikiwa na maana watu mil 5 kwa mwaka, sasa kwa taarifa yako magonjwa km Heart Disisese (iliyoua watu 9mil kwa mwaka mmoja) na Stroke (iliyowahi kuua watu 6.5mil kwa mwaka) ndio most deadly. Hata death rate ya Black Death ilikuwa kubwa by far kuliko hiyo smallpox ambayo ilikuwepo "thousands of years". Karne ya 18 death rate ye smalpox was just watu 400,000 kwa mwaka.
 
Conspiracists watasema yalikiwa ni bio weapons au yalisababishwa na Babu yake Bill Gates.
Watu hawapendi wala hawataki kabisa kujihangaisha.......Hawataki kuchanganya na za kwao!!
 
Swali: Vipi kuhusu lockdown kipindi hicho....Hayo maradhi yaliondokaje duniani....Athari zake kwa Afrika ilikuaje?
Ni swali pana sana maana kila ugo0njwa walideal nao kulingana na jinsi ulivokua except hiyo Prehistoric Epidemic ambayo iliua kijiji kizima... lkn kwa sehemu kubwa magonja mengi either miji iliwekwa lockdown au walikua wanawatenga wagonjwa husika.

Mifano:
1. Plague of Justinian: Watu walikua wanawakimbia waliokua wanaumwa maana iliua nusu ya population ya dunia. Inasemekana waliopona ni wale tu waliokua na immune ya kutosha kukabiliana na maradhi yale.

2. The Black Death: Pamoja na lockdown, Wageni walilazimishwa kuwekwa kwenye isolation kwa muda wa mpaka siku 40 au quarantino (ndio chimbuko la neno Quarantine) ili kuprove kua hawakua na maambukizi.

3. The Great Plague of London: Hawa walipiga marufuku public gatherings na entertainments alafu waliwekeza sana kwenye utaratibu wa separate and isolate lakini walienda mbele zaidi kwa kuziwekea alama fulani nyumba zote ambazo zilikuwa na waathirika wa ugonjwa, madirisha yaliwekwa alma ya msalaba mwekundu yakiwa na maandishi "MUNGU UTUREHEMU". Kama ilipolazimika mtu kutoka nje ya nyumba kwa dharura basi alilazimika kushika fimbo nyeupe ili kuonyesha jamii kuwa ni mwathirika wa ugonjwa ili wakae nae mbali.

4. Smallpox: Inasemekana watu wa mexico na marekani ambako ndiko chimbuko la ugonjwa hawakua na immunity kabisa ya kupambana na gonjwa hili hivyo kufagia watu wengi sana. Kilichonurusu watu ni baada ya kupatikana chanjo na inasemekana huu ndo ugonjwa wa kwanza kudhibitiwa kwa chanjo.

5. Chorela: Hii ni maswala ya usafi zaidi, kuweka mifumo mizuri ya maji taka, kuwa na maji safi na salama ya kunywa nk ndio udhibiti wa Chorela.

Mkuu yapo mengi unaweza kufuatilia zaidi lkn angalau unaweza kupata picha namna gani walipambana na HALI ZAO
 
Pampja na kwamba Covid-19 inatisha na bado hatujamaliza hata mwaka lkn speed yake ni ya kawaida. Kwa muda wa miezi sita sasa tangu ilipuke, waliothirika ni milioni 3 tu huku vifo vikiwa 350,000 duniani kote
 
Bado imbombo ngafuu.....
 
Back
Top Bottom