Yahusu kula chumvi nyingi

Yahusu kula chumvi nyingi

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Lakini, chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu.

Umuhimu wa chumvi katika maisha
Ndio kiungo pekee kinachotumiwa na na asilimia 99.99 na wanadamu wote duniani.. Ndio kiungo kwenye chakula muhimu zaidi kinachonogesha na kuleta ladha kwenye chakula.

Chumvi haiharibiki. Lakini, ikiharibika inafanywa nini?
Haifai tena kabisa bali hutupwa barabarani na kukanyagwa na watu. Je, kwenye maisha yako umeshawahi kuona chumvi iliyoharibika na kutupwa? Jibu laweza kuwa hapana kwakuwa chumvi haiharibiki.

Mojawapo ya kazi za chumvi ni kuzuia kuoza na kuharibika
Kama vile chumvi ilivyo na umuhimu kwa wanadamu, ndivyo hivyo hivyo huweza kukufanya kiroho ukawa na umuhimu wa wengine
Waswahel hawasemi fulani kala sukari nyingi la hasha bali husema kala chumvi nyingi! Ni kwasababu ya umuhimu wake mwilini.

Unaweza ukamaliza siku bila kula sukari lakini sio chumvi. Watu wenye umri mkubwa huambiwa wamekula chumvi nyingi kwa maana ya kwamba katika umri wao wameona mengi na mengine mengi.

Ukila sukari nyingi Maisha yako yatakuwa mafupi sana, lakini sio chumvi!
Maisha ni changamoto na changamoto ndio chumvi inayokujenga na kukufanya imara zaidi. Ukomavu wa akili hauletwi na shangwe na karamu(sukari) bali changamoto na mitikisiko ya maisha.

Vidole vyako ndio changamoto zako za maisha. CHUMVI na kucha zako ndio starehe zako katika maisha!SUKARI..!! Si unaona ilivyo rahisi kukosa ukucha kuliko kukosa kidole?

Ulemavu wa kukosa kucha hauwezi kufanana kamwe na ulemavu wa kukosa vidole! Unajua ni kwanini? Kucha ziko kwenye vidole kama vile tu shangwe zilivyo kwenye changamoto na chumvi inavyotumika zaidi kuliko sukari.

IMG-20210610-WA0078.jpg
 
Maneno yako yamejikita ktk msingi 'dhana halisi ya maisha tunayoishi.

Maisha yana ladha yake halisi japo kila mmoja anaweza kuihisi Kwa namna yake kutokana na anachokula.

Watumiaji wa sukari ni vigumu kwao kuvuka balehe ya tatu wakiwa na utimamu sahihi akili japo miili yao huonekana inanguvu zisizo wasaidia.

Changamoto hutujenga japo Kwa ladha yake ni wachache wenye kustahmili.
 
Maneno yako yamejikita ktk msingi 'dhana halisi ya maisha tunayoishi.

Maisha yana ladha yake halisi japo kila mmoja anaweza kuihisi Kwa namna yake kutokana na anachokula.

Watumiaji wa sukari ni vigumu kwao kuvuka balehe ya tatu wakiwa na utimamu sahihi akili japo miili yao huonekana inanguvu zisizo wasaidia.

Changamoto hutujenga japo Kwa ladha yake ni wachache wenye kustahmili.
Watumiaji wa sukari ni vigumu kwao kuvuka balehe ya tatu wakiwa na utimamu sahihi akili japo miili yao huonekana inanguvu zisizo wasaidia.[emoji1545][emoji1545][emoji1545][emoji1545]
 
"Lakini, chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu".Magufuli alikuwa ni chumvi iliyooza.
Mungu wangu! Yani wewe na kayafa[emoji848][emoji3064][emoji3][emoji3]
 
YESU aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Nyinyi ndio chumvi ya dunia.” (Mathayo 5:13) Nao Waarabu husema kwamba, “Kuna chumvi kati yetu,” na Waajemi husema kuhusu “asiye wa kweli kwa chumvi” (asiye mwaminifu au asiye na shukrani). Kwa kuwa chumvi inaweza kuhifadhi vitu, neno “chumvi” limeheshimiwa na kustahiwa katika lugha za kale na hata za leo.

Chumvi pia imekuwa alama ya uthabiti na udumifu. Hiyo ndiyo sababu, katika Biblia agano muhimu liliitwa “agano la chumvi,” na wale waliokubaliana mara nyingi walikula mlo pamoja, uliotiwa chumvi ili kuidhinisha agano hilo. (Hesabu 18:19) Chini ya Sheria ya Musa, chumvi ilitiwa kwenye matoleo madhabahuni, bila shaka ikionyesha hali ya kutokuwa na ufisadi au uharibifu wowote.

Jr[emoji769]
 
Years of total sacrifices and hardships
FB_IMG_1624202478050.jpg
 
Lakini, chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu.

Umuhimu wa chumvi katika maisha
Ndio kiungo pekee kinachotumiwa na na asilimia 99.99 na wanadamu wote duniani.. Ndio kiungo kwenye chakula muhimu zaidi kinachonogesha na kuleta ladha kwenye chakula.

Chumvi haiharibiki. Lakini, ikiharibika inafanywa nini?
Haifai tena kabisa bali hutupwa barabarani na kukanyagwa na watu. Je, kwenye maisha yako umeshawahi kuona chumvi iliyoharibika na kutupwa? Jibu laweza kuwa hapana kwakuwa chumvi haiharibiki.

Mojawapo ya kazi za chumvi ni kuzuia kuoza na kuharibika
Kama vile chumvi ilivyo na umuhimu kwa wanadamu, ndivyo hivyo hivyo huweza kukufanya kiroho ukawa na umuhimu wa wengine
Waswahel hawasemi fulani kala sukari nyingi la hasha bali husema kala chumvi nyingi! Ni kwasababu ya umuhimu wake mwilini.

Unaweza ukamaliza siku bila kula sukari lakini sio chumvi. Watu wenye umri mkubwa huambiwa wamekula chumvi nyingi kwa maana ya kwamba katika umri wao wameona mengi na mengine mengi.

Ukila sukari nyingi Maisha yako yatakuwa mafupi sana, lakini sio chumvi!
Maisha ni changamoto na changamoto ndio chumvi inayokujenga na kukufanya imara zaidi. Ukomavu wa akili hauletwi na shangwe na karamu(sukari) bali changamoto na mitikisiko ya maisha.

Vidole vyako ndio changamoto zako za maisha. CHUMVI na kucha zako ndio starehe zako katika maisha!SUKARI..!! Si unaona ilivyo rahisi kukosa ukucha kuliko kukosa kidole?

Ulemavu wa kukosa kucha hauwezi kufanana kamwe na ulemavu wa kukosa vidole! Unajua ni kwanini? Kucha ziko kwenye vidole kama vile tu shangwe zilivyo kwenye changamoto na chumvi inavyotumika zaidi kuliko sukari.

View attachment 1814299wee Mshana...​
 
Back
Top Bottom